< Exodus 23 >

1 Thou shalt not receive a false report: put not thy hand with the wicked to be an unrighteous witness.
Haupaswi kutoa taarifa ya uongo kuhusu yeyote. usijiunge na mwanaume muovu kuwa shahidi wa uongo.
2 Thou shalt not follow a multitude to do evil; neither shalt thou speak in a cause, to incline after many, to wrest judgment.
Haupaswi kufuata umati kufanya uovu, wala kutoa ushahidi ukiwa na umati ili kupotosha haki.
3 Neither shalt thou countenance a poor man in his cause.
Haupaswi kumpendelea mwanaume maskini kwenye kesi yake.
4 If thou meet thy enemy's ox or his ass going astray, thou shalt surely bring it back to him again.
Ukikutana na ng'ombe wa adui wako au punda wake amepotea, lazima umrudishie.
5 If thou see the ass of him that hateth thee lying under his burden, and wouldest forbear to unload him, [thou must not do so, but] thou shalt surely unload with him.
Ukiona punda wa yule anaye kuchukia ameanguka chini na mzigo wake, hauta muacha huyo mtu. Lazima umsaidie na punda wake
6 Thou shalt not wrest the judgment of thy poor in his cause.
Haupaswi kupotosha haki kama yapaswa kwenda kwa watu maskini katika kesi ya mwanaume maskini.
7 Keep thyself far from a false speech; and him who hath been declared innocent and righteous thou shalt not slay; for I will not justify the wicked.
Usijiunge na wengine kufanya shutuma za uongo, na usiue asiye na hatia wala mwenye haki, kwa kuwa sitamuacha muovu.
8 And thou shalt take no bribe; for the bribe blindeth the clear-sighted, and perverteth the words of the righteous.
Husiwai chukuwa rushwa, kwa kuwa rushwa inawapofusha wanaoona, na kupotosha maneno ya wakweli.
9 And a stranger shalt thou not oppress; for ye know well the spirit of the stranger, seeing ye yourselves were strangers in the land of Egypt.
Haupaswi kumnyanyasa mgeni, kwa kuwa wewe ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri.
10 And six years shalt thou sow thy land, and shalt gather in the fruits thereof;
Kwa miaka sita utapanda mbegu kwenye nchi yako na kukusanya mazao yake.
11 But the seventh year shalt thou let it rest and lie still; that the needy of thy people may eat [of it]; and what they leave the beasts of the field shall eat: in like manner shalt thou deal with thy vineyard, and with thy olive tree.
Lakini katika mwezi wa saba utaacha hakujalimwa, ili kwamba maskini miongoni mwenu wale. Wanacho acha, wanyama wa porini watakula. Utafanya hivyo na mashamba yenu ya mizabibu na ya mizaituni.
12 Six days shalt thou do thy work, and on the seventh day shalt thou rest; that thy ox and thy ass may repose, and the son of thy hand-maid, and the stranger, may be refreshed.
Wakati wa siku sita utafanya kazi, lakini siku ta saba utapumzika. Fanya hivi ili ng'ombe na punda wako wapumzike, na ili wana wa watumwa wako wa kike na wageni wapumzike na kupata hauweni.
13 And in all things that I have said unto you be on your guard; and of the name of other gods ye shall make no mention, it shall not be heard out of thy mouth.
Kuwa makini kwa kila kitu nilicho kwambia. Husitaje majina ya miungu mingine, wala kuruhusu majina yao kusikika kutoka mdomoni mwako.
14 Three times shalt thou keep a feast unto me in the year.
Lazima usafiri kusherehekea mara tatu kwa ajili yangu kila mwaka.
15 The feast of unleavened bread shalt thou keep; seven days shalt thou eat unleavened bread, as I commanded thee, in the time appointed of the month of Abib; for in it thou camest out from Egypt: and none shall appear before me empty.
Lazima uadhimishe sherehe ya Mkate usiotiwa Chachu. Kama nilivyo kuamuru, utakula mkate usiotiwa chachu kwa siku saba. Wakati huo, utajitokeza kwangu mwezi wa Abibu, uliowekwa kwa ajili ya kusudi hili. Ni kwa mwezi huu uliyo toka Misri. Lakini usijitokeze kwangu mikono mitupu.
16 And the feast of harvest, of the first-fruits of thy labors, which thou hast sown in thy field: and the feast of ingathering, at the conclusion of the year, when thou gatherest in thy labors out of the field.
Lazima uadhimishe Sherehe ya Mavuno, matunda ya kwanza ya kazi yako ulipo panda mbegu shambani. Pia lazima uadhimishe Sherehe ya Ukusanyaji wa mwisho wa mwaka, unapo kusanya mazao yako kutoka shambani.
