< Jeremiah 26 >

1 In the beginning of the reign of Jehoyakim the son of Josiah the king of Judah came this word from the Lord, saying,
Mwanzoni mwa utawala wake Yehoyakimu mwana wa Yosia, neno likaja kutoka kwa Yeremia, likisema,
2 Thus hath said the Lord, Place thyself in the court of the house of the Lord, and speak against all of the cities of Judah, who come to prostrate themselves in the house of the Lord, all the words that I have commanded thee to speak unto them: omit not a word [thereof];
“Yahwe anasema hivi: Simama katika uwanja wa nyumba yangu na sema kuhusu miji yote ya Yuda ambao huja kuabudu katika nyumba yangu. Tangaza maneno yote niliyokuamuru kuyasema kwao. Usipunguze neno lolote!
3 Perhaps it be that they will hearken, and return every man from his evil way, that I may bethink me of the evil, which I purpose to do unto them, because of the wrongfulness of their doings.
Labda watasikiliza, kwamba kila mtu ataziacha njia zake mbaya, ili nighairi majanga ninayokusudia kuyaleta juu yao kwa sababu ya uovu wa matendo yao.
4 And thou shalt say unto them, Thus hath said the Lord, if ye will not hearken unto me, to walk in my law, which I have set before you,
Kwa hiyo lazima useme kwao, 'Yahwe anasema hivi: Kama hamtanisikiliza ili mtembee katika sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu—
5 To hearken unto the words of my servants the prophets, whom I send unto you, yea, making them rise up early, and sending them, while ye have not hearkened:
kama hamsikilizi maneno ya watumishi wangu manabii ambao naendelea kuwatuma kwenu—lakini hamjasikiliza! —
6 Then will I render this house like Shiloh, and this city will I render a curse unto all the nations of the earth.
kisha nitaifanya nyumba hii kuwa kama Shilo; nitaifanya nyumba hii kuwa laana katika macho ya mataifa yote juu ya dunia.
7 And the priests and the prophets and all the people heard Jeremiah speaking these words in the house of the Lord:
Makuhani, manabii, na watu wote wakamsikia Yeremia akitangaza maneno haya katika nyumba ya Yahwe.
8 And it came to pass, when Jeremiah had finished speaking all that the Lord had commanded [him] to speak unto all the people, that the priests and the prophets and all the people seized on him, saying, Thou shalt surely die.
Kwa hiyo ikatokea kwamba Yeremia alipomaliza kutangaza aliyokuwa Yahwe alimwwamuru kuyasema kwa watu wote, makuhani, manabii, na watu wote wakamsimamisha na kusema, “Hakika utakufa!
9 Why hast thou prophesied in the name of the Lord, saying, Like Shiloh shall this house be, and this city shall be ruined, [left] without an inhabitant? And all the people assembled themselves against Jeremiah in the house of the Lord.
Kwa nini umetabiri katika jina la Yahwe na kusema kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa, pasipo wakaaji?” Kwa maana watu wote wameunda kundi dhidi ya nyumba ya Yeremia.
10 But when the princes of Judah heard these things, they came up from the king's house unto the house of the Lord, and sat down at the entrance of the new gate of the Lord's house.
Kisha wakuu wa Yuda wakasikia maneno haya na wakapanda kutoka nyumba ya mfalme kwenda kwenye nyumba ya Yahwe. Wakakaa katika njia ya lango katika Lango Jipya la nyumba ya Yahwe.
11 Then said the priests and the prophets unto the princes and unto all the people, as followeth, This man deserveth the punishment of death; for he hath prophesied against this city, as ye have heard with your own ears.
Makuhani na manabii wakasema kwa wakuu wa Yuda na kwa watu wote. Wakasema, “Ni haki kwa mtu huyu kufa, kwa maana ametabiri juu ya mji huu, kama mlivyosikia kwa masikio yenu!”
12 Then said Jeremiah unto all the princes and unto all the people, as followeth, The Lord hath sent me to prophesy against this house and against this city all the words that ye have heard.
Kwa hiyo Yeremia akasema kwa wakuu wote na watu wote, “Yeremia amenituma kutabiri juu ya nyumb hii na mji wake, kusema maneno yote ambayo mmeyasikia.
13 But now amend your ways and your doings, and hearken to the voice of the Lord your God: and the Lord will bethink him of the evil that he hath spoken against you.
Kwa hiyo sasa, imarisheni njia zenu na matendo yenu, na sikilizeni sauti ya Yahwe Mungu wenu kwamba ataghairi kuhusu janga ambalo ametangaza dhidi yenu.
