< Ezekiel 33 >

1 And the word of the Lord came unto me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Son of man, speak to the children of thy people, and say unto them, If there be a land over which I bring the sword, and the people of the land take a man from among themselves, and appoint him unto themselves for a watchman;
“Mwanadamu, sema hivi kwa watu wako; waambie, 'Nitakapoleta upanga juu ya nchi, kisha watu wa hiyo nchi wakamchukua mtu mmoja kutoka mingoni mwao na kumfanya awe mlinzi wao.
3 And if he see the sword coming over the land, and blow the cornet, and warn the people;
Atazamapo kwa upanga kama unakuja juu ya nchi, na apige tarumbeta kuwaonya watu!
4 And whosoever heareth the sound of the cornet, and taketh no warning; and the sword cometh, and taketh him away: his blood shall be upon his own head.
Kama watu wakisikia sauti ya tarumbeta lakini bila kusikia, na kama upanga ukija na kuwaua, kisha damu ya kila mmoja iko juu ya kichwa chake mwenyewe.
5 The sound of the cornet hath he heard, and he hath taken no warning; his blood shall be upon him. But had he taken warning he would have delivered his soul.
Kama mtu akisikia sauti ya tarumbeta na hakusikiliza, damu yake iko juu yake; lakini kama akisikia, ataokoa maisha yake mwenyewe.
6 But if the watchman see the sword coming, and blow not the cornet, so that the people be not warned, and the sword cometh, and taketh away from among them some person: this one is taken away for his iniquity; but his blood will I require from the watchman's hand.
Bali, kama mlinzi akiona upanga unakuja, lakini kama asipopiga tarumbeta, pamoja na matokeo kwamba watu hawajaonywa, na kama upanga ukija na kuchukua uhai wa mtu yeyote, kisha yule mtu akafa kwenye dhambi yake mwenyewe, lakini nitaitaka damu yake kutoka mlinzi.'
7 But as for thee, O son of man, I have appointed thee a watchman unto the house of Israel: so that when thou hearest a word from my mouth, thou shalt warn them from me.
Sasa wewe mwenyewe, mwanadamu! Nimekufanya kuwa mlinzi kwa ajili ya nyumba ya Israeli; utasikia maneno kutoka kinywani mwangu na uwaonye badala yangu.
8 When I say unto the wicked, O wicked one, thou shalt surely die; and thou dost not speak to warn the wicked from his way: that wicked one shall die for his iniquity; but his blood will I require from thy hand.
Kama nikimwambia mtu mwovu, 'Mwovu, hakika utakufa!' lakini kama hutangazi hivi ili kwa ajili ya kumuonya mtu mwovu kuhusu hii njia, kisha huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako!
9 Nevertheless, if thou hast indeed warned the wicked of his way to turn away from it, and he do not turn from his way: he shall certainly die for his iniquity; but thou hast delivered thy soul.
Lakini wewe, kama ukimwonya mwovu kuhusu hii njia, hivyo basi anaweza kurudi kutoka hiyo, na kama kama asipogeuka kutoka njia yake, kisha atakufa katika dhambi yake, lakini wewe mwenyewe utakuwa umeokoa maisha yako.
10 But thou, O son of man, speak unto the house of Israel, Thus do ye speak, saying, Truly our transgressions and our sins are upon us, and through them do we pine away: how then shall we live?
Basi wewe, mwanadamu, sema kwa nyumba ya Israeli, 'Mnasema hivi, Makosa yetu na dhambi zetu zi juu yetu, na tunadhoofika kwa ajili yao! Je! tutaishije?”'
11 Say unto them, As I live, saith the Lord Eternal, I have no pleasure in the death of the wicked; but in the return of the wicked from his way that he may live: return ye, return ye from your evil ways; for why will ye die, O house of Israel?
