< Genesis 44 >
1 And he commanded the superintendent of his house, saying, Fill the sacks of these men with food, as much as they can carry, and put every man's money in the mouth of his sack.
Yusufu akamwamru msimamizi wa nyumba yake, akisema, “Jaza magunia ya watu hawa kwa chakula, kiasi wawezacho kubeba, na uweke pesa ya kila mtu katika mdomo wa gunia lake.
2 And my cup, the silver cup, thou shalt put in the mouth of the sack of the youngest, and the money for his corn. And he did according to the word of Joseph which he had spoken.
Uweke kikombe changu, cha fedha, katika mdomo wa gunia la mdogo, na pesa yake ya chakula pia.” Msimamizi akafanya kama Yusufu alivyosema.
3 As soon as the morning was light, the men were sent away, they and their asses.
Kukapambazuka asubuhi, na wale watu wakaruhusiwa kuondoka, wao na punda zao.
4 They were gone out of the city, not yet far off, when Joseph said unto the superintendent of his house, Up, follow after the men; and when thou hast overtaken them, say unto them, Wherefore have ye returned evil for good?
Walipokuwa wametoka mjini lakini hawajafika mbali, Yusufu akamwambia msimamizi wa nyumba yake, “Inuka, uwafuatie wale watu, na utakapowapata, wambie, 'Kwa nini mmelipa uovu badala ya mema?
5 Is not this out of which my lord drinketh, and whereby indeed he divineth? ye have done evil in so doing.
Je hiki siyo kikombe ambacho bwana wangu hukinywea, na kikombe akitumiacho kwa uaguzi? Mmefanya vibaya, kwa jambo hili mlilolifanya.”
6 And he overtook them, and he spoke unto them these same words.
Msimamizi wa nyumba akawapata na kuwambia maneno haya.
7 And they said unto him, Wherefore will my lord speak such words as these? God forbid that thy servants should do any thing like this.
Wakasema, “Kwa nini bwana wetu anasema maneno kama haya? Na iwe mbali na watumishi wako kwamba wanaweza kufanya jambo hili.
8 Behold the money, which we found in the mouth of our sacks, we brought back unto thee out of the land of Canaan: how then should we steal out of thy lord's house silver or gold?
Tazama, pesa tulizozikuta katika midomo ya magunia yetu, tulizileta kwako kutoka katika nchi ya Kanaani. Ni kwa jinsi gani basi tunaweza kuiba katika nyumba ya bwana wako fedha au dhahabu?
9 With whomsoever of thy servants it be found, let him die; and we also will be bondmen unto thy lord.
Yeyote kitakayeonekana kwake miongoni mwa watumishi wako, atakufa, nasi sote tutakuwa watumwa wa bwana wangu.”
10 And he said, Now also let it be according to your words: he with whom it is found shall be my servant; but ye shall be blameless.
Msimamizi akasema, “Basi na iwe kwa kadili ya maneno yenu. Yeye ambaye kikombe kitaonekana kwake atakuwa mtumwa wangu, nanyi wengine mtakuwa bila hatia.”
11 And they made haste, and every one of them took down his sack to the ground, and every one opened his sack.
Kisha kila mtu akaharakisha na kulishusha gunia lake chini. na kila mtu akalifungua gunia lake.
12 And he searched, at the eldest he began, and at the youngest he left off; and the cup was found in Benjamin's sack.
Msimamizi akatafuta. akaanza na mkubwa wa wote na kumaliza kwa mdogo wa wote, na kikombe kikaonekana katika gunia la Benjamini.
13 Then they rent their clothes, and every one loaded his ass, and they returned to the city.
Wakararua mavazi yao. Kila mtu akapakia juu ya punda wake nao wakarudi mjini.
14 And Judah and his brothers came into Joseph's house, and he was yet there; and they fell down before him on the ground.
Yuda na ndugu zake wakaja katika nyumba ya Yusufu. Bado alikuwepo pale, nao wakainama mbele zake hata chini.
15 And Joseph said unto them, What deed is this that ye have done? knew ye not that such a man as I can certainly divine?
Yusufu akawambia, “Je ni nini hili mlilolifanya? Je hamjui kwamba mtu kama mimi anafanya uaguzi.
16 And Judah said, What shall we say unto my lord? what shall we speak? or how shall we justify ourselves? God hath found out the iniquity of thy servants: behold we are servants unto my lord, both we, as also he in whose hand the cup was found.
Yuda akasema, “Je tunaweza kumwambia nini bwana wangu? Tuseme nini? au ni jinsi gani twaweza kujithibitisha wenyewe? Mungu ameona uovu wa watumishi wako. Tazama, sisi ni watumwa wa bwana wangu, wote sisi na yule ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake.”
17 And he said, God forbid that I should do this: the man in whose hand the cup was found, he shall be my servant; and as for you, go you up in peace unto your father.
