< Jeremiah 23 >
1 Woe unto the shepherds that destroy and scatter the flocks of my pasture! saith the Lord.
“Ole wao wachungaji ambao huangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu-hii ndiyo ahadi ya Bwana.”
2 Therefore thus hath said the Lord the God of Israel concerning the shepherds that feed my people, Ye have scattered my flocks, and driven them away, and have not taken care of them: now, behold, I will visit upon you the evil of your doings, saith the Lord.
Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi juu ya wachungaji ambao wanawachunga watu wake, “Ninyi mnawatawanya kundi langu na kuwafukuza. Hamuwajali hata kidogo. Tambueni hili! Mimi nitawalipiza uovu wa matendo yenu-hili ni tamko la Bwana.
3 And I will indeed gather the remnant of my flock together out of all the countries whither I have driven them; and I will bring them back again to their folds: and they shall be fruitful and multiply.
Mimi mwenyewe nitakusanya mabaki ya kondoo wangu kutoka nchi zote nilizowafukuza, nami nitawarejesha kwenye eneo la malisho, ambako watazaa na kuongezeka.
4 And I will raise up over them shepherds who shall feed them: and they shall fear no more, nor be dismayed, and none of them shall be missing, saith the Lord.
Ndipo nitawainua wachungaji juu yao ambao watawachunga hivyo hawataogopa tena au kupotezwa. Hakuna hata mmoja atakayepotea-hili ni tamko la Bwana.
5 Behold, days are coming, saith the Lord, when I will raise up unto David a righteous sprout, and he shall reign as king, and prosper, and he shall execute justice and righteousness on the earth.
Angalia, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-nitakapomuinulia Daudi tawi la haki. Atatawala kama mfalme; atatenda kwa busara na kusababisha hukumu na haki katika nchi.
6 In his days shall Judah be helped, and Israel shall dwell in safety: and this is his name whereby he shall be called, The Lord is our righteousness.
Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli wataishi kwa usalama. Na jina lake atakayeitwa Bwana ni haki yetu.
7 Therefore, behold, days are coming, saith the Lord, when they shall no more say, As the Lord liveth, who hath brought up the children of Israel out of the land of Egypt;
Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-hawatasema tena, 'Kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya Misri.'
8 But, As the Lord liveth, who hath brought up and who hath led forth the seed of the house of Israel out of the north country, and out of all countries whither I had driven them: and they shall dwell in their own land.
Badala yake watasema, 'Kama Bwana aishivyo, ambaye aliwaleta na ambaye aliwaongoza wana wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote walizofukuzwa.' Nao watakaa katika nchi yao wenyewe.”
9 To the prophets—Broken is my heart within me; all my bones shake; I am like a drunken man, and like a person whom wine hath overcome, because of the Lord, and because of his holy words.
Kuhusu manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu, na mifupa yangu yote imetetemeka. Nimekuwa kama mlevi, kama mtu ambaye ameshindwa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
10 For of adulterers is the land full; for because of false swearing mourneth the land, dried up are the pastures in the wilderness; because their course was for evil, and their strength was for injustice.
Kwa maana nchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya hayo nchi imeuka. Milima katika jangwa imekauka. Njia hizi za manabii ni mbaya; nguvu zao hazitumiwi kwa namna sahihi.
11 For both prophet and priest are hypocrites: yea, in my own house have I found their wickedness, saith the Lord.
Kwa maana manabii na makuhani wote wamekufuru. Nimeona uovu wao ndani ya nyumba yangu! - hili ndilo tamko la Bwana;
12 Therefore shall their way be unto them as slippery ways in the darkness; they shall be pushed forward, and fall thereon; for I will bring upon them evil, the year of their punishment, saith the Lord.
kwa hiyo njia yao itakuwa kama mahali pa kupumzika katika giza. Watasukumwa chini. Wao wataanguka ndani yake. Kwa maana nitawatuma mabaya juu yao katika mwaka wa adhabu yao; hili ndilo tamko la Bwana.
13 And on the prophets of Samaria have I seen absurdity: they prophesied by Ba'al, and misled my people Israel.
kwa maana nimeona uchungu kati ya manabii huko Samaria. Walitabiri kwa Baali na wakawaongoza watu wangu Israeli kwenye njia sahihi.
14 But on the prophets of Jerusalem have I seen a horrible thing; they commit adultery, and walk in falsehood; and they strengthen the hands of evil-doers, so that not one of these doth return from his wickedness: they are become unto me all of them as Sodom, and its inhabitants as Gomorrah.
