< Ezekiel 30 >

1 And the word of the Lord came unto me, saying,
Neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Son of man, prophesy and say, Thus hath said the Lord Eternal, Wail ye, Woe unto the day!
“Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
3 For nigh is the day, yea nigh is the day of the Lord; a cloudy day; the time of the nations' [misfortune] shall it be.
siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
4 And the sword shall come into Egypt, and there shall be trembling in Ethiopia, when the slain fall in Egypt, and when they take away its multitude, and its foundations shall be broken down.
Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
5 Ethiopia, and Put, and Lud, and all the confederates, and Cub, and all the men of the leagued land, shall fall with them by the sword.
Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
6 Thus hath said the Lord, Yea, there shall fall those that uphold Egypt; and there shall come down the pride of her strength: from Migdol to Seveneh shall they fall in her by the sword, saith the Lord Eternal.
Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
7 And they shall be made desolate in the midst of the desolate countries, and its cities shall be counted in the midst of the cities that have been laid in ruins.
Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
8 And they shall know that I am the Lord, when I set fire to Egypt, and when all her helpers shall be broken.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
9 On that day shall messengers go forth from my presence in ships to terrify the secure Ethiopians, and there shall be trembling among them, as on the day of Egypt; for, lo, it cometh.
Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
10 Thus hath said the Lord Eternal, I will also cause the multitude of Egypt to cease through the hand of Nebuchadrezzar the king of Babylon.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
11 He and his people with him, the fiercest of nations, shall be brought to destroy the land; and they shall draw their swords against Egypt, and they shall fill the land with the slain.
Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
12 And I will render the streams dry, and sell the land into the hand of evil men; and I will make the land desolate, and all that filleth it, by the hand of strangers: I the Lord have spoken it.
Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
13 Thus hath said the Lord Eternal, I will also destroy the idols, and I will cause false gods to cease out of Noph; and a prince out of the land of Egypt shall there not be any more: and I will lay fear on the land of Egypt.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
14 And I will make Pathros desolate, and set fire to Zo'an; and I will execute judgments in No.
Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
15 And I will pour my fury over Sin, the stronghold of Egypt; and I will cut off the multitude of No.
Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
16 And I will set fire to Egypt: Sin shall have great pain, and No shall be broken in, and [over] Noph shall the besiegers [prevail] by broad day.
Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
17 The young men of Aven and of Pi-besseth shall fall by the sword; and they themselves shall go into captivity.
Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
18 And at Thechaphneches the day shall be darkened, when I break there the yoke-bars of Egypt, and the pride of her strength ceaseth therein: as for her, a cloud shall cover her, and her daughters shall go into captivity.
Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
19 Thus will I execute judgments on Egypt: and they shall know that I am the Lord.
Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
20 And it came to pass in the eleventh year, in the first month, on the seventh day of the month, that the word of the Lord came unto me, saying,
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
21 Son of man, the arm of Pharaoh the king of Egypt have I broken; and lo, it shall not be bound up to apply remedies, to put on a bandage to bind it up, to make it strong that it may grasp the sword.
“Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
22 Therefore thus hath said the Lord Eternal, Behold, I will be against Pharaoh the king of Egypt, and will break his arms, both the strong, and that which was already broken; and I will cause the sword to fall out of his hand.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
23 And I will scatter the Egyptians among the nations, and I will disperse them through the countries.
Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
24 And I will strengthen the arms of the king of Babylon, and will put my sword in his hand; but I will break the arms of Pharaoh, and he shall groan, with the groanings of a deadly wounded man before him.
Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
25 Yea I will make strong the arms of the king of Babylon, but the arms of Pharaoh shall fall down: and they shall know that I am the Lord, when I place my sword into the hand of the king of Babylon, that he may stretch it out over the land of Egypt.
Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
26 And I will scatter the Egyptians among the nations, and disperse them among the countries: and they shall know that I am the Lord.
Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'

< Ezekiel 30 >