14 As for me, behold, I am in your hand: do with me as seemeth good and just in your eyes.
Mimi mwenyewe—niangalieni! —niko mikononi mwenu. Nitendeeni yaliyo mema na sahihi katika macho yenu.
15 But know ye for certain, that if ye put me to death, ye will surely place [the guilt of] innocent blood upon yourselves, and upon this city, and upon its inhabitants; for in truth hath the Lord sent me unto you to speak in your ears all these words.
Lakini kwa hakika lazima mjue kwamba kama mtaniua mimi, basi mnaiweka damu isiyo na hatia juu yenu wenyewe na juu ya mji huu na wakaaji wake, kwa maana Yahwe amenituma kweli kwenu ili nitangaze maneno yote kwa ajili ya masikio yenu.”
16 Then said the princes and all the people unto the priests and to the prophets, This man is not deserving the punishment of death; for in the name of the Lord our God hath he spoken unto us.
Kisha wakuu na watu wote wakasema kwa makuhani na manabii, “Si vyema kwa mtu huyu kufa, kwa maana ametangaza mambo haya kwetu katika jina la Yahwe Mungu wetu.”
17 And then rose up certain men of the elders of the land, and said to all the assembly of the people, as followeth,
Kisha watu kutoka wazee wa nchi wakasimama na kusema kwa kusanyiko lote la watu.
18 Michah the Morashthite prophesied in the days of Hezekiah the king of Judah. and said to all the people of Judah, as followeth, Thus hath said the Lord of hosts, Zion shall be ploughed up like a field, and Jerusalem shall become heaps of ruins, and the mountain of the house, woody high-places.
Wakasema, “Mikaya Mmorashi alikuwa akitabiri katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda. Alinena kwa watu wote wa Yuda na kusema, 'Yahwe wa majeshi anasema hivi: Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalemu utakuwa lundo la magofu, na mlima wa hekalu utakuwa kilima kilichoota vichaka.' Hezekia mfalme wa Yuda na Yunda wote walimuua?
19 Did Hezekiah the king of Judah and all Judah attempt to put him to death? behold, he did fear the Lord, and besought the Lord, and the Lord bethought him of the evil which he had spoken against them. And shall we bring a great wickedness on our souls?
Hakumwogopa Yahwe na kuutaka radhi uso wa Yahwe ili kwamba Yahwe angeghairi kuhusu janga ambalo alilitangaza kwao? Kwa hiyo tutafanya maovu makubwa zaidi juu ya maisha yetu sisi wenyewe?”
20 And there was also a man that prophesied in the name of the Lord, Uriyah the son of Shema'yahu of Kiryath-ye'arim, who prophesied against this city and against this land in accordance with all the words of Jeremiah;
Wakati huo huo palikuwa na mtu mwingine ambaye alitabiri katika jina la Yahwe—Uria mwan wa Shemaya kutoka Kiriath Yearimu—pia alitabiri juu ya mji na nchi hii, akikubaliana na maneno yote ya Yeremia.
21 And when king Jehoyakim, with all his mighty men, and all the princes, heard his words, the king sought to put him to death; but when Uriyahu heard it, he was afraid, and fled, and arrived in Egypt;
Lakini Mfalme Yohoyakimu na wanajeshi wake wote na watumishi wake wote waliposikia maneno yake, kisha mfalme alijaribu kumuua, lakini Uria alisikia na kuogopa, kwa hiyo alikimbia na akaenda Misiri
22 But king Jehoyakim sent some men into Egypt, namely, Elnathan the son of 'Achbor, and some men with him into Egypt:
Kisha mfalme Yehoyakimu alituma watu kwenda Misiri—Elnathani mwana wa Achbori na watu kwenda Misiri kumfuata Uria.
23 And they fetched Uriyahu out of Egypt, and brought him unto king Jehoyakim, who slew him with the sword, and cast his dead body upon the graves of the common people.
Wakamtoa Uria nje kutoka Misiri na kumleta kwa Mfalme Yehoyakimu. Kisha Yehoyakimu akamuua kwa upanga na kumpeleka nje kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
24 But the hand of Achikam the son of Shaphan was with Jeremiah, so as not to give him up into the hand of the people to put him to death.
Lakini mkno wa Ahikamu mwana wa Shapni alikuwa pamoja na Yeremia, hivyo hakutiwa mikonono mwa watu ili auawe.

< Jeremiah 26 >