< Exodus 3 >

1 And Moses was keeping the flock of Jithro his father-in-law, the priest of Midian; and he led the flock far away into the desert, and came to the mountain of God, to Choreb.
Wakati huu Musa aliendelea kuchunga mifugo ya Yethro baba mkwe wake, kuhani wa Midiani. Musa aliliongoza kundi la mifugo kuelekea upande wa mbali wa jangwa mpaka kufika Horebu, mlima wa Mungu.
2 And an angel of the Lord appeared unto him in a flame of fire out of the midst of a thorn-bush; and he looked, and, behold, the thorn-bush was burning with fire, but the thorn-bush was not consumed.
Akiwa pale malaika wa Yahwe akamtokea kama mwali wa moto katika kichaka. Musa aliangalia, na tazama, kichaka kiliwaka moto lakini hakikuteketea.
3 And Moses said, I must turn aside, and see this great sight, why the thorn-bush is not burnt.
Musa akasema, “Nitageuka ili nione kitaku hiki cha ajabu, kwa nini kichaka hakiteketei.”
4 And when the Lord saw that he turned aside to see God called unto him out of the midst of the thorn-bush, and said, Moses, Moses; and he said, Here am I.
Yahwe alipoona ya kuwa amegeuka upande ili aone, Mungu alimwita kutoka katika kile kichaka na kusema, “Musa, Musa.” Musa akasema, “Mimi hapa.”
5 And he said, Draw not nigh hither; put off thy shoes from off thy feet; for the place whereon thou standest is holy ground.
Mungu akasema, “Usinikaribie! Vua viatu katika miguu yako, kwa kuwa mahali uliposimama ni mahali palipowekwa wakfu kwa ajili yangu.”
6 And he said, I am the God of thy father, the God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob; and Moses hid his face; for he was afraid to look up to God.
Aliongeza kusema, “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Kisha Musa akaufunika uso wake, kwa kuwa aliogopa kumwangalia Mungu.
7 And the Lord said, I have truly seen the affliction of my people that is in Egypt, and have heard its cry by reason of its taskmasters; yea, I know its sorrows;
Yahwe akasema, “Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri. Nimesikia kelele zao kwa sababu ya mabwana wao, kwa kuwa nayajua mateso yao.
8 And I am come down to deliver it out of the hand of the Egyptians, and to bring it up out of that land unto a land, good and large, unto a land flowing with milk and honey; unto the place of the Canaanites, and the Hittites, and the Emorites, and the Perizzites, and the Hivites, and the Jebusites.
Nimekuja chini kuwaokoa dhidi ya mamlaka ya Wamisri na kuwatoa katika nchi ile na kuwaleta katika nchi nzuri, pana, nchi ijaayo maziwa na asali; kwenye ukanda wa Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
9 Now therefore, behold, the cry of the children of Israel is come unto me: and I have also seen the oppression wherewith the Egyptians oppress them.
Sasa kilio cha watu wa Israeli kimenifikia mimi. Zaidi sana, Mimi nimeyaona mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
10 And now then go, and I will send thee unto Pharaoh, and thou shalt bring forth my people the children of Israel out of Egypt.
Sasa basi, nitakutuma wewe kwa Farao ili upate kuwatoa watu wangu, wana wa Israeli, kutoka katika nchi ya Misri.”
11 And Moses said unto God, Who am I, that I should go unto Pharaoh, and that I should bring forth the children of Israel out of Egypt?
Lakini Musa akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata niende kwa Farao na kuwatoa Waisraeli kutoka Misri?”
12 And he said, Because I will be with thee; and this shall be unto thee the token, that I have sent thee: when thou hast brought forth the people out of Egypt, ye shall serve God upon this mountain.
Mungu akamjibu, “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Hii itakuwa ishara kwako ya kuwa nimekutuma. Utakapokuwa umewatoa watu kutoka Misri, mtaniabubu mimi katika mlima huu.”
