< Jeremiah 25 >

1 The word that came to Jeremiah concerning all the people of Judah, in the fourth year of Jehoyakim the son of Josiah the king of Judah, which is the first year of Nebuchadrezzar the king of Babylon;
Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
2 Which Jeremiah the prophet spoke concerning all the people of Judah, and to all the inhabitants of Jerusalem, saying,
Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
3 From the thirteenth year of Josiah the son of Amon the king of Judah, even until this day, that is now three and twenty years, the word of the Lord hath come unto me, and I have spoken unto you, rising early and speaking; but ye have not hearkened.
Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
4 And the Lord hath sent unto you all his servants the prophets, making [them] rise early and sending [them]; but ye have not hearkened, and have not inclined your ear to hear.
Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
5 They said, O do turn away every one from his evil way, and from the wrongfulness of your doings; and ye shall remain in the land that the Lord hath given unto you and to your fathers, for from eternity to eternity;
Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
6 And go not after other gods to serve them, and to bow down to them, and provoke me not to anger with the works of your hands; and I will not injure you.
Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
7 Yet have ye not hearkened unto me, saith the Lord: in order that ye might provoke me to anger with the works of your own hands to your own injury.
“Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
8 Therefore thus hath said the Lord of hosts, Because ye have not hearkened to my words:
Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
9 Behold, I will send and take all the families of the north, saith the Lord, and to Nebuchadrezzar the king of Babylon, my servant, and I will bring them over this land, and over its inhabitants, and over all these nations round about, and I will utterly destroy them, and make them an astonishment, and a derision, and perpetual ruins.
nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
10 And I will banish from them the voice of gladness, and the voice of joy, the voice of the bridegroom, and the voice of the bride, the sound of the mill, and the light of the lamp.
Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
11 And this whole land shall become a ruin and an [object of] astonishment; and these nations shall serve the king of Babylon seventy years.
Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
12 And it shall come to pass, when seventy years are completed, that I will visit on the king of Babylon, and on that nation, saith the Lord, their iniquity, and on the land of the Chaldeans, and will change it into perpetual desolations.
“Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
13 And I will bring over that land all my words which I have spoken concerning it, all that is written in this book, which Jeremiah hath prophesied concerning all the nations.
Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
14 For when many nations and great kings shall have made them also serve: I will then recompense them according to their deeds, and according to the work of their own hands.
Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
15 For thus hath said the Lord the God of Israel unto me, Take the cup of the wine of this fury out of my hand, and cause all the nations to whom I send thee to drink it.
Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
16 And they shall drink, and reel about, and be mad, because of the sword that I will send among them.
Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
17 And I took the cup out of the hand of the Lord, and caused to drink all the nations, unto whom the Lord had sent me:
Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
18 Jerusalem, and the cities of Judah, and its kings, and its princes, to make them a ruin, an astonishment, a derision, and a curse; as it is this day;
Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
19 Pharaoh the king of Egypt, and his servants, and his princes, and all his people;
pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
20 And all the confederated nations, and all the kings of the land of 'Uz, and all the kings of the land of the Philistines, and Ashkelon, and Gazzah, and 'Ekron, and the remnant of Ashdod;
pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
21 Edom, and Moab, and the children of 'Ammon;
Edomu, Moabu na Amoni;
22 And all the kings of Tyre, and all the kings of Zidon, and the kings of the isle which is beyond the sea;
wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
23 Dedan, and Thema, and Buz, and all those that have their hair cut round;
Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
24 And all the kings of Arabia, and all the kings of the confederated nations that dwell in the wilderness;
wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
25 And all the kings of Zimri, and all the kings of 'Elam, and all the kings of Media;
wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
26 And all the kings of the north, that are far and that are near, one with another, and all the kingdoms of the world, which are upon the face of the earth; and the king of Sheshach shall drink after them.
na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
27 And thou shalt say unto them, Thus hath said the Lord of hosts, the God of Israel, Drink ye, and become drunken, and vomit, and fall, and rise no more, because of the sword, which I am sending among you.
“Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
28 And it shall be, if they refuse to take the cup of thy hand to drink, that thou shalt say unto them, Thus hath said the Lord of hosts, Ye must certainly drink;
Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
29 For lo, on the city which is called by my name, I begin to inflict evil, and ye will remain utterly unpunished? Ye shall not remain unpunished; for a sword am I calling up over all the inhabitants of the earth, saith the Lord of hosts.
Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
30 But thou, do thou prophesy concerning them all these words, and say unto them, The Lord will cry aloud from on high, and from his holy habitation will he send forth his voice; he will cry out very loudly over his habitation; the vintner's call, as they that tread out the grapes, will he lift up against all the inhabitants of the earth.
“Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
31 A tumultuous noise cometh even to the ends of the earth; for the Lord hath a controversy with the nations, he holdeth judgment over all flesh: the wicked, —these he giveth up to the sword, saith the Lord.
Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
32 Thus hath said the Lord of hosts, Behold, evil goeth forth from nation to nation, and a great storm-wind waketh up from the farthest ends of the earth.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
33 And the slain of the Lord shall be on that day from one end of the earth even unto the other end of the earth: they shall not be lamented, nor gathered up, nor buried; they shall be as dung upon the surface of the ground.
Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
34 Wail, ye shepherds, and cry; and roll yourselves about [in the dust], ye leaders of the flocks; for full are your days for you to be slaughtered, and I will scatter you; and you shall fall like a costly vessel.
Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
35 And lost shall be the place of refuge for the shepherds, and the escape for the leaders of the flocks to escape.
Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
36 There is the voice of the cry of anguish of the shepherds, and the wailing of the leaders of the flocks; for the Lord hath devastated their pasture.
Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
37 And in silent desolation lie the pasture-lands of peace, because of the fierceness of the anger of the Lord.
Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
38 He hath forsaken his covert, like the young lion; for their land is become desolate, because of the fierceness of the wasting [sword], and because of the fierceness of his anger.
Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.

< Jeremiah 25 >