< Esther 1 >

1 And it came to pass in the days of Achashverosh, of the same Achashverosh who reigned, from India even unto Ethiopia, over a hundred and seven and twenty provinces,
Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
2 In those days, when this king Achashverosh was sitting on the throne of his kingdom, which was in Shushan the capital,
Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
3 That, in the third year of his reign, he made a feast unto all his princes and his servants, the army of Persia and Media, the nobles and the princes of the provinces who were near him:
Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
4 When he showed the riches and the glory of his kingdom, and the brilliance [and] the splendor of his greatness, during many days, a hundred and eighty days.
Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
5 And when these days were completed, the king made unto all the people that were found in Shushan the capital, unto every one, from the great even to the small, a feast of seven days, in the court of the garden of the king's palace;
Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
6 [Where were] white, green, and blue [hangings], fastened with cords of fine linen and purple, on rollers of silver and pillars of marble; couches of gold and silver, upon a pavement of green, and white, and yellow, and black marble.
Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
7 And they gave them to drink in vessels of gold, —the vessels being diverse one from the other, —and the royal wine was in abundance, according to the ability of the king.
Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
8 And the drinking was, according to the [king's] order, without compulsion; for so had the king enjoined on all the officers of his house, to do according to the pleasure of every man.
Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
9 Also Vashti the queen made a feast for the women, in the royal house which belonged to king Achashverosh.
Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
10 On the seventh day, when the heart of the king was merry with wine, he commanded Mehuman, Biztha, Charbona, Bigtha, and Abagtha, Zethar, and Carcass, the seven chamberlains that served in the presence of king Achashverosh,
Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
11 To bring Vashti the queen before the king [ornamented] with the royal crown, to show the people and the princes her beauty; for she was handsome in appearance.
kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
12 But queen Vashti refused to come at the word of the king brought by the hand of the chamberlains; and the king was very wroth, and his fury burnt in him.
Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
13 Then said the king to the wise men, who knew [the occurrences of] the times; for so [came] every affair of the king before all acquainted with law and state institutions;
Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
14 And those next unto him were Carshena, Shethar, Admatha, Tharshish, Meress, Marsena, and Memuchan, the seven princes of Persia and Media, who could see [at all times] the king's face, who sat in the first rank in the kingdom:
nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
15 What should according to law be done with queen Vashti; because she had not fulfilled the order of king Achashverosh by the hand of the chamberlains?
Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
16 Then said Memuchan before the king and the princes, Not against the king alone hath Vashti the queen done wrong, but also against all the princes, and against all the people that are in all the provinces of king Achashverosh.
Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
17 For the conduct of the queen will go abroad unto all the women, so that they will despise their husbands in their eyes, when it shall be reported, King Achashverosh ordered Vashti the queen to be brought into his presence, but she came not.
Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
18 And even this day will the ladies of Persia and Media, who have heard of the conduct of the queen, say this unto all the princes of the king; and there will arise too much contempt and quarrel.
Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
19 If it please the king, let there go forth a royal order from him, and let it be written among the laws of the Persians and the Medes, that no one transgress it, That Vashti come no more before king Achashverosh: and let the king give her royal dignity unto another that is better than she.
“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
20 And when the king's decree which he will make shall be published throughout all his kingdom, however great it is: all the wives will show respect to their husbands, unto every one, from the great even to the small.
Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
21 And the speech was pleasing in the eyes of the king and of the princes; and the king did according to the speech of Memuchan.
Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
22 And he sent letters unto all the provinces of the king, unto every province according to its writing, and to every people according to its language, that every man should bear rule in his own house, however he may speak according to the language of his people.
Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.

< Esther 1 >