< Isaiah 49 >

1 Hearken, O isles, unto me; and listen, ye people, from afar: The Lord hath called me from my birth; from my mother's womb hath he made mention of my name.
Nisikilize mimi, enyi mkao pwani! na kuwa makini, enyi watu mkao mbali. Yahwe amenita mimi kutoka kuzaliwa kwa jina, mama yangu aliponileta duniani.
2 And he hath rendered my mouth like a sharp sword; in the shadow of his hand hath he hidden me: and he hath rendered me as a polished arrow; in his quiver hath he concealed me;
Amefanya mdomo wangu kuwa kama upanga mkali; amenificha mimi katika kivuli cha mkono wake; amenifanya mimi kuwa mshale unaong'aa; katika podo yake amenificha mimi.
3 And said unto me, My servant art thou, O Israel, thou on whom I will be glorified.
Amesema na mimi, ''Wewe ni mtumishi wangu, Israeli, kupitia yeye nitaonyesha utukufu wangu.''
4 But I had indeed said, For no purpose have I labored, for naught and vanity have I spent my strength; yet surely my cause is with the Lord, and the recompense of my work with my God.
Lakini nilimjibu, ''Japo nilifikiria nilifanya kazi bure, nimetumia nguvu zangu bure, ikiwa haki yangu iko pamoja na Yahwe, na zawadi yangu iko kwa Mungu wangu.
5 And now hath said the Lord that formed me from the womb to be his servant, to bring Jacob again to him, that Israel may be gathered unto him, that I should be honored in the eyes of the Lord, while my God was my strength, —
Na sasa Yahwe asema hivi, yeye aliyeniumba mimi toka kuzaliwa na kuwa mtumishi wake, kumrejesha Yakobo tena kwake mwenyewe, na Israeli wakusanyike kwake. Mimi ninaheshimika katika macho ya Yahwe, na Mungu wangu amekuwa nguvu zangu.
6 And he said, It is too light a thing that thou shouldst be my servant to raise up the tribes of Jacob, and to bring back the preserved of Israel! but I will [also] appoint thee for a light to the nations, that my salvation may reach as far as the end of the earth.
Asema hivi, ''Ni kitu kidogo sana kwa wewe kuwa mtumishi wangu ili kuanzisha ukoo wa Yakobo, na kuwarejesha wanaoishi Israeli. Nitakufanya wewe kuwa mwanga kwa Wayunani, ili uwe wokovu wangu katika mipaka ya nchi.
7 Thus hath said the Lord, the Redeemer of Israel, his Holy One, to him who is despised by men, to him who is abhorred by nations, to the servant of rulers, Kings shall see it and rise up, princes, and they shall prostrate themselves, for the sake of the Lord, who is faithful, the Holy One of Israel, who hath made choice of thee.
Yahwe asema hivi, Mkombozi wa Israeli, Mtatakatifu wao, kwa yeye ambae maisha yake yamedharauliwa, kuchukiwa na mataifa, na mtumwa wa viongozi, ''Mfalme atakuona wewe na nyanyuka, na wakuu watakuona wewe na inama chini, kwa sababu ya Yahwe ambae ni mwaminifu, hata mtakatifu wa Israeli, aliyewachagua ninyi.''
8 Thus hath said the Lord, In the time of favor have I answered thee, and on the day of salvation have I helped thee; and I will preserve thee, and I will appoint thee as a people of my covenant to raise up the land, to divide out desolate heritages;
Yahwe asema hivi, ''Kwa mda huu nimeamua kuwaonyesha neema yangu na nitawajibu ninyi, na siku ya wokovu nitawasaidi ninyi; Nitakulinda wewe; na nitawapa kama agano kwa watu, kuitengeneza tena nchi, kuwarihtisha urithi uliokuwa na ukiwa.
9 When I say to the prisoners, Go forth; to those that are in darkness, Show yourselves. On the roads shall they feed, and on all mountain-peaks shall be their pasture.
Utasema kwa wafungwa, 'Tokeni nje; kwa wale mlio katika giza gerezani, 'Jionyeshe mwenyewe. 'Watachunga pembeni ya barabara, na juu ya miteremko ya wazi yatakuwa malisho yake.
10 They shall not be hungry nor thirsty, and neither heat nor sun shall smite them; for he that hath mercy on them will lead them, and by springs of water will he guide them.
Hawatasikia njaa wala kiu; wala joto au jua halitawaunguza, kwa yeye mwenye huruma juu yao atawaongoza wao; atawaongoza wao kwenye mikondo ya maji.
11 And I will change all my mountains into a road, and my highways shall be lifted up.
Na nitafanya milima yote kuwa barabara, na kufanya njia za juu kuwa sawa''
12 Behold, these shall come from afar; and, lo, these from the north and from the west; and these from the land of Sinim.
Tazama, haya yatatoka kutoka mbali, baadhi kutoka kaskazini na magharibi; na wengine kutoka nchi ya Sinimi.
