< Ezekiel 43 >

1 Then did he lead me to the gate, even the gate that was turned in an eastern direction.
Yule mtu kisha akanileta hata kwenye lango lililokuwa linaelekea mashariki.
2 And, behold, the glory of the God of Israel came from the way of the east; and his voice was like a noise of many waters; and the earth gave light from his glory.
Tazama! Utukufu wa Mungu wa Israeli ukaja kutoka mashariki; sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi, na nchi iling'aa kwa utukufu wake.
3 And it was like the appearance of the vision which I had seen, yea, like the vision that I had seen when I came to destroy the city; and the visions were like the vision that I had seen by the river Kebar: and I fell upon my face.
Yalikuwa yanalingana na sura ya ono nililolona, kulingana na ono nililokuwa nimeliona wakati alipokuja kuuteketeza mji, na maono yalikuwa kama maono ambayo niliyokuwa nimeyaona Keberi Kanali nikaanguka kifudi fudi.
4 And the glory of the Lord came into the house by the way of the gate which was turned in an eastern direction.
Hivyo utukufu wa Yahwe ukaja kwenye nyumba ya karibu na njia ya lango lililokuwa wazi kwa upande wa magharibi.
5 Then did the Spirit take me up, and bring me into the inner court: and, behold, the glory of the Lord filled the house.
Kisha Roho akanichukua na kunileta kwenye ua wa ndanni. Tazama! Utukufu wa Yahwe ulikuwa umeijaza nyumba.
6 And I heard him speaking unto me out of the house; and a man was standing alongside of me.
Mtu alisimama karibu na mimi, na nikamsikia mtu mwingine akizungumza na mimi kutoka kwenye nyumba.
7 And he said unto me, Son of man, [this] is the place of my throne, and the place of the soles of my feet, where I will dwell in the midst of the children of Israel forever: and the house of Israel shall not defile any more my holy name, neither they, nor their kings, by their lewdness, nor by the carcasses of their kings on their high-places.
Akanambia, “Mwanadamu, hapa ndipo mahali pangu pa enzi na mahali kwa ajili ya ya miguu yangu, ambapo nitaishi kati ya watu wa Israeli milele. Nyumba ya Israeli haitalikufuru tena jina langu takatifu-wao au wafalme wao katika mahali patakatifu pao.
8 Inasmuch as they placed their threshold by my threshold, and their door-posts close by my door-posts, and the wall being only between me and them, and they defiled my holy name by their abominations which they committed; so that I made an end of them in my anger.
Hawatalikufuru tena jina langu takatifu kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu, na nguzo yao ya lango karibu na nguzo yangu ya lango, bila kitu lakini ukuta kati yangu na wao. Wamelikufuru jina langu kwa matendo yao machafu, hivyo nimewala kwa hasira yangu.
9 Now will they have to put away their lewdness, and the carcasses of their kings, far from me, and I will dwell in the midst of them for ever.
Sasa waache waondoe udanganyifu wao na maiti za wafalme wao kutoka kwangu, na nitaishi katikati yao milele.
10 Thou, son of man, tell the house of Israel of the house, that they may be confounded because of their iniquities: and let them measure the outlines.
Mwanadamu, wewe mwenyewe utaiambia nyumba ya Israeli kuhusu nyumba hii hivyo watajiskia aibu ya uovu wao. Wanaweza kutafakari kuhusu haya maelezo.
11 And if they be confounded because of all that they have done: then let them know the form of the house, and its arrangements, and its means of egress, and its entrances, and all its forms, and all its statutes, and all its forms, and all its laws, and write them down before their eyes; that they may observe the whole of its form, and all its statutes, and carry them out.
Kwa kuwa wameaibika kwa yote waliyoyafanya, kisha waonyeshe mchoro wa nyumba, maelezo yake, matokeo yake, maingio yake, na mchoro wake, sheria zake zote na kanuni. Kisha andika hivi chini mbele ya macho yao ili waweze kutunza michoro yote na kanuni zake zote, hivyo kama wazitiivo.
12 This is the law for the house, Upon the top of the mount shall its whole limit all round about be most holy: behold, this is the law for the house.
Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba: Kutoka kwenye kilele cha mlima hata mpaka wote unaoizunguka, patakuwa patakatifu sana. Tazama! Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba.
13 And these are the measures of the altar in cubits, The cubit is a cubit and a hand-breadth; and the bottom shall be a cubit high, and a cubit broad, and its border on its edge round about shall be a span: and this shall be the outside of the altar.
Hivi vitakuwa vipimo vya madhabahu katika dhiraa-hiyo dhiraa kuwa dhiraa ya kawaida na urefu wa kiganja. Hivyo mfereji ulio uzunguka madhabahu utakuwa dhiraa moja chini, na upana wake pia utakuwa dhiraa moja. Mpaka wa karibu uizungukayo machinjio shubiri moja. Hii itakuwa kitako cha madhabahu.
