< Ezra 3 >

1 And when the seventh month drew near, and the children of Israel were in the cities, the people gathered themselves together as one man to Jerusalem.
Ilikuwa miezi saba baaada ya watu wa Israeli kurudi kwenye miji yao, ndipo walipojikusanya pamoja kama mtu mmoja katika Yerusalem.
2 Then arose Jeshua' the son of Jozadak, and his brethren the priests, and Zerubbabel the son of Shealthiel, and his brethren, and they built the altar of the God of Israel, to offer thereon burnt-offerings, as it is written in the law of Moses the man of God.
Yeshua mwana wa Yosadaki na kaka yake kuhani, na Zerubabeli mwana wa Sheatieli na kaka yake wakainuka na kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli na kutoa sadaka ya kuteketezwa kama ilivyoagizwa katika sheria ya Musa, Mtu wa Mungu.
3 And they erected the altar upon its foundations; for there was fear upon them because of the people of these countries; and they offered thereon burnt-offerings unto the Lord, burnt-offerings at morning and at evening.
Ndipo wakaanzisha madhabahu juu ya msingi, kwa hofu waliokuwa nayo kwa sababu ya watu wa nchi/ Wakatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe asubuhi na jioni.
4 And they celebrated the feast of tabernacles, as it is written, and [offered] the daily burnt-offerings by number, according to the prescribed manner, the offering of every day on its day;
Pia vilevile wakaichunguza sikukuu ya vibanda kama ilivyoandikwa na wakatoa sadaka ya kuteketezwa siku kwa siku kama ilivyoagizwa, kila siku kwa siku yake.
5 And afterward the continual burnt-offering, and that for the new moons, and for all the feasts of the Lord that are hallowed, and that of every one who willingly offered a free-will offering unto the Lord.
Kulikuwa na sadaka ya kila siku ya kuteketezwa na mwezi mara moja na sadaka za siku ya Yahwe za kudumu, pamoja na sadaka zote za hiari.
6 From the first day of the seventh month began they to offer burnt-offerings unto the Lord: although the foundation of the temple of the Lord had not yet been laid.
Walianza kutoa sadaka za kuteketezwa za Yahwe siku ya kwanza ya mwezi wa saba, ingawa hekalu lilikuwa halijaanza kujengwa.
7 Then did they give money unto the masons, and to the carpenters; and food, and drink, and oil, unto the Zidonians and Tyrians, to bring cedar-trees from the Lebanon by sea to Joppa, according to the permission of Cyrus the king of Persia for them.
Hivyo wakatoa fedha kwa wahunzi na fundi wa mkono, na wakawapa chakula, vinywaji na mafuta kwa watu wa Sidoni na Tiro, ili kwamba walete miti ya mierezi kupitia baharini kutoka Lebanoni mpaka Yafa, na kama walivyo ruhusiwa na mfalme Koreshi wa Uajemi.
8 And in the second year of their coming unto the house of God at Jerusalem, in the second month, did Zerubbabel the son of Shealthiel and Jeshua' the son of Jozadak, and the remainder of their brethren the priests and the Levites, and all they that were come out of the captivity unto Jerusalem make a beginning; and they appointed the Levites, from twenty years old and upward, to superintend the work of the house of the Lord.
Ndipo mwezi wa pili katika mwaka wa pili baadae wakaja kwenye nyumba ya Mungu Yerusalem, Zerubabeli, Yoshua mwana wa Yosadaki, na baadhi ya makuhani na walawi na wale walikuja kutoka uhamishoni kurudi Yerusalem wakaanza kazi. Wakawachagua walawi walikuwa na miaka ishirini na zaidi kusimamia kazi ya nyumba ya Yahwe,
9 Then stood forward Jeshua' with his sons and his brethren, Kadmiel and his sons, the sons of Judah, as one man, to superintend the workmen in the house of God; [also] the sons of Chenadad, their sons and their brethren the Levites.
Yoshua akamsimamisha kijana wake na kaka yake, Kadmiel na watoto wake, na kizazi cha yuda kusimamia kufanya kazi katika nyumba ya Mungu. Pamoja na wao kulikuwa na wana wa Henadadi, na uzao wao, na pia jamaa zao walawi.
10 And when the builders laid the foundation of the temple of the Lord, they placed the priests in their apparel with trumpets, and the Levites the sons of Assaph with cymbals, to praise the Lord, after the manner of David the king of Israel.
Wajenzi wakasimamisha msingi wa Hekalu la Yahwe, Na hii ikawawezesha makuhani kusimama na mavazi yao wakiwa na tarumbeta, na walawi wana wa Asafu, kumtukuza Yahwe kwa matoazi, kama mkono wa mfalme Daudi wa Israel alivyoagiza.
11 And they sang responsively in praise and thanksgiving unto the Lord; because he is good, for unto everlasting endureth his kindness toward Israel. And all the people shouted with a great shout, while praising the Lord; because the foundation of the house of the Lord had been laid.
Waliimba kwa kumsifu na kumshukuru Yahwe. “Yeye ni mwema! Agano lake ni kweli kwa Israel ladumu milele.”Watu wote wakapiga kelele kwa sauti kuu za shangwe wakimsifu Yahwe kwa sababu misingi ya Hekalu ilikuwa imekamilika.
12 But many of the priests and Levites and chiefs of the divisions, the aged, who had seen the first house, when the foundation of this house was laid before their eyes, wept with a loud voice, while many, shouting for joy, raised aloud their voice:
Lakini wengi wa Makuhani, walawi, wakuu wa kale, na wazeee wa zamani walioiona nyumba ya kwanza, wakati misingi ilipowekwa wakaishuhudia kwa macho yao, walilia kwa sauti. Lakiniwengi walipiga kelele kwa sauti za shangwe na furaha na sauti za kushangaza.
13 So that the people could not distinguish the noise of the shout of joy from the noise of the weeping of the people; for the people shouted with a loud shout, and the noise was heard ever so far off.
Na matokeo yake, watu hawakuweza kutofautisha sauti za furaha na sauti za shangwe na sauti za watu waliokuwa wanalia, kwa kuwa watu walikuwa wanalia kwa sauti kuu ya shangwe na sauti ilisikika kutoka mbali.

< Ezra 3 >