< Hosea 11 >
1 When Israel was yet young, then I loved him, and out of Egypt did I call my son.
“Wakati Israeli alikuwa kijana nilimpenda, na nikamwita mtoto wangu kutoka Misri.
2 The [prophets] called them; but the more they went from them: unto the Be'alim would they sacrifice, and to the graven images would they burn incense.
Kwa kadiri waliyoitwa, ndivyo walivyoondoka kwangu. Wakawafanyia dhabihu Baali, wakatafuta uvumba kwa sanamu.
3 Yet I myself appointed a leader for Ephraim, who took them up in his arms; but they would not acknowledge that I healed them.
Lakini mimi ndio niliyemfundisha Efraimu kutembea. Ndiye niliyewainua kwa silaha zao, lakini hawakujua kwamba niliwajali.
4 With human cords I ever drew them forward, with leading-strings of love: and I was to them as those that lift off the yoke from their jaws, and I held out unto them food.
Niliwaongoza kwa kamba za ubinadamu, na mafungo ya upendo. Mimi nilikuwa kama mtu aliyepunguza jozi juu ya taya zao, na nikainama na kuwalisha.
5 He should not return unto the land of Egypt: yet [now] is the Assyrian his king; because they refused to repent.
Je, hawatarudi nchi ya Misri? Je, Ashuru haitatawala juu yao kwa sababu wanakataa kurudi kwangu?
6 And the sword shall fall on his cities, and shall make an end of his boughs, and consume them, because of their [evil] counsels.
Upanga utaanguka juu ya miji yao na kuharibu makomeo ya milango yao; itawaangamiza kwa sababu ya mipango yao wenyewe.
7 For my people are only bent on backsliding from me; and though upward they call them, they altogether will not elevate themselves.
Watu wangu wameamua kuniacha. Ingawa wanaita kwa Aliye Juu, hakuna mtu atawasaidia.
8 How shall I give thee up, Ephraim? how shall I surrender thee, Israel? how shall I make thee as Admah? how shall I change thee as Zeboyim? turned is my heart within me, all my compassion is enkindled together.
Ninawezaje kukuacha, Efraimu? Ninawezaje kukupeleka, Israeli? Ninawezaje kukufanya kama Adma? Ninawezaje kukufanya kama Seboimu? Moyo wangu umebadilika ndani yangu; huruma zangu zote zimeongezeka.
9 I will not execute the fierceness of my anger, I will not again destroy Ephraim; for God am I, and not man, the Holy One in the midst of thee, and I will not come with an enemy's hatred.
Sitafanya hasira yangu kali; Mimi sitawaangamiza Efraimu tena. Kwa maana mimi ni Mungu, wala si mtu; Mimi ni Mtakatifu kati yenu, nami sitakuja katika ghadhabu.
10 They shall follow after the Lord, when he will roar like a lion; for he will roar, and the children shall hasten together from the west;
Watanifuata, Bwana. Nitanguruma kama simba. Nami nitaomboleza, na watu watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.
11 They shall hasten together as birds out of Egypt, and as doves out of the land of Assyria: and I will cause them to dwell in their houses, saith the Lord.
Watakuja wakitetemeka kama ndege kutoka Misri, kama njiwa kutoka nchi ya Ashuru. Nitawafanya wapate kuishi katika nyumba zao.” Hii ndiyo tamko la Bwana.
12 With lies hath Ephraim encompassed me about, and with deceit, the house of Israel; but Judah yet ruleth with God, and is faithful to the Holy One.
Efraimu ananizunguka kwa maneno ya uongo, na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Lakini Yuda bado anaendelea nami, Mungu, na ni mwaminifu kwangu, Mtakatifu.