< Deuteronomy 7 >
1 When the Lord thy God shall bring thee into the land whither thou goest to possess it, and cast out many nations before thee, the Hittites, and the Girgashites, and the Emorites, and the Canaanites, and the Perizzites, and the Hivites, and the Jebusites, seven nations, greater in number and mightier than thou;
Wakati Yahwe Mungu wenu atuleta katika nchi ambayo mnaenda kuimiliki na kuwaondoa mataifa mengi mbele zenu- Mhiti, Mgirgashi na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, Mhivi, Myebusi- mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko wewe.
2 And when the Lord thy God shall give them up before thee, and thou dost smite them: thou shalt utterly destroy them; thou shalt not make any covenant with them, nor show mercy unto them.
Na wakati Yahwe Mungu wenu awapa ninyi ushindi juu yao pindi mnakutana nao katika vita, mtawashambulia, basi mnapaswa kuwateketeza kabisa. Hamtafanya agano nao, wala kuonesha huruma kwao.
3 Neither shalt thou make marriages with them; thy daughters shalt thou not give unto his son, and his daughter shalt thou not take unto thy son.
Wala hamtapanga ndoa zozote pamoja nao, hamtawatoa binti zenu kwa vijana wao, na hamtawachukua binti zao kwa