< Ecclesiastes 3 >

1 For every thing there is a season; and a [proper] time is for every pursuit under the heavens.
Kwa kuwa kila kitu na wakati wake, na majira kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 [There is] a time to be born, and a time to die; a time to plant, and a time to pluck up what hath been planted;
Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kung'oa yaliyopandwa,
3 A time to kill, and a time to heal; a time to break down, and a time to build up;
wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomo na wakati wa kujenga.
4 A time to weep, and a time to laugh; a time to mourn, and a time to dance;
Kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati kucheza,
5 A time to throw away stones, and a time to gather up stones; a time to embrace, and a time to be far from embracing;
wakati wa kutupa mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia watu wengine wakati wa kutokumbatia.
6 A time to seek, and a time to let things be lost; a time to keep, and a time to throw away;
Kuna wakati wa kutafuta vitu na wakati wa kutotafuta, wakati wa kutunza vitu na wakati wa kuvitupa,
7 A time to rend, and a time to sew; a time to keep silence, and a time to speak;
wakati kuchana mavazi na wakati wa kuyashona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza.
8 A time to love, and a time to hate; a time of war, and a time of peace.
Kuna wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
9 What profit hath [now] he that worketh in that wherein he toileth?
Ni faida gani mfanyakazi aipatayo katika kazi yake?
10 I have seen the employment, which God hath given to the sons of men to busy themselves therewith.
Nimeona kazi ambayo Mungu amewapa wanadamu kuitimiza.
11 Every thing hath he made beautiful in its [proper] time: he hath also placed the eternity in their heart, without a man's being able to find out the work that God hath made from the beginning to the end.
Mungu amefanya kila kitu kufaa kwa wakati wake. Pia ameweka umilele ndani ya mioyo yao. Lakini mwanadamu hawezi kuelewa matendo ambayo Mungu ameyafanya, tangu mwanzo wao hadi mwisho.
12 I know that there is nothing good [inherent] in them, but for every one to rejoice and to do what is good during [all] his life.
Ninajua kuwa hakuna kilicho bora kwa mtu yeyote kuliko kufurahi na kutenda mema maadamu anaishi-
13 For also that every man should eat and drink, and enjoy what is good for all his toil, is likewise a gift of God.
na kwamba kila mmoja anapaswa ale na kunywa na anapaswa kuelewa jinsi ya kufurahia mazuri ambayo yanatoka katika kazi zake zote. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu.
14 I know that whatsoever God doth, that will be for ever; to it nothing can be added, and from it there is nothing to be diminished: and God hath so made it, that men should be afraid of him.
Ninajua kwamba chochote afanyacho Mungu kinadumu milele. Hakuna kinaweza kuongezwa au kuondolea, kwa sababu Mungu ndiye aliyekifanya, ili kwamba watu wamsogelee kwa heshima.
15 That which hath been hath long since appeared [again]; and what is to be hath already been; and God seeketh [again] that which is sped away.
Chochote kilichopo kimekwisha kuwepo; chochote kitakachokuwepo kimekwisha kuwepo. Mungu huwafanya wanadamu kutafuka vitu vilivyjificha.
16 And moreover I have seen under the sun, [that in] the place of justice, even there was wickedness; and [that in] the place of righteousness, even there was wickedness.
Na nimeona kwamba chini ya jua ubaya upo mahali palipopaswa kuwa na haki, na sehemu ya haki mara nyingi ina ubaya.
17 I said in my heart, God will judge the righteous and the wicked; for there is a time for every pursuit; and on account of every deed there [will he judge].
Nikasema moyoni mwangu, “Mungu atahukumu mwenye haki na mbaya kwa wakati muafaka kwa kila jambo na kila tendo.
18 I said in my heart concerning the speaking of the sons of men, that God might make it clear to them, and that they might see that they by themselves are but beasts.
Nikasema moyoni mwangu, “Mungu huwajaribu wanadamu kuwaonyesha kwamba wao ni kama wanyama.”
19 For that which befalleth the sons of men befalleth beasts; even the same thing befalleth them; as the one dieth, so dieth the other; yea, they have all one kind of spirit: so that the preeminence of man above the beast is nought; for all is vanity.
Kwa kuwa mwisho watoto wa wanadamu na mwisho wa wanyama ni sawa. Kifo cha mmoja ni sawa na kifo cha mwingine. Wote wana pumzi sawa. Hakuna faida kwa mwanadamu zaidi ya wanyama. Kwa kuwa hakuna kila kitu isipokuwa pumzi?
20 Every thing goeth unto one place: every thing came from the dust, and every thing returneth to the dust.
Kila kitu kinaenda sehemu moja. Kila kitu kinatoka mavumbini, na kila kitu kinarudi katika mavumbini.
21 Who knoweth the spirit of the sons of man that ascendeth upward, and the spirit of the beast that descendeth downward to the earth?
Ni nani ajuaye kama roho ya mwanadamu inaenda juu na roho ya wanyama inaenda chini ya nchi?
22 And so did I perceive that there is nothing better, than that a man should rejoice in his own works; for that is his portion; for who can bring him to look with pleasure on what will be after him?
kwa hiyo tena nikatambua kwamba hakuna lililo jema kwa yeyote zaidi ya kufurahia kazi yake, kwa kuwa hilo ndilo jukumu lake. Ni nani awezaye kumleta tena kuona kinachotokea baada yake?

< Ecclesiastes 3 >