< Ezekiel 25 >

1 And the word of the Lord came unto me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Son of man, set thy face against the sons of 'Ammon, and prophesy against them;
“Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
3 And say unto the sons of 'Ammon, Hear ye the word of the Lord Eternal, Thus hath said the Lord Eternal, Because thou hast said, Aha, concerning my sanctuary, when it was profaned; and concerning the land of Israel, when it was made desolate; and concerning the house of Judah, when they went into exile:
Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
4 Therefore, behold, I will give thee up to the children of the east for a possession, and they shall set up their towers in thee, and place in thee their dwellings; they shall indeed eat thy fruit, and they shall surely drink thy milk.
kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
5 And I will change Rabbah into a pasture for camels, and [the land of] the sons of 'Ammon into a resting-place for flocks: and ye shall know that I am the Lord.
Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
6 For thus hath said the Lord Eternal, Whereas thou didst clap thy hands, and stamp with thy feet, and rejoice with all thy derision in the soul over the land of Israel:
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
7 Therefore, behold, will I stretch out my hand over thee, and will give thee up for a spoil to the nations; and I will cut thee off from the people, and I will cause thee to perish out of the countries; I will destroy thee, and thou shalt know that I am the Lord.
Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
8 Thus hath said the Lord Eternal, Because Moab and Se'ir do say, Behold, the house of Judah is like all the nations:
Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
9 Therefore, behold, I will open the side of Moab from the cities, from his cities on his frontiers, the glory of the country, Beth-ha-yeshimoth, Ba'al-me'on, and Kiryathayim,
Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
10 Unto the children of the east [coming] against the sons of 'Ammon, and I will give them in possession; in order that the sons of 'Ammon may not be remembered among the nations.
kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
11 And on Moab will I execute judgments: and they shall know that I am the Lord.
Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
12 Thus hath said the Lord Eternal, Because the Edomites have acted revengefully against the house of Judah, and have greatly offended, and have taken vengeance on them:
Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
13 Therefore thus hath said the Lord Eternal, I will also stretch out my hand against Edom, and cut off from it man and beast; and I will make it a ruined land from Theman; and they of Dedan shall fall by the sword.
Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
14 And I will display my vengeance on Edom by the hand of my people Israel; and they shall do in Edom according to my anger and according to my fury: and they shall feel my vengeance, saith the Lord Eternal.
Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
15 Thus hath said the Lord Eternal, Because the Philistines have acted in revenge, and have taken vengeance with derision in their soul, to destroy out of ancient enmity:
Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
16 Therefore thus hath said the Lord Eternal, Behold, I will stretch out my hand against the Philistines, and I will cut off the Kerethim, and destroy the remnant of the [dwellers] of the sea-coast.
Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
17 And I will execute on them great vengeances with furious chastisements: and they shall know that I am the Lord, when I display my vengeance on them.
Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'

< Ezekiel 25 >