< Job 9 >

1 Then answered Job, and said,
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Truly I know that it is so: and how could a mortal be righteous before God?
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 If he were desirous to enter into a contest with him, he could not give him one answer out of a thousand.
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 He is wise of heart, and mighty in strength: who hath hardened himself against him, and escaped unscathed?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 [He it is] who removeth mountains, and they know it not, yea, when he overturneth them in his anger;
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 Who shaketh the earth loose out of her place, that her pillars tremble;
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 Who speaketh to the sun, and he shineth not, and around the stars he placeth a seal;
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 Who spread out the heavens by himself alone, and treadeth upon the hillocks of the sea;
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 Who made the Bear, Orion, and the Pleiades, and the chambers the south;
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 Who doth great things which are quite unsearchable, and wonders which are quite without number.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Lo, were he to go past by me, I should not see him; and were he to pass along, I should not perceive him.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 Behold, were he to snatch aught away, who could hold him back? who would say unto him, What dost thou?
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 God will not withdraw his anger: beneath him sink down the helpers of the proud.
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 How much less then could I answer him, and select my words [to contend] with him?
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 Whom, were I even righteous, I could not answer? to him that condemneth me I could [only] make supplication.
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 Or were I to call, and he would answer me, I could yet not believe that he would give ear unto my voice—
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 He that bruiseth me with [his] tempest, and multiplieth my wounds without a cause.
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 He suffereth me not to recover my breath; but feedeth me overmuch with bitter things.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 If it regard strength, lo, he is the powerful; and if justice, who will cite him for me to appear?
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 If I were righteous even, my own mouth would condemn me: were I innocent, it would still prove me perverse.
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 I am innocent; I will not have regard for myself: I will despise my life.
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 One thing is [certain], therefore have I said it, The innocent and the wicked he bringeth to their end.
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 If a scourge should slay suddenly, he will mock at the trial of the guiltless.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 Is a land given up into the hand of the wicked? he covereth the faces of its judges: if this be not the truth, who is it then?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 And my days pass swifter than a runner: they flee away, they see no happiness,
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 They hasten along like pirate ships: like the eagle that stoopeth down upon his food.
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 If I say, I will forget my complaint, I will leave off my sorrowful countenance, and recover my cheerfulness:
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 O then would I be in dread of all my pains; I know that thou wilt not declare me innocent.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 I must ever be guilty: why then should I fatigue myself for nought?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 If I were to wash myself in snow-water, to cleanse myself in the purity of my hands:
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 Even then wouldst thou plunge me in the ditch, that my own clothes would render me abhorred.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 For he is not a man, like me, that I could answer him, that we should enter together into a contest.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 There is no one who can decide between us, who could lay his hand upon us both.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Let him but remove from me his rod, and let not his dread terrify me:
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 Then would I speak, and not fear him; for the like I feel not within me.
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.

< Job 9 >