Waambie, 'Kama niishivyo-asema Bwana Yahwe-sifurahii kifo cha mwovu, kwa kuwa kama mwovu akitubu kutoka njia yake, kisha ataishi! Tubu! Tubu kutoka njia zako mbaya! Kwa nini mnataka kufa, nyumba ya Israeli?'
12 But thou, son of man, say unto the children of thy people, The righteousness of the righteous shall not deliver him on the day of his transgression; and as for the wickedness of the wicked, he shall not stumble through it on the day that he returneth from his wickedness; nor shall the righteous be able to live through the other on the day that he sinneth.
Hivyo basi wewe, mwanadamu, waambe watu wako, 'Haki ya mwenye haki haitamwokoa kama akikosa! Uovu wa mtu mwovu hautamfanya kuangamia kama akitubu dhambi zake! Kwa kuwa mtu mwenye haki hataweza kuishi kwa sababu ya haki yake kama akikosa.
13 When I say of the righteous, that he shall surely live, and he trusteth to his own righteousness, and committeth what is wrong: all his righteous deeds shall not be remembered, and for his wrong that he hath committed, —through this shall he die.
Kama nikisema kwa mwenye haki, “Hakika ataisha!” na kama akiamini katika haki yake na kisha akafanya udhalimu, sitokumbuka haki yake yoyote. Atakufa kwa ajili ya uovu alioufanya.
14 Again, when I say unto the wicked, Thou shalt surely die; and he turneth from his sin, and executeth justice and righteousness;
Hivyo kama nikisema kwa mwovu, “Utakufa hakika,” lakini kama akitubu kutoka kwenye dhambi zake na kufanya yaliyo halali na haki-
15 If the wicked restore the pledge, make restitution for what he hath robbed, walk in the statutes of life, so as not to do any wrong: he shall surely live, he shall not die.
kama akirudisha dhamana ambayo aliyomnyang'anya, au kama akirudisha alichokipoteza, na kama akitembea katika amri zitoazo uhai na bila kufanya dhambi-kisha ataishi hakika. Hatakufa.
16 All his sins that he hath committed shall not be remembered unto him: justice and righteousness hath he executed, he shall surely live.
Dhambi alizozifanya hazitakumbukwa kwa ajili yake. Ametenda halali na haki, na hivyo, ataishi hakika!
17 Yet say the children of thy people, The way of the Lord is not equitable: while, as to them, their way is not equitable.
Lakini watu wako husema, “Njia ya Bwana haiko sawa!” lakini ni njia zako ndizo haziko sawa!
18 When the righteous turneth away from his righteousness, and doth what is wrong, he shall even die therefore.
Wakati mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye haki na kufanya dhambi, kisha atakufa katika hiyo!
19 And when the wicked returneth from his wickedness, and executeth justice and righteousness, he shall surely live therefore.
Wakati mtu mbaya ageukapo kutoka kwenye ubaya wake na kufanya iliyo halali na haki, ataishi kwa sababu ya hayo mambo!
20 Yet ye say, The way of the Lord is not equitable. Every one after his own ways will I judge you, O house of Israel.
Lakini ninyi watu husema, “Njia ya Bwana haiko sawa!” Nitawahukumu kila mmoja wenu kulingana na njia yake, nyumba ya Israeli!”'
21 And it came to pass in the twelfth year, in the tenth month, on the fifth day of the month after our exile, that there came unto me one that had escaped out of Jerusalem, saying, The city hath been smitten.
Ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya tano ya mwezi wa kumi ya uhamisho wetu, mtu mmoja akatoroka kutoka Yerusalemuna kusema, “Mji umetekwa!”
22 Now the inspiration of the Lord was come upon me in the evening, before the coming of the one who had escaped; and he had opened my mouth, before he was come to me in the morning; and my mouth was opened and I was not kept dumb any more.
Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu jioni kabla yule mtoro hajaja, na mdomo wangu ulikuwa wazi mda huo alikuja kwangu wakati wa mapambazuko. Hivyo mdomo wangu ulikuwa wazi; sikuwa bubu tena!
