< Job 32 >

1 So had these three men abstained from answering Job; because he was righteous in his own eyes.
Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
2 Thereupon was kindled the wrath of Elihu the son of Barachel the Buzite, of the family of Ram: against Job was his wrath kindled, because he had declared himself more righteous than God.
Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
3 And against his three friends was his wrath kindled; because they had found no answer, and yet had condemned Job.
Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
4 Now Elihu had held back toward Job [his] words; because the others were older in days than he.
Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
5 But when Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, then was his wrath kindled.
Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
6 And Elihu the son of Barachel the Buzite commenced, and said, Young am I in days, and ye are very old: therefore I hesitated and feared to show you what I know.
Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
7 I had said, Days shall speak, and multitude of years shall make wisdom known.
Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
8 But it is the spirit in man, and the breath of the Almighty which giveth them understanding.
Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
9 Not those rich in years must be always wise: neither do the aged constantly understand what is just.
Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
10 Therefore do I say, Hearken to me: I also will show forth what I know myself.
Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
11 Behold, I waited for your words: I gave an attentive ear to your reasonings, till you might have searched out the [proper] words.
Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
12 And now I understand you fully, and, behold, there is none that convinceth Job, or, that answereth his speeches among you.
Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
13 Say then not, We have found wisdom: God will thrust him down, not man.
Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
14 But he hath not directed any words against me: and with your speeches will I not answer him.
Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
15 They are dismayed, they answer no more: words have escaped away from them.
Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
16 And should I wait [longer], because they cannot speak, because they stand stilt and answer no more?
Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
17 [But] I also will surely answer my part, I myself also will show forth what I know;
La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
18 For I am full of words, the spirit in my bosom urgeth me hard.
Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
19 Behold, my bosom is like [fresh] wine which hath not been opened: like new bottles it is ready to burst.
Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
20 I will speak, that I may breathe freer: I will open my lips and answer.
Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
21 On no account will I show undue favor to any man, and to no son of earth will I give flattering titles.
Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
22 For I know not to give flattering titles; [for else] my Maker would speedily carry me away.
Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.

< Job 32 >