< Exodus 29 >

1 And this is the thing that thou shalt do unto them to hallow them, to become priests unto me: Take one young bullock, and two rams without blemish,
Sasa Hivi ndivyo wapaswa kufanya kuwatenga ili wanitumikie kama makuhani. Chukuwa mtoto wa ng'ombe dume na kondoo bila lawama,
2 And unleavened bread, and unleavened cakes, mingled with oil, and unleavened wafers, anointed with oil; of fine wheaten flour shalt thou make them.
mkate bila hamira, na keki bila hamira iliyo changanywa na mafuta. Pia chukuwa maandazi bila hamira yalio pakwa mafuta. Fanya maandazi kwa unga mzuri wa ngano.
3 And thou shalt put them into one basket, and bring them near in the basket, with the bullock and the two rams.
Lazima uweke kwenye ndoo moja, leta kwenye ndoo, na kuleta pamoja na ng'ombe dume na wana kondoo wawili.
4 And Aaron and his sons shalt thou bring near unto the door of the tabernacle of the congregation, and shalt wash them with water.
Lazima nawe umlete Aruni na wana wake wawili katika lango la kuingilia hema la kukutania. Lazima uwasafishe Aruni na wana wake kwenye maji.
5 And thou shalt take the garments, and clothe Aaron with the coat, and the robe of the ephod, and the ephod, and the breastplate, and gird him with the girdle of the ephod:
Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
6 And thou shalt put the mitre upon his head, and thou shalt fasten the holy crown upon the mitre.
Nawe mvike kile kilemba kichwani, na ile taji takatifu utaitia katika kile kilemba.
7 Then shalt thou take the anointing oil, and pour it upon his head, and anoint him.
Ndipo utakapotwaa hayo mafuta ya kutiwa, na kummiminia kichwani mwake, na kumtia mafuta.
8 And his sons shalt thou bring near, and clothe them with coats.
Kisha walete hao wanawe na kuwavika kanzu.
9 And thou shalt gird them with the girdles, Aaron and his sons, and bind the bonnets on them; and the priest's office shall be theirs for a perpetual statute: and thus shalt thou consecrate Aaron and his sons.
Nawe uwakaze mishipi, Aruni na wanawe, na kuwavika kofia. Nao watakuwa na huo ukuhani kwa amri ya milele. Nawe utawaweka Haruni na wanawe kwa kazi takatifu.
10 And thou shalt cause the bullock to be brought before the tabernacle of the congregation: and Aaron and his sons shall lay their hands upon the head of the bullock.
Kisha utamleta huyo ng’ombe mbele ya hema ya kukutania; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe.
11 And thou shalt kill the bullock before the Lord, by the door of the tabernacle of the congregation.
Kisha utamchinja huyo ng’ombe mbele ya Yahweh pa hema ya kukutania. BWANA,
12 And thou shalt take of the blood of the bullock, and put it upon the horns of the altar with thy finger, and all the remaining blood shalt thou pour out beside the bottom of the altar.
Kisha twaa baadhi ya damu ya ng’ombe, uitie katika pembe za madhabahu kwa kidole chako; na kuimimina damu yote chini ya madhabahu.
13 And thou shalt take all the fat that covereth the inwards, and the midriff above the liver, and the two kidneys, and the fat that is upon them, and burn them upon the altar.
Kisha chukuwa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.
14 But the flesh of the bullock, and his skin, and his dung, shalt thou burn with fire, without the camp: it is a sin-offering.
Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.
15 And the one ram shalt thou take; and Aaron and his sons shall lay their hands upon the head of the ram.
Pia mtwae kondoo mume mmoja; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo mume.
16 And thou shalt slay the ram, and thou shalt take his blood, and sprinkle it upon the altar round about.
Kisha utamchinja huyo kondoo mume, na kuitwaa damu yake, na kuinyunyiza katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
17 And the ram shalt thou cut in pieces, and wash his inwards, and his legs, and put them with his pieces, and with his head.
Kisha utamkata-kata kondoo vipande vyake, na kuyaosha matumbo yake na miguu yake, na kuiweka pamoja na vipande vyake na kichwa chake,
18 And thou shalt burn the whole ram upon the altar, it is a burnt-offering unto the Lord; it is a sweet savor, an offering made by fire unto the Lord.
nawe mteketeze kondoo mzima juu ya madhabahu. Ni sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yaYahweh; ni harufu nzuri, sadaka iliyosongezwa kwa Yahweh kwa njia ya moto.
19 And thou shalt take the other ram; and Aaron and his sons shall lay their hands upon the head of the ram.
Kisha mtwae huyo kondoo mwingine; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo.