13 And Moses said unto God, Behold, if I come unto the children of Israel, and say unto them, The God of your fathers hath sent me unto you; and they then say to me, What is his name? what shall I say unto them?
Musa akamwambia Mungu, “Nikienda kwa Waisraeli na kuwaambia, 'Mungu wa baba zenu amenituma mimi kwenu,' na kisha wakiniambia, 'jina lake nani?' nitawaambia nini?”
14 And God said unto Moses, I will be that I will be: and he said, Thus shalt thou say unto the children of Israel, I will be hath sent me unto you.
Mungu akamwambia Musa, “MIMI NIPO AMBAYE NIPO.” Mungu akasema, “Ni lazima uwaambie Waisraeli, “MIMI NIPO amenituma kwenu.”
15 And God said moreover unto Moses, Thus shalt thou say unto the children of Israel, The Everlasting One, the God of your fathers, the God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob, hath sent me unto you: this is my name for ever, and this is my memorial unto all generations.
Pia Mungu akamwambia Musa, “Lazima uwaambie Waisraeli, 'Yahwe, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amenituma mimi kwenu. Hili ndio jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa na vizazi vyote.'
16 Go, and assemble the elders of Israel, and say unto them, The Everlasting One, the God of your fathers, the God of Abraham, of Isaac, and of Jacob, hath appeared unto me, saying, I have surely taken cognizance of you and of that which is done to you in Egypt:
Nenda ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja. Waambie, 'Yahwe, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, wa Isaka na Yakobo, amenitokea mimi na kusema, “Hakika nimewatazama na nimeona yale mliyotendewa huko Misri.
17 And I have said, I will bring you up out of the affliction of Egypt, unto the land of the Canaanites, and the Hittites, and the Emorites, and the Perizzites, and the Hivites, and the Jebusites, unto a land flowing with milk and honey.
Nimeahidi kuwatoa ninyi katika mateso ya Misri na kuwaleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Wamwori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi. Nchi ijaayo maziwa na asali.”
18 And they will hearken to thy voice: and thou shalt come, thou and the elders of Israel, unto the king of Egypt, and ye shall say unto him, The Everlasting One, the God of the Hebrews hath met with us; and now let us go, we beseech thee, a three days' journey into the wilderness, that we may sacrifice to the Lord our God.
Watakusikiliza. Wewe pamoja na wazee wa Israeeli itawapasa kwenda kwa mfalme wa Misri, na imewapasa kumwambia, 'Yahwe, Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Hivyo tuache sisi twende safari ya siku tatu katika jangwa ili tupate kutoa sadaka kwa Yahwe Mungu wetu.'
19 But I am sure that the king of Egypt will not let you go, unless it happen through a mighty hand.
Lakini nafahamu ya kuwa mfalme wa Misri hatawaacha ninyi mwende, isipokuwa kwa kulazimishwa.
20 And I will stretch out my hand, and smite Egypt with all my wonders which I will do in the midst thereof; and after that he will let you go.
Nitainua mkono wangu na kuwapiga Wamisri kwa miujiza yote nitakayoifanya kati yao. Baada ya hayo, atawaacha mwende.
21 And I will give this people favor in the eyes of the Egyptians; and it shall come to pass, that, when ye go, ye shall not go empty:
Nitawapa watu hawa kufadhiliwa kutoka kwa Wamisri ili muondokapo msiende mikono mitupu.
22 But every woman shall ask of her neighbor, and of her that sojourneth in her house, vessels of silver, and vessels of gold, and garments; and ye shall put them upon your sons, and upon your daughters; and ye shall empty out Egypt.
Kila mwanamke ataomba kwa jirani yake Mmisri na kwa kila mwanamke akaaye kwenye nyumba ya jirani yake, vyombo vya fedha na vya dhahabu na nguo. Nanyi mtawavika watoto wenu wa kiume na binti zenu. Kwa njia hii mtawateka nyara Wamisri.”

< Exodus 3 >