Na miongoni mwa manabii huko Yerusalemu nimeona mambo ya kutisha: wanafanya uzinzi na huenda kwa udanganyifu. Wanaimarisha mikono ya waovu; hakuna mtu anarejea na kuacha uovu wake. Wote wamekuwa kama Sodoma kwangu na wenyeji wake kama Gomora!”
15 Therefore thus hath said the Lord of hosts concerning the prophets, Behold, I will feed them with wormwood, and make them drink poison-water; for from the prophets of Jerusalem is hypocrisy gone forth over all the land.
Kwa hiyo, Bwana wa majeshi asema hivi juu ya manabii, “Tazameni, nitawafanya wale magugu na kunywa maji yenye sumu, kwa maana kufuru imetoka kwa manabii wa Yerusalemu na kuingia katika nchi yote.”
16 Thus hath said the Lord of hosts, Hearken not unto the words of the prophets that prophesy unto you, they bring you unto vanity: a vision of their own heart do they ever speak, not out of the mouth of the Lord.
Bwana wa majeshi asema hivi, “Usisikilize maneno ya manabii wanaokuhubiri. Wamekudanganya! Wanatangaza maono kutoka kwenye mawazo yao wenyewe, si kwa kinywa cha Bwana.
17 They say indeed unto those that incense me, The Lord hath spoken, Peace shall ye have; and unto every one that walketh in the stubbornness of his own heart, they said, There shall come no evil upon you.
Wanasema daima kwa wale wanaonidharau mimi, 'Bwana asema kutakuwa na amani kwako.' Na kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake anasema, 'mabaya hayatakuja kwenu.'
18 For who hath stood in the secret counsel of the Lord, that he could perceive and hear his word? who hath listened to his word and heard it?
Lakini nani amesimama katika mkutano wa baraza la Bwana? Ni nani anayeona na kusikia neno lake? Ni nani anayezingatia maneno yake na kusikiliza?
19 Behold, the storm-wind of the Lord is gone forth in fury, yea, a whirling storm: upon the head of the wicked shall it fall grievously.
Tazama, kuna dhoruba inayotoka kwa Bwana! Hasira yake inatoka, na dhoruba inazunguka. Inazunguka vichwa vya waovu.
20 The anger of the Lord will not return, until he have executed, and until he have fulfilled the purposes of his heart: in the end of days shall ye understand this fully.
Hasira za Bwana hazitarejea mpaka zitakapotimiza nia ya moyo wake. Katika siku za mwisho, utaelewa.
21 I had not sent these prophets, yet they ran: I had not spoken to them, yet they prophesied.
Sikuwatuma manabii hawa. Wao tu walionekana. Sikuwahubiri jambo lolote kwao, lakini bado wanatabiri.
22 But if they had stood in my secret counsel, they should have announced my words to my people, and have caused them to turn back from their evil way, and from the wrongfulness of their doings.
Kwa kuwa kama walisimama katika mkutano wangu wa baraza, wangeweza kuwasababisha watu wangu kusikia neno langu; wangewafanya wapate kuacha maneno yao mabaya na mazoea mabaya.
23 Am I a God for those near at hand, saith the Lord, and not a God for those who are afar off?
Mimi ni Mungu aliye karibu-hili ni tamko la Bwana-mimi sio Mungu aliye mbali?
24 If a man should hide himself in secret places should I not then see him? saith the Lord. Do I not fill the heavens and the earth? saith the Lord.
Je, kuna mtu yeyote anayejificha mahali penye siri ili nisiweze kumwona? -Hili ndilo tamko la Bwana-Je mbingu na nchi hazikujawa nami? -hili Ndilo tamko la Bwana.
25 I have heard what the prophets have said, that prophesy falsely in my name, saying, I have dreamt, I have dreamt.
Nimesikia yale waliyosema manabii, wale waliokuwa wanatabiri uongo kwa jina langu. Wakisema, 'Nilikuwa na ndoto!
26 How long shall it be in the heart of the prophets that prophesy falsehood? yea, the prophets of the deceit of their own heart, —
Nilikuwa na ndoto!' Je, hii itaendelea mpaka lini, manabii wanaotabiri uongo kutoka kwa akili zao, na wanasema nini kutokana na udanganyifu mioyoni mwao?
27 [How long] do they think to cause my people to forget my name by their dreams which they relate every man to his neighbor, as their fathers forgot my name for the sake of Ba'al?