20 Then shalt thou kill the ram, and take of his blood, and put it upon the tip of Aaron's right ear, and upon the tip of the right ear of his sons, and upon the thumb of their right hand, and upon the great toe of their right foot, and sprinkle the blood upon the altar round about.
Kisha utamchinja kondoo, na kuitwaa damu yake, na kuitia katika ncha ya sikio la Aruni la upande wa kuume, na katika ncha za masikio ya kuume ya wanawe, na katika vyanda vya gumba vya mikono yao ya kuume, na katika vidole vikuu vya miguu yao ya kuume, na kuinyunyiza hiyo damu katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
21 And thou shalt take of the blood that is upon the altar, and of the anointing oil, and sprinkle them upon Aaron, and upon his garments, and upon his sons, and upon the garments of his sons with him: and he shall be hallowed, together with his garments, and his sons, and the garments of his sons with him.
Kisha twaa katika hiyo damu iliyo juu ya madhabahu, na katika hayo mafuta ya kutiwa, na kumnyunyizia Aruni, juu ya mavazi yake, na wanawe, na mavazi yao pia, pamoja naye; naye atatakaswa, na mavazi yake, na wanawe, na mavazi ya wanawe, pamoja naye.
22 And thou shalt take from the ram the fat and the rump, and the fat that covereth the inwards, and the midriff above the liver, and the two kidneys, and the fat that is upon them, and the right shoulder; for it is a ram of consecration;
Tena yatwae mafuta ya huyo kondoo mume, na mkia wake wa mafuta, na mafuta yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo katika hizo figo, na paja la kuume; kwani ni kondoo ambaye ni wa kuwekwa kwa kazi takatifu.
23 And one loaf of bread, and one cake of the oiled bread, and one wafer, out of the basket of the unleavened bread that is before the Lord.
Utwae na mkate mmoja wa unga, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na kaki moja katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, kilichowekwa mbele ya Yahweh.
24 And thou shalt put all this upon the hands of Aaron, and upon the hands of his sons; and thou shalt make with them a waving before the Lord.
Nawe utavitia hivi vyote katika mikono ya Aruni, na katika mikono ya wanawe; nawe utavitikisa-tikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
25 And thou shalt then take them from their hands, and burn them upon the altar upon the burnt-offering; for a sweet savor before the Lord, it is an offering made by fire unto the Lord.
Kisha uvitwae vile vitu mikononi mwao, na kuviteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri mbele yangu; ni sadaka iliyotengenezwa kwangu kwa njia ya moto.
26 And thou shalt take the breast of the ram of the consecration that belongeth to Aaron, and make therewith a waving before the Lord; and it shall belong to thee as thy portion.
Kisha twaa kidari cha huyo kondoo wa kuwekwa kwake Haruni kwa kazi takatifu, na kukitikisa-tikisa kiwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahwe nacho kitakuwa ni sehemu yako.
27 And thou shalt sanctify the breast which hath been waved, and the shoulder which hath been lifted up, which was waved, and which was heaved up, of the ram of the consecration, of that which belongeth to Aaron, and of that which belongeth to his sons:
Nawe kitakase kile kidari cha ile sadaka ya kutikiswa, na lile paja la sadaka ya kuinuliwa, lililotikiswa, na lililoinuliwa juu, vya yule kondoo wa kuwekwa kwa kazi takatifu, huyo aliyekuwa kwa ajili ya Aruni na wanawe.
28 That they shall belong to Aaron and to his sons, as a statute forever, from the children of Israel; for it is a heave-offering; and a heave-offering it shall remain from the children of Israel, from the sacrifices of their peace-offerings, as their heave-offering unto the Lord.
Navyo vitakuwa vya Haruni na wanawe posho ya lazima sikuzote itokayo kwa hao wana wa Israeli; kwa kuwa ni sadaka ya kuinuliwa; nayo itakuwa ni sadaka ya kuinuliwa itokayo kwa hao wana wa Israeli katika dhabihu zao za sadaka za amani, ni sadaka yao ya kuinuliwa kwa ajili ya Yahweh.
29 And the holy garments belonging to Aaron shall be for his sons after him, to anoint them therein, and to consecrate them therein.
Na hayo mavazi matakatifu ya Aruni yatakuwa ya wanawe baada yake, wayavae watakapotiwa mafuta, na watakapowekwa kwa kazi takatifu.
30 Seven days shall that one of his sons put them on who is to be priest in his place, who is to go into the tabernacle of the congregation to minister in the sanctuary.
Huyo mwanawe atakayekuwa kuhani badala yake atayavaa muda wa siku saba, hapo atakapoingia ndani ya hiyo hema ya kukutania, ili atumike ndani ya mahali patakatifu.