23 And the word of the Lord came unto me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
24 Son of man, they that dwell in these ruins in the land of Israel say as followeth, But one man was Abraham, and he obtained the land as an inheritance; and as we are many, the land must [surely] be given to us for an inheritance.
“Mwanadamu, wale waishio mahali palipoharibika katika nchi ya Israeli huongea na kusema, 'Ibrahimu alikuwa mtu pekee, na alirithi nchi, lakini sisi tukowengi! Tumepewa nchi kama wamiliki.”
25 Therefore say unto them, Thus hath said the Lord Eternal, By the blood do ye eat, and your eyes do you lift up toward your idols, and blood do ye shed: and ye expect to possess the land?
Kwa hiyo waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Mnakula damu, na mmeziinulia macho yenu sanamu, kisha mnazimwagia damu za watu. Je! mna uhakika wa kuimiliki hii nchi?
26 Ye depend upon your sword, ye commit abomination, and ye defile every one his neighbor's wife: and ye expect to possess the land?
Mnategemea upanga wenu na mmetenda mambo maovu; kila mtu amemnajisi mke wa jirani yake. Je! kweli mtaimiliki nchi?'
27 Thus shalt thou say unto them, Thus hath said the Lord Eternal, As I live, surely those that are in the ruined places shall fall by the sword, and him that is in the open field will I give to the beasts that they may devour him, and those that are in the strongholds and in the caves shall die through the pestilence.
Utawaambia hivi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kama niishivyo, hakika wale walio katika uharibifu wataanguka kwa upanga, na nitawapatia wale walio katika mashamba viumbe hai kama chakula, na wale walio katika ngome na mapango watakufa kwa tauni.
28 And I will render the land desolate and wasted, and the pride of her strength shall cease; and the mountains of Israel shall be desolate, with none to pass through them.
Kisha nitairudisha nchi kwenye ukiwa na tishio, na kiburi cha uwezo wake kitakoma, kwa kuwa milima ya Israeli itakuwa jangwa, na hakutakuwa na mtu yeyote atakayewapitia.'
29 And they shall experience that I am the Lord, when I render the land desolate and wasted, because of all their abominations which they have committed.
Hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapoifanya nchi ukiwa na tishio kwa sababu ya machukizo yote waliyoyafanya.
30 And thou, son of man, [there are] the children of thy people, who are talking about thee by the walls and in the entrances of the houses, and speak one to another, every one to his brother, saying, Do come, and hear what the word is which cometh forth from the Lord.
Hivyo basi wewe, mwanadamu-watu wako wanasema mambo yako karibu na kuta na malango ya nyumba, na kila mmoja anaambizana na mwenzake-kila mtu na ndugu yake, 'Twende na tukasikilize neno la nabii lililotoka kwa Yahwe!
31 And then they come unto thee as the people come, and they sit before thee [as] my people, and they hear thy words, but do not execute them; for as merry songs they carry them in their mouth, while their heart goeth after their unlawful gains.
Hivyo watu wangu watakuja kwako, kama wafanyavyo mara nyingi, na nitaketi mbele yako na kusikiliza maneno yako, lakini mioyo yao inafuata udhalimu kwa faida yao.
32 And, lo, thou art unto them as a merry song of one that hath a pleasant voice, and can play well: and [thus] they hear thy words, but execute them not.
Kwa kuwa umekuwa kama wimbo mzuri kwao, sauti nzuri awezaye kucheza kinanda vizuri, hivyo watasikia maneno yako, lakini hakuna atakaye yatii.
33 But when it cometh to pass, [lo, it will come, ] then shall they know that a prophet hath been among them.
Hivyo wakati haya yote yatakapotokea-tazama! itatokea! -watajua yakwamba nabii alikuwa miongoni mwao.”

< Ezekiel 33 >