13 Sing, O heavens; and be joyful, O earth; and break forth, O mountains, into song; for the Lord hath comforted his people, and upon his oppressed will he have mercy.
Imba, ewe mbingu, na uwe na furaha, ewe nchi pazeni sauti ya kuimmba enyi milima! maana Yahwe anawafariji watu wake, na watakuwa na huruma kwa wale wanoteseka.
14 Yet Zion said, the Eternal hath forsaken me, and the Lord hath forgotten me.
Lakin Sayuni asema, Yahwe ameniacha mimi, na Bwana amenisahau mimi.''
15 Can a woman forget her sucking child, not to have mercy on the son of her body? yea, should these even forget, yet would I not forget thee.
''Je mwanamke anaweza kumsahau mtoto wake, aliyemnyonyesha, hivyo hana huruma na mtoto aliye mzaa? ndio, hawakusahau, lakini siwezi kukusahau wewe.
16 Behold, upon the palms of my hands have I engraved thee; thy walls are continually before me.
Tazama, nimeliandika jina lako kwenye kiganja cha mkono wangu; Kuta zako zinaendelea kuwa mbele yangu.
17 Thy children come in haste; thy destroyers and they that laid thee waste shall go away from thee.
Watoto wangu wamerudi haraka, wakati wale wanowaangaimiza nyie wameenda mbali.
18 Lift up thy eyes round about, and see; they all are assembled together, they come to thee: as I live, saith the Lord, thou shalt surely clothe thyself with them all, as with an ornament, and bind them on thee, as a bride.
Tazama karibu na uone, wote wamekusanyika na wanakuja kwako. Nitahakikisha kama ninaishi- hili ni tamko la Yahwe- hakika mtavivaaa kama kama kijiti; utajifungia kama bibi harusi.
19 For thy ruins and thy desolate places, and thy wasted land, —yea, now shall it be too narrow for thee by reason of the inhabitants, and thy destroyers shall be far away.
Japo umeharibiwa na kuwa na ukiwa, nchi iliyoharibiwa, sasa itakuwa ndogo sana kwa wenyeji, na wale wanao waliokumeza watakuwa mbali,
20 Yet again will say before thy ears the children of whom thou wast deprived, The place is too narrow for me; make room for me that I may dwell.
Watoto watakaozaliwa katika kipindi cha msiba watasema mkiwa mnawasikiliza, 'Sehemu hii ni duni kwetu, tengeneza chumba kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi hapa.
21 And thou wilt say in thy heart, Who hath born me these, seeing I was bereft of my children, and was solitary, an exile, and outcast? and who hath brought up these? Behold, I was left entirely alone; these, where have they been?
Halafu utajiuliza mwenyewe, ni nani aliyewazaa watu hawa kwangu? Mimi nilifiwa na ni tasa, niliyefungwa na kupewa talaka. Ni nani aliyewalea hawa watoto? Tazama, niliachiwa yote mimi mwenyewe; Je haya yametoka wapi?''
22 Thus hath said the Lord Eternal, Behold, I will lift up to the nations my hand, and to the people will I raise up high my standard; and they shall bring thy sons in [their] arms, and thy daughters shall be carried upon shoulders.
Yahwe asema hivi, ''Tazama, nitanyanyua mkono wangu juu ya mataifa; Nitanyanyua bendera yangu ya ishara kwa watu. Watawaleta watoto wako kwenye mikono yao na watawabeba binti zako juu ya mabega yao.
23 And kings shall be thy nursing-fathers, and their princesses thy nursing-mothers; with the face toward the earth shall they bow down to thee, and the dust of thy feet shall they lick up: and thou shalt know that I am the Lord, who will not suffer those who hope in me to be ashamed.
Wafalme watakuwa baba zako wa kambo, na malikia watakuwa wafanyakazi wa ndani; watakuinamia chini wewe kw uso wao kwa nchi na kukung'uta mavumbi ya miguu yenu; wale wanonisubiri mimi hawataabika.''
24 Shall the prey be taken from the mighty, or shall the captive of the victor escape?
Je mateka wanaweza kuchukuliwa kwa shujaa, au wafungwa kukombolewa kutoka kwa mkali?
25 For thus hath said the Lord, Also the captive of the mighty shall be taken away, and the prey of the powerful shall escape; and with those who contend against thee will I contend, and thy children will I indeed save.
Lakini Yahwe asema hivi, ''Wafungwa watachukuliwa kutoka kwa shujaa, na maeteka watakombolewa; maana utampinga adui yako na kuwakomboa watoto wako.
26 And I will feed thy oppressors with their own flesh; and as with new wine shall they be made drunken with their own blood: and all flesh shall know that I the Eternal am thy Saviour, and thy Redeemer the Mighty One of Jacob.
Na nitawalisha wanowaonea kwa mwili wao wenyewe; na watalewa kwa damu zao wenyewe, kama iliyo mvinyo; na watu wote watajua kwamba Mimi Yahwe, ni Mokozi wenu na Mkombozi wenu, yeye aliyemkuu wa Isareli.

< Isaiah 49 >