< Genesis 20 >
1 And Abraham journeyed from there toward the south country, and dwelt between Kadesh and Shur and sojourned in Gerar.
Abraham akasafiri kutoka pale hadi nchi ya Negebu, na akakaa kati ya Kadeshi na Shuri. Akawa mgeni akiishi Gerari.
2 And Abraham said of Sarah his wife, She is my sister; and Abimelech the king of Gerar sent and took Sarah.
Abraham akasema kususu mkewe Sara, “ni dada yangu.” Kwa hiyo Abimeleki mfalme wa Gerari akatuma watu wake kumchukua Sara.
3 But God came to Abimelech in a dream by night, and said to him, Behold, thou shalt die for the sake of the woman whom thou hast taken; for she is a man's wife.
Lakini Mungu akamtokea Abimeleki usiku katika ndoto, akamwambia, “Tazama, wewe ni mfu kutokana na mwanamke uliye mchukua, kwa kuwa ni mke wa mtu.”
4 But Abimelech had not come near to her; and he said, Lord, wilt thou then slay also a righteous nation?
Basi Abimeleki alikuwa bado hajamkaribia hivyo akasema, “Bwana, Je utaua hata taifa lenye haki?
5 Said he not unto me, She is my sister? and she, even she herself, said, He is my brother; in the integrity of my heart and the innocency of my hands have I done this.
Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?' Hata Sara mwenyewe alisema, 'ni kaka yangu.' Nimefanya hili katika uadilifu wa moyo wangu na katika mikono isiyo na hatia.”
6 And God said unto him in the dream, Yea, I also well know that thou hast done this in the integrity of thy heart; therefore did I also withhold thee from sinning against me; for this cause I suffered thee not to touch her.
Kisha Mungu akasema naye katika ndoto, “Kweli, ninajua pia kwamba umefanya hili katika uadilifu wa moyo wako, na pia nilikuzuia usitende dhambi dhidi yangu mimi. Ndiyo maana sikuruhusu umshike.
7 And now restore the man's wife, for he is a prophet, and he will pray for thee, that thou mayest live; and if thou restore her not, know thou, that thou shalt surety die, thou and all that are thine.
Kwa hiyo, mrudishe huyo mke wa mtu, kwa kuwa ni nabii. Atakuombea, na utaishi. Lakini usipo mrudisha, ujuwe kwamba wewe pamoja na wote walio wa kwako mtakufa hakika.
8 And Abimelech rose early in the morning, and called all his servants, and told all these things in their hearing; and the men were greatly afraid.
Abimeleki akaamka asubuhi na mapema akawaita watumishi wake wote waje kwake. Akawasimulia mambo haya yote, na watu wale wakaogopa sana.
9 Then Abimelech called Abraham, and said unto him, What hast thou done unto us? and in what have I offended thee, that thou hast brought on me and on my kingdom a great sin? deeds that ought not to be done thou hast done unto me.
Kisha Abimeleki akamwita Abraham na kumwambia, “Umetufanyia jambo gani? Ni kwa jinsi gani nimekutenda dhambi kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi hii kubwa? Umenifanyia mimi jambo ambalo halipaswi kufanywa.”
10 And Abimelech said unto Abraham, What sawest thou, that thou didst this thing?
Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini kilikushawishi wewe kutenda jambo hili?”
11 And Abraham said, Because I thought, Surely there is no fear of God in this place, and they will slay me for the sake of my wife.
Abraham akasema, “Ni kwasababu nilifikiri hakika hakuna hofu ya Mungu katika sehemu hii, na kwamba wataniua kwa ajili ya mke wangu.'
12 And yet indeed she is my sister, the daughter of my father, but not the daughter of my mother; and she became my wife.
Licha ya kwamba kweli ni dada yangu, binti wa baba yangu, ingawa si binti wa mama yangu; na ndiye alifanyika kuwa mke wangu.
13 And it came to pass, when God caused me to wander from my father's house, that I said unto her, This is thy kindness which thou shalt show unto me; at every place whither we shall come, say of me, He is my brother.
Wakati Mungu aliponiondoa katika nyumba ya baba yangu na kusafiri kutoka mahali kwenda mahali pengine, nilimwambia mke wangu, kwa kila sehemu tutakayo kwenda, unioneshe uaminifu wako kama mke wangu: Kila mahali tutakapo kwenda, useme juu yangu kuwa, “Ni kaka yangu.”'''
14 And Abimelech took sheep, and oxen, and men-servants, and women-servants, and gave them unto Abraham, and restored to him Sarah his wife.
Ndipo Abimeleki akatwaa kondoo, maksai, watumwa wa kiume na wa kike akampatia Abraham. Basi Abimeleki akamrudisha Sara, mke wa Abraham.
15 And Abimelech said, Behold, my land is before thee: dwell where it is pleasing in thy eyes.
Abimeleki akasema, Tazama, Nchi yangu i mbele yako. Kaa mahali utakapopendezewa.”
16 And unto Sarah he said, Behold, I have given thy brother a thousand pieces of silver: behold, this is to thee a covering of the eyes unto all that are with thee; and with all others thou canst thus justify thyself.
Na kwa Sara akasema, Tazama, nimempatia kaka yako vipande elfu vya fedha. Navyo ni kwa ajili ya kufunika kosa lolote dhidi yako machoni pa wote walio pamoja na wewe, na mbele ya kila mtu ambaye umemfanya kuwa na haki.”
17 And Abraham prayed unto God; and God healed Abimelech, and his wife, and his maid-servants, so that they could bear children.
Kisha Abraham akaomba kwa Mungu, Na Mungu akamponya Abimeleki, mkewe, na watumwa wake wa kike kiasi kwamba wakaweza kupata watoto.
18 For the Lord had fast closed up every womb of the house of Abimelech, because of Sarah, Abraham's wife.
Kwa kuwa Yahwe alikuwa amewafanya wanawake wote wa nyumaba ya Abimeleki kuwa tasa kabisa, kwa sababu ya Sara, mke wa Abraham.