< Job 33 >

1 Therefore do thou but hear, O Job, my speeches, and give ear to all my words.
Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
2 Behold now, I have opened my mouth, my tongue speaketh in my mouth.
Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
3 Out of my straightforward heart [come] my sayings, and my lips utter knowledge clearly.
Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
4 The spirit of God hath made me, and the breath of the Almighty giveth me life.
Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
5 If thou canst, answer me, array thyself before me, stand forward.
Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
6 Behold, I am in the same relation as thyself toward God: I myself also am cut out of the clay.
Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
7 Behold, dread of me cannot terrify thee, and my pressure will not be too heavy upon thee.
Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
8 But thou hast said before my ears, and the sound of the words I still hear,
Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
9 “I am pure without transgression, I am quite clean; and there is no iniquity in me:
'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
10 Yet, behold, he findeth hateful backsliding on me, he regardeth me as an enemy unto him;
Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
11 He putteth my feet in the stocks, he watcheth all my paths.”
Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
12 Behold, In this thou art not just: I will answer thee; for God is far greater than a mortal.
Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
13 Why dost thou contend against him? for with all his words will he not give an answer.
Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
14 For God speaketh once, yea twice: [yet man] regardeth it not.
Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
15 In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falleth upon men, in slumbers upon the couch:
Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
16 Then doth he lay open the ear of men, and sealeth it with their warning;
basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
17 To remove the son of earth [from his intended] deed and he covereth up pride from man;
kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
18 He withholdeth his soul from the pit, and his life from passing away by the sword.
Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
19 And so is he admonished by pain upon his couch, and all his bones with violent [aches].
Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
20 So that his inclination abhorreth bread, and his soul, the most agreeable food.
ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
21 His flesh is consumed away, that it cannot be seen, and his bones that were not seen stick out.
Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
22 Yea, his soul draweth near unto the pit, and his life to those that slay.
Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
23 If there be now about him one single angel, as defender, one out of a thousand, to tell for man his uprightness:
Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
24 Then is he gracious unto him, and saith, Release him from going down to the pit, I have found an atonement.
na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
25 His flesh becometh full again as in youth: he returneth to the days of his boyhood.
kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
26 He will offer his entreaty unto God, and he will receive him in favor, that he may see his face with joy: so doth He recompense unto the mortal his righteousness.
Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
27 He then should assemble men around, and say, “I had sinned, and perverted what is right, yet have I not received a like return.”
Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
28 Thus he redeemeth his soul from passing into the pit, and his life will look joyously on the light.
Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
29 Lo, all these things doth God two or three times with man;
Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
30 To bring back his soul from the pit, that she may shine in the light of life.
kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
31 Listen well, O Job, hearken unto me: keep silence, and I will truly speak.
Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
32 If thou hast any words, answer me: speak, for I wish to justify thee.
Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
33 If not, hearken thou unto me: keep silence, and I will teach thee wisdom.
Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”

< Job 33 >