< Genesis 19 >
1 And the two angels came to Sodom in the evening, and Lot was sitting in the gate of Sodom; and when Lot saw them he rose up to meet them, and he bowed himself with his face to the ground.
Malaika wawili wakaja Sodoma jioni, wakati ambao Lutu alikuwa amekaa langoni mwa Sodoma. Lutu akawaona, akainuka kuwalaki, na akainama uso wake chini ardhini.
2 And he said, Behold now, my lords, turn in, I pray you, into your servant's house, and tarry all night, and wash your feet, and ye can rise up early, and go on your way. And they said, Nay; but we will abide in the street all night.
Akasema, Tafadhari Bwana zangu, nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu, mlale pale usiku na muoshe miguu yenu. Kisha muamke asubuhi na mapema muondoke.” Nao wakasema, “Hapana, usiku tutalala mjini.”
3 And he pressed upon them greatly, and they turned in unto him, and entered into his house; and he made them a feast, and baked unleavened bread, and they did eat.
Lakini akawasihi sana, mwishowe wakaondoka pamoja nae, na wakaingia katika nyumba yake. Akaandaa chakula na kuoka mkate usiotiwa chachu, wakala.
4 But before they had lain down, the men of the city, even the men of Sodom, compassed the house round, both old and young, all the people from every quarter:
Lakini kabla hawaja lala, wanaume wa mji, wa Sodoma, vijana kwa wazee wakaizunguka nyumba, wanaume wote kutoka kila kona ya mji.
5 And they called unto Lot, and said unto him, Where are the men who came in to thee this night? bring them out unto us, that we may know them.
Wakamwita Lutu, na kumwambia, “Wale wanaume walioingia kwako usiku wakowapi? watoe hapa nje waje kwetu, ili tuweze kulala nao.”
6 And Lot went out unto them, at the entrance [of the house], and shut the door after him.
Lutu akatoka nje na akafunga mlango.
7 And he said, I pray you, my brethren, do not act wickedly.
Akasema, “Nawasihi, ndugu zangu, msitende uovu.
8 Behold now, I have two daughters who have not known man; let me, I pray you, bring them out unto you, and do ye to them as is good in your eyes, only unto these men do nothing, since they have once come under the shadow of my roof.
Tazama, nina mabinti wawili ambao hawajawahi kulala na mwanaume yeyote. Nawaomba tafadhari niwalete kwenu, na muwafanyie lolote muonalo kuwa jema machoni penu. Msitende lolote kwa wanaume hawa, kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha dari yangu.”
9 And they said, Stand back. And they said, This one man came in to sojourn, and he will needs be a judge; now will we deal worse with thee than with them. And they pressed sorely upon the man Lot, and they came near to break the door.
Wakasema, “Ondoka hapa!” Wakasema pia, huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni, na sasa amekuwa mwamuzi! Sasa tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao.” Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango.
10 But the men put forth their hand, and pulled Lot to them into the house, and the door they locked.
Lakini wale wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga mlango.
11 And the men that were at the entrance of the house they smote with blindness, both small and great, so that they wearied themselves to find the entrance.
Kisha wale wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume waliokuwa nje ya nyumba, vijana na wazee kwa pamoja, kiasi kwamba wakachoka wakati wakiutafuta mlango.
12 And the men said unto Lot, Hast thou here any besides? a son-in-law, and thy sons, and thy daughters, and whatsoever thou hast in the city, bring out of this place.
Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je una mtu mwingine yeyote hapa? wakwe zako, wanao na mabinti zako, na yeyote mwingine katika huu mji, ukawatoe hapa.
13 For we will destroy this place, because the cry against them is waxed great before the face of the Lord; and the Lord hath sent us to destroy it.
Kwa kuwa tunakaribia kuiangamiza sehemu hii, kwa sababu mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi kiasi kwamba ametutuma kuuangamiza.”
14 And Lot went out and spoke unto his sons-in-law, who were to marry his daughters, and said, Arise, get yourselves out of this place, for the Lord will destroy this city; but he seemed as one that jesteth in the eyes of his sons-in-law.
Lutu akatoka na akazungumza na wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake, akawambia, “Ondokeni upesi mahali hapa, kwa kuwa Yahwe anakaribia kuuangamiza mji.” Lakini kwa wakwe zake alionekana kuwa anawatania.
15 And as the morning dawn arose, the angels urged Lot, saying, Arise, take thy wife, and thy two daughters that are here, lest thou be consumed for the iniquity of the city.
Alfajiri, malaika wakamsihi Lutu, wakisema, ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili ambao wako hapa, ili kwamba usipotelee katika adhabu ya mji huu.”
16 And while he yet lingered, the men laid hold of his hand, and of the hand of his wife, and of the hand of his two daughters, because the Lord desired to spare him; and they brought him forth, and set him without the city.
Lakini akakawia-kawia. Kwa hiyo watu wale wakamshika mkono wake, na mkono wa mkewe, na mikono ya binti zake wawili, kwa sababu Yahwe alimhurumia. Wakawatoa nje, na kuwaweka nje ya mji.
17 And it came to pass, when they had brought them forth abroad, that he said, Escape for thy life, look not behind thee, neither stay thou in all the plain; escape to the mountain, lest thou be consumed.
