< Job 40 >
1 And the Lord addressed Job, and said,
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Will he that contendeth with the Almighty yet find fault? him that reproveth God answer this.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Then answered Job the Lord, and said,
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Behold, I am too vile: what shall I answer thee? my hand do I place on my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Once have I spoken; but I will not answer: yea, twice; but I will not repeat it again.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Then answered the Lord unto Job out of the storm-wind, and said,
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Do but gird up like a mighty man thy loins: I will ask thee, and do thou inform me.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Wilt thou indeed annul my decree? wilt thou condemn me, in order that thou mayest appear righteous?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 But if thou hast an arm like God, or if thou canst thunder loudly like him:
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Then do deck thyself with excellence and greatness, and clothe thyself in majesty and glory.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Scatter abroad the ragings of thy wrath, and look on every proud one, and humble him.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Look on every proud one, and bend him low; and tread down the wicked in their place.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust altogether: bind up their faces in concealment.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then will I also myself praise thee, when thy own right hand hath helped thee.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Only behold Behemoth, which I made near thee: grass he eateth like the ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Only see, [how great] is his strength in his loins, and his force, in the muscles of his belly.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 He stretcheth out his tail like a cedar: the sinews of his loins are closely wrapped together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are like pipes of brass: his frame is like bars of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is the first in rank of the works of God: he that made him can alone bring his sword near unto him.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 But truly the mountains bear for him his food, and all the beasts of the field play there.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Under shady trees he lieth down, in the covert of the reeds, and swamp.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Shady trees cover him as his shadow: willows of the brook encompass him about.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Behold, a river sweepeth violently along, but he hasteneth not away: he remaineth quiet, though a Jordan rusheth up to his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Can one catch him before his eyes? pierce his nose by means of snares?—
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?