Yusufu akasema, “Na iwe mbali nami kwamba naweza kufanya hivyo. Mtu ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake, huyu ndiye atakuwa mtumwa wangu, lakini ninyi wengine, nendeni kwa amani kwa baba yenu.”
18 Then Judah came near unto him, and said, Pardon, my lord, let thy servant, I pray thee, speak a word in my lord's ears, and let not thy anger burn against thy servant; for thou art even as Pharaoh.
Ndipo Yuda alipomkaribia na kusema, “Bwana wangu, tafadhari mwache mtumishi wako aseme neno katika masikio ya bwana wangu, na usiziache hasira zako kuwaka dhidi ya mtumishi wako, kwani wewe ni kama Farao.
19 My lord asked his servants, saying, Have ye a father, or a brother.
Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, kusema, Je mnaye baba au ndugu?'
20 And we said unto my lord, We have an old father, and a little child born in his old age; and his brother is dead, and he alone is left of his mother, and his father loveth him.
Nasi tukamwambia bwana wangu, 'Tunaye baba, ni mzee, na mwana wa uzee wake, ni mdogo. Na ndugu yake alishakufa, na yeye peke yake ndiye amebaki kwa mama yake, na baba yake anampenda.'
21 And thou saidst unto thy servants, Bring him down unto me, that I may set my eye upon him.
Nawe ukawambia matumishi wako, 'Mleteni ili nimwone.'
22 And we said unto my lord, The lad cannot leave his father; for if he should leave his father, he would die.
Nasi tukamwambia bwana wangu, 'Kijana hawezi kumwacha babaye. Kwani akimwacha babaye baba yake angekufa.'
23 And thou saidst unto thy servants, Except your youngest brother come down with you, ye shall not see my face any more.
Na ukawambia watumishi wako, 'Mdogo wenu asipokuja pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.'
24 And it came to pass, when we came up unto thy servant my father, that we told him the words of my lord.
Na ikawa tulipokwenda kwa mtumishi wako baba yangu, tulimwambia maneno ya bwana wangu.
25 And our father said, Go back and buy us a little food.
Na baba yetu akasema, Nendeni tena, mkatununulie chakula.'
26 And we said, We cannot go down: if our youngest brother be with us, then will we go down; for we cannot see the man's face, except our youngest brother be with us.
Nasi tukasema, “Hatuwezi kushuka. Ikiwa mdogo wetu atakuwa nasi, ndipo tutakaposhuka, kwani hatuwezi kuuona uso wa mtu yule mdogo wetu asipokuwa pamoja nasi.'
27 And thy servant my father said unto us, Ye know that my wife bore me two sons;
Mtumishi wako baba yetu akatwambia, 'Mnajua kwamba mke wangu alinizalia wana wawili.
28 And the one went out from me, and I said, Surely he hath been torn to pieces; and I have not seen him up to this time.
Na mmoja akatoka kwangu nami nikasema, “Bila shaka ameraruliwa vipande, na tangu hapo sijamwona.”
29 And if ye take this one also from me, and mischief befall him, ye will bring down my gray hairs with sorrow to the grave. (Sheol )
Nanyi mkimchukua huyu naye kutoka kwangu mabaya yanaweza kumpata, mtashusha mvi zangu kwa kaburini kwa huzuni. (Sheol )
30 And now, when I come to thy servant my father, and the lad be not with us; seeing that his life is bound up in the lad's life;
Kwa hiyo, basi, nitapokuja kwa mtumishi wako baba yangu, na kijana hayupo nasi, kwa kuwa uhai wake umefungamanishwa katika uhai wa kijana,
31 It will come to pass, that when he seeth that the lad is not with us, he will die: and thy servants would thus bring down the gray hairs of thy servant our father with sorrow to the grave. (Sheol )
itakuwa, atakapoona kwamba kijana hayupo nasi atakufa. Na watumishi wako watazishusha mvi za mtumishi wako baba yetu kaburini kwa masikitiko. (Sheol )
32 For thy servant became surety for the lad unto my father, saying, If I bring him not unto thee, then shall I have sinned against my father all the days.
Kwani mtumishi wako alikuwa mdhamini wa kijana kwa baba yangu na alisema, 'Ikiwa sitamleta kwako, ndipo nitakapokuwa mwenye hatia kwa baba yangu daima.”
33 Now therefore, I pray thee, let thy servant abide instead of the lad as bond-man to my lord; and let the lad go up with his brothers.
Kwa hiyo sasa, tafadhari mwache mtumishi wake akae kama mtumwa kwa bwana wangu badala ya kijana, na umwache kijana aende na ndugu zake.
34 For how shall I go up to my father, and the lad be not with me? I should perhaps be compelled to witness the evil which would come on my father.
Kwa maana nitakwenda jinsi gani kwa baba yangu ikiwa kijana hayupo nami? Ninaogopa kuona mabaya yatakayompata baba yangu.”