31 And the ram of the consecration shalt thou take, and seethe his flesh in a holy place.
Nawe twaa huyo kondoo mume aliyekuwa wa kuwekwa kwa kazi takatifu, na kuitokosa nyama yake katika mahali patakatifu.
32 And Aaron with his sons shall eat the flesh of the ram, and the bread that is in the basket, by the door of the tabernacle of the congregation.
Na Aruni na wanawe wataila ile nyama ya kondoo, na mikate iliyo katika kile kikapu, hapo mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
33 And they shall eat those things wherewith the atonement was made, to consecrate them and to sanctify them; but a stranger shall not eat thereof, because they are holy.
Nao watakula vile vitu ambavyo upatanisho ulifanywa kwa hivyo, ili kuwaweka kwa kazi takatifu na kuwatakasa; lakini mgeni asivile, maana, ni vitu vitakatifu.
34 And if aught of the flesh of the consecration sacrifice, or of the bread, remain unto the morning, then shalt thou burn the remainder with fire; it shall not be eaten, because it is holy.
Na kwamba kitu cho chote cha ile nyama, iliyo kwa ajili ya kuweka kwa kazi takatifu, au cho chote cha hiyo mikate, kikisalia hata asubuhi, ndipo utavichoma kwa moto hivyo vilivyosalia; havitaliwa, maana, ni vitu vitakatifu
35 And thou shalt do unto Aaron, and to his sons thus, all as I have commanded thee; seven days shalt thou consecrate them.
Ni hivyo utakavyowatendea Aruni na wanawe kama nilivyo kuagiza. Utawaweka kwa kazi takatifu siku saba.
36 And a bullock shalt thou offer every day for a sin-offering as an atonement: and thou shalt cleanse the altar, in as much as thou makest an atonement upon it; and thou shalt anoint it, to sanctify it.
Kila siku utamtoa ng’ombe wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho; nawe utaisafisha hiyo madhabahu, hapo utakapofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu; nawe utaitia mafuta, ili kuitakasa.
37 Seven days shalt thou make an atonement upon the altar and sanctify it; and the altar shall be most holy; whatsoever toucheth the altar shall be holy.
Utafanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu muda wa siku saba, na kuitakasa; ndipo madhabahu itakapokuwa takatifu sana; kila kitu kiigusacho madhabahu kitakuwa kitakatifu.
38 And this is what thou shalt offer upon the altar: Two sheep of the first year for every day, continually.
Lazima utoe kwenye madhabahu wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku
39 The one sheep shalt thou offer in the morning; and the other sheep shalt thou offer toward evening.
daima. Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni
40 And a tenth part of fine flour mingled with the fourth part of a hin of beaten oil, and the fourth part of a hin of wine for a drink-offering, shall be for the one sheep.
Pamoja na mwana-kondoo mmoja utatoa vibaba vitatu vya unga mzuri uliochanganyika na mafuta yenye kupondwa, kiasi cha kibaba na robo kibaba; na divai kiasi cha kibaba na robo kibaba, iwe sadaka ya kinywaji.
41 And the other sheep shalt thou offer toward evening; according to the meat-offering of the morning, and according to its drink-offering shalt thou do unto it, for a sweet savor, an offering made by fire unto the Lord.
Na huyo mwana-kondoo wa pili utamchinja wakati wa jioni. Nawe utamfanyia vivyo kama ile sadaka ya unga ya asubuhi, na kama ile sadaka yake ya kinywaji. Hii itatoa harufu nzuri, ni dhabihu ya kusongezwa kwangu kwa njia ya moto.
42 A continual burnt-offering throughout your generations [shall this be] at the door of the tabernacle of the congregation before the Lord; where I will meet with you, to speak unto thee there.
Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa milele katika vizazi vyenu vyote mlangoni pa ile hema ya kukutania mbele ya Yahweh, hapo nitakapokutana nanyi, ili niseme na wewe hapo.
43 And I will meet there with the children of Israel, and it shall be sanctified by my glory.
Nami nitakutana na wana wa Israeli hapo; na hiyo hema itafanywa takatifu na utukufu wangu. Nami nitaitakasa hiyo hema ya kukutania, na hiyo madhabahu.
44 And I will sanctify the tabernacle of the congregation, and the altar: and both Aaron and his sons will I sanctify, that they may he priests unto me.
Pia Aruni na wanawe nitawatakasa, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
45 And I will dwell among the children of Israel, and I will be to them for a God.
Na mimi nitakaa kati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao.
46 And they shall know that I am the Eternal, their God, who brought them forth out of the land of Egypt, that I might dwell among them: I am the Lord their God.
Nao watanijua kuwa mimi ndimi Yahweh, Mungu wao, niliyewaleta watoke katika nchi ya Misri, nipate kukaa kati yao. Ni mimi Yahweh, Mungu wao.

< Exodus 29 >