17 Three times in the year shall all thy males appear before the Lord, the Eternal.
Wanaume wote wako lazima wajitokeze kwa Bwana Yahweh mara tatu kila mwaka.
18 Thou shalt not offer the blood of my sacrifice with leavened bread; neither shall the fat of my festive sacrifice remain until morning.
Haupaswi kutoa damu iliyo tolewa dhabihu kwangu na mkate uliyotiwa hamira. Mafuta kutoka kwa dhabihu za sherehe zangu hayapaswi kubaki usiku wote mpaka asubui.
19 The first of the first-fruits of thy land shalt thou bring unto the house of the Lord thy God. Thou shalt not seethe a kid in its mother's milk.
Lazima ulete matunda ya kwanza bora kutoka shambani mwako ndani ya nyumba yangu, nyumba ya Yahweh Mungu wako. Haupaswi kumchemsha mbuzi mtoto akiwa bado ananyonya.
20 Behold, I send an angel before thee, to keep thee on the way, and to bring thee unto the place which I have prepared.
Ninaenda kumleta malaika mbele yako kukuongoza njiani, na kukuleta sehemu niliyo iandaa.
21 Beware of him, and obey his voice, disobey him not; for he will not pardon your transgression, because my name is in him.
Kuwa makini naye na kumtii.
22 But if thou wilt carefully hearken to his voice, and do all that I shall speak: then will I be an enemy unto thy enemies, and afflict those that afflict thee.
Husimkasirishe, kwa kuwa hatasamehe makosa yako. Jina langu liko kwake. Kama hakika ukimtii sauti yake na kufanya kila ninacho kwambia, kisha nitakuwa adui kwa adui zako na mpinzani kwa wapinzani wako.
23 For my angel shall go before thee, and bring thee in unto the Emorites, and the Hittites, and the Perizzites, and the Canaanites, the Hivites, and the Jebusites; and I will cut them off.
Malaika mwangu ataenda mbele zako na kukuleta kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanani, Wahivi, na Wayebusi. Nitawaharibu.
24 Thou shalt not bow down to their gods, nor serve them, nor do after their deeds; but thou shalt utterly overthrow them, and completely break down their statuary images.
Haupaswi kuinamia miungu yao, kuabudu, au kufanya wanavyo fanya. Badala yake, lazima uwapindue kabisa na kuvunja nguzo zao za mawe vipande vipande.
25 And ye shall serve the Lord your God, and he will bless thy bread, and thy water; and I will remove sickness from the midst of thee.
Lazima umuabudu Yahweh Mungu wako, na atabariki mkate wako na maji. Nitaondoa magonjwa miongoni mwenu.
26 There shall be no one casting her children, nor a barren woman, in thy land; the number of thy days I will make full.
Hakuna mwanamke atakaye kuwa tasa au mimba kuharibika katika nchi yako. Nitawapa maisha marefu.
27 My terror will I send before thee, and will bring in confusion all the people to which thou shalt come; and I will make all thy enemies turn their back unto thee.
Nitatuma hofu yangu kwao ambao mnaenda. Nitaua wote mnao kutana nao. Nitafanya maadui zenu wawaogope kwa kugeuza migongo yao kwenu.
28 And I will send hornets before thee, and they shall drive out the Hivite, the Canaanite, and the Hittite, from before thee.
Nitatuma mavu kwenu watakao fukuza Wahivi, Wakanani, na Wahiti mbele zenu.
29 I will not drive them out from before thee in one year; lest the land become desolate, and the beast of the field multiply against thee.
Sitawaondoa kwenu kwa mwaka mmoja, au nchi itakuwa imetelekezwa, na wanyama wa porini watakuwa wengi kwenu.
30 Little by little will I drive them out from before thee, until thou be increased and canst possess the land.
Badala yake, nitawafukuza kidogo kidogo kutoka kwenu mpaka utakapo kuwa umestawi na kurithi nchi.
31 And I will set thy bounds from the Red Sea unto the sea of the Philistines, and from the desert unto the river; for I will deliver into your hand the inhabitants of the land, and thou shalt drive them out before thee.
Nitatengeneza mipaka yako kutoka Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kutoka nyikani hadi Mto Frati. Nitakupa ushindi juu ya wakazi wote wa nchi. Utawaondoa kutoka kwako mwenyewe.
32 Thou shalt not make a covenant with them, nor with their gods.
Haupaswi kufanya agano na wao au na miungu yao.
33 They shall not dwell in thy land, lest they cause thee to sin against me; for thou mightest [be led to] serve their gods, and this would surely be a snare unto thee.
Hawapaswi kuishi nchini mwako, au watakufanya ufanya dhambi dhidi yangu. Ukiabudu miungu yao, hakika watakuwa mtego kwako.'”

< Exodus 23 >