14 And from the bottom upon the ground up to the lower projection shall be two cubits, and the breadth one cubit; and from the lesser projection up to the greater projection shall be four cubits, and the breadth one cubit.
Usawa wa kutoka kwenye mferji hadi kwenye machinijo ya chini ya madhabahu itakuwa dhiraa mbili, na hiyo machinjio yenyewe itakuwa dhiraa moja upana. Kisha kutoka machinjio madogo hadi kwenye machinjio makubwa ya madhabahu, itakuwa dhiraa nne, na machinjio makubwa yatakuwa dhraa moja upana.
15 And the upper portion of the altar shall be four cubits; and from the upper surface of the altar and upward shall be the four horns.
Meko juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ni dhiraa nne juu, na kuna pembe nne zilizoelekea juu kwenye meku.
16 And the upper surface of the altar shall be twelve cubits long, by twelve broad, square on its four sides.
Meku ina dhiraa kumi na moja urefu na dhiraa kumi na mbili upana, za mraba.
17 And the projection shall be fourteen cubits in length, by fourteen in breadth on its four sides; and the border round about it shall be half a cubit; and its bottom shall be a cubit round about; and its steps shall look toward the east.
Mpaka wake ni dhiraa kumi na nne urefu na dhiraa kumi na nne upana pande zake zote nne, na ukingo wake ni nusu dhiraa upana. Mfereji ni dhiraa moja upana kuzuka kote pamoja na ngazi zielekeazo mashariki.”
18 And he said unto me, Son of man, thus hath said the Lord Eternal, These are the statutes of the altar on the day when it shall be finished, to offer thereon burnt-offerings, and to sprinkle thereon blood.
Kisha akanambia, “Mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Hizi ndizo sheria kwa ajili ya madhabahu katika siku watakayoitengeza, kwa ajili kutoa sadaka ya kuteketezwa kwenye hiyo, na kwa jili ya kunyunyiza damu juu yake.
19 And thou shalt give to the priests the Levites that are of the seed of Zadok, who approach unto me, saith the Lord Eternal, to minister unto me, a young bullock for a sin-offering.
Utatoa ng'ombe kutoka kwenye kundi kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya Walawi makuhani ambao ni uzao wa Zadoki, wale wajao karibu nami kunitumikia-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
20 And thou shalt take of his blood, and put it on its four horns, and on the four corners of the projection, and upon the border round about; and thou shalt cleanse it and make an atonement for it.
Kisha utachukua baadhi ya damu yake na kuiweka juu pembe nne za madhabahu na pande nne za machinjio na kuuzunguka ukingo; utaitakasa na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 And thou shalt take the bullock of the sin-offering, and some one shall burn him at an appointed place of the house, without the sanctuary.
Kisha chukua ng'ombe kama sadaka ya dhambi na iteketezwe katika eneneo lililotengwa la nje ya patakatifu.
22 And on the second day shalt thou offer a he-goat without blemish for a sin-offering: and they shall cleanse the altar, as they did cleanse it with the bullock.
Kisha katika siku ya pili utatoa mbuzi dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini kama sadaka ya dhambi; makuhani wataisafisha madhabahu kama walivyoisafisha kwa ng'ombe.
23 When thou hast made an end of cleansing it, shalt thou offer a young bullock without blemish, and a ram out of the flock without blemish.
Utakapomaliza kusafisha, toa ng'ombe asiyekuwa na dosari kutoka kwenye mifugo na kondoo dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini.
24 And thou shalt bring them near before the Lord, and the priests shall throw salt upon them, and they shall offer them up as a burnt-offering unto the Lord.
Watoe mbele ya Yahwe; makuhani watanyunyiza chumvi juu yao na kuwainua juu kama sadaka ya kutekezwa kwa Yahwe.
25 Seven days shalt thou prepare a goat for a sin-offering every day; and a young bullock, and a ram out of the flock, without blemish shall they prepare.
Utaandaa mbuzi dume kama sadaka ya dhambi kila siku kwa mda wa siku saba, na makuhani pia wataandaa ng'ombe asiye na dosari kutoka kwenye kundi na kondoo dume kutoka kwenye kundi.
26 Seven days shall they atone for the altar and purify it; and they shall consecrate the same.
Wataipatanisha madhabahu kwa siku saba na kuitakasa, wataitakasa kwa njia hii.
27 And when these days are expired, it shall be, that on the eighth day, and thenceforward, the priests shall prepare upon the altar your burnt-offerings, and your peace-offerings: and I will accept you in favor, saith the Lord Eternal.
Watamaliza hizi siku saba, na katika siku ya nane na kuendelea itakuwa kwamba makuhani wataandaa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani kwenye madhabahu, ndipo nitakapowakubali-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 43 >