Wana mpango wa kuwafanya watu wangu kusahau jina langu kwa ndoto ambazo wanazoripoti, kila mmoja kwa jirani yake, kama vile babu zao walivyosahau jina langu kwa ajili ya jina la Baali.
28 The prophet that hath had a dream, let him relate his dream; and he that hath received my word, let him speak my word of truth. What hath the straw to do with the corn? saith the Lord.
Nabii aliye na ndoto, aseme ndoto hiyo. Lakini yule ambaye nimemwambia kitu fulani, basi aseme neno langu kwa kweli. Je, majani yanahusiana na nafaka? - hili ni tamko la Bwana-
29 Is not thus my word, like the fire? saith the Lord, and like a hammer that shivereth the rock?
Na neno langu si kama moto? -Hili ni tamko la Bwana-na kama mwamba wenye kupiga nyundo?
30 Therefore, behold, I am against the prophets, saith the Lord, that steal my words every one from his neighbor.
Tazameni, ninapingana na nabii-hii ndiyo ahadi ya Bwana-yeyote anayeiba maneno kutoka kwa mtu mwingine na anasema yanatoka kwangu.
31 Behold, I am against the prophets, saith the Lord, that use their own word, and say, [The Lord] saith.
Tazama, ninapingana na manabii-hili ndilo tamko la Bwana-ambao hutumia lugha zao kutabiri maneno.
32 Behold, I am against those that prophesy with false dreams, saith the Lord, and do relate them, and mislead my people by their falsehoods, and by their vain boasting: while I have not sent them, nor commanded them; and they cannot bring the least profit to this people, saith the Lord.
Tazameni, ninapingana na manabii wanaoota ndoto-hii ndiyo ahadi ya Bwana-na kisha kuwahubiri na kwa njia hii kuwadanganya watu wangu kwa udanganyifu wao na kujivunia. Mimi ni juu yao, kwa kuwa sikuwatuma wala kuwapa amri. Kwa hivyo hawatawasaidia watu hawa - hili ndilo tamko la Bwana.
33 And if this people, or the prophet, or a priest, should ask thee, saying, What is the message of the Lord? then shalt thou say unto them, Because of this “What is the message?” will I even cast you off, saith the Lord.
Watu hawa au nabii au kuhani wakakuuliza, 'Je, ni nini tamko la Bwana?' basi lazima uwaambie, 'Ni tamko gani? Kwa maana nimekuacha wewe-hili ndilo tamko la Bwana.
34 And as for the prophet, and the priest, and the people, that will say, “A message of the Lord,” I will even inflict punishment on that man and on his house.
Kwa habari ya manabii, makuhani, na watu wanaosema, 'Hili ndilo tamko la Bwana,' nitamuadhibu mtu huyo na nyumba yake.
35 Thus shall ye say every one to his neighbor, and every one to his brother, What hath the Lord answered? and, What hath the Lord spoken?
Endelea kusema, kila mtu kwa jirani yake na kila mtu kwa ndugu yake, 'Bwana alijibu nini?' na 'Bwana alitangaza nini?'
36 But “A message of the Lord” shall ye not mention any more; for the message cometh indeed to the man of his [prophetic] word; but ye pervert the words of the living God, of the Lord of hosts our God.
Lakini usizungumze tena juu ya tamko la Bwana, kwa kuwa kila tamko kutoka kwa kila mtu limekuwa ujumbe wake mwenyewe, na umepotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana wa majeshi, Mungu wetu.
37 Thus shalt thou say to the prophet, What hath the Lord answered thee? and, What hath the Lord spoken?
Utamuuliza nabii hivi, 'Bwana alikujibu nini? Je, Bwana alisema nini? Kisha unasema tamko kutoka kwa Bwana;
38 But if ye will say, “A message of the Lord,” then thus saith the Lord, Because ye say this word, “A message of the Lord,” and I have sent unto you, saying, Ye shall not say, “A message of the Lord:”
lakini Bwana asema hivi, Sema hivi, “Hili ni tamko la Bwana” ingawa nimekuagiza na kusema, “Usiseme: Hili ni tamko kutoka kwa Bwana.”
39 Therefore, behold, I am here, and I will tear you completely away, and I will cast you off, and the city that I have given to you and to your fathers, out of my presence;
Kwa hiyo, angalia, nitawachukua na kukutupa mbali na mimi, pamoja na jiji ambalo nilikupa wewe na baba zako.
40 And I will lay upon you an everlasting disgrace, and a perpetual shame, which shall not be forgotten.
Ndipo nitaweka aibu ya milele na fedheha juu yenu ambayo haitasahauliwa.'”