Wakisha kuwatoa nje mmoja wa wale watu akasema, “jiponye nafsi yako! usitazame nyuma, au usikae mahali popote kwenye hili bonde. Toroka uende milimani ili kwamba usije ukatoweshwa mbali.”
18 And Lot said unto them, Oh, not so, my lord!
Lutu akawambia, “Hapana, tafadhali bwana zangu!
19 Behold now, thy servant hath found grace in thy eyes, and thou hast magnified thy kindness, which thou hast showed unto me in saving my life; and I cannot escape to the mountain, lest the evil overtake me, and I die.
Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako, na umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu, lakini sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa.
20 Behold now, this city is near to flee thereunto, and it is little; oh, let me, I pray thee, escape thither, [as it is but little, ] that my life may be saved.
Tazama, ule mji pale uko karibu nijisalimishe pale, na ni mdogo. Tafadhari niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa.”
21 And he said unto him, See, I have favored thee concerning this thing also, that I will not overthrow this city, of which thou hast spoken.
Akamwambia, “Sawa, nimekubali ombi hili pia, kwamba sitaangamiza mji ambaoumeutaja.
22 Haste thee, escape thither; for I cannot do any thing till thou hast come thither. Therefore was the name of the city called Zoar.
Harakisha! toroka uende pale, kwa kuwa sitafanya chochote mpaka ufike pale.” kwa hiyo mji ule ukaitwa Soari.
23 The sun rose over the earth, when Lot entered into Zoar.
Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi wakati Lutu alipofika Soari.
24 And the Lord rained upon Sodom and upon Gomorrah brimstone and fire, from the Lord, out of heaven;
Kisha Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni.
25 And he overthrew those cities, and all the plain, and all the inhabitants of the cities, and that which grew upon the ground.
Akaharibu miji ile, na bonde lote, na vyote vilivyomo katika miji, na mimea iliyo chipua juu ya ardhi.
26 But his wife looked back from behind him, and she became a pillar of salt.
Lakini mke wa Lutu aliye kuwa nyuma yake, akatazama nyuma, na akawa nguzo ya chumvi.
27 And Abraham got up early in the morning to the place where he had stood before the Lord:
Abraham akaamuka asubuhi na mapema akaenda mahali alipokuwa amesimama mbele ya Yahwe.
28 And he looked toward Sodom and Gomorrah, and toward all the land of the plain, and beheld, and lo, smoke went up from the earth as the smoke of a furnace.
Akatazama chini kuelekea Sodoma na Gomora na kuelekea katika nchi yote bondeni. Akaona na tazama, moshi ulikuwauki ukienda juu kutoka chini kama moshi wa tanuru.
29 And it came to pass, when God destroyed the cities of the plain, that God remembered Abraham, and sent Lot away out of the midst of the overthrow, when he overthrew the cities in which Lot had dwelt.
Wakati Mungu alipoharibu miji ya bondeni, Mungu akamkumbuka Abraham. Akamtoa Lutu kutoka katika maangamizi alipoangamiza miji ambayo katika hiyo Lutu aliishi.
30 And Lot went up out of Zoar, and dwelt in the mountain, and his two daughters with him, for he feared to dwell in Zoar; and he dwelt in a cave, he, and his two daughters.
Lakini Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima akiwa pamoja na binti zake wawili, kwa sababu aliogopa kuishi Soari. Kwa hiyo akaishi pangoni, yeye na binti zake wawili.
31 And the first-born said unto the younger, Our father is old, and there is not a man in the country to come in unto us after the manner of all the earth:
Yule wa kwanza akamwambia yule mdogo, “Baba yetu ni mzee, na hakuna mwanaume mahali popote wa kulala na sisi kulingana na desturi ya dunia yote.
32 Come, let us make our father drink wine, and we will lie with him, that we may preserve seed of our father.
Njoo na tumnyweshe baba yetu mvinyo na tulale naye ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
33 And they made their father drink wine that night; and the first-born went in, and lay with her father, and he perceived not when she lay down, nor when she arose.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yako mvinyo usiku ule. Kisha yule wa kwanza akaingia na akalala na baba yake; Baba yake hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka.
34 And it came to pass on the morrow, that the first-born said unto the younger, Behold, I lay yesternight with my father; let us make him drink wine this night also, and go thou in, and lie with him, that we may preserve seed of our father.
Siku iliyo fuata yule wa kwanza akamwambia mdogowake, “Sikiliza, usiku wa jana nililala na baba yangu. Na tumnyweshe mvinyo usiku wa leo pia, na uingie ukalale naye. Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu.”
35 And they made their father drink wine that night also; and the younger arose, and lay with him, and he perceived not when she lay down, nor when she arose.
Kwa hiyo wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule pia, na yule mdogo akaenda na akalala naye. Baba yake hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka.
36 And both the daughters of Lot became with child by their father.
Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
37 And the first-born bore a son, and called his name Moab; the same is the father of the Moabites unto this day.
Wa kwanza akazaa mwana wa kiume, na akamwita jina lake Moabu. Akawa ndiye baba wa wamoabu hata leo.
38 And the younger, she also bore a son, and called his name Ben-ammi: the same is the father of the children of Ammon unto this day.
Nayule mdogo naye akazaa mwana wa kiume, na akamwita Benami. Huyu ndiye baba wa watu wa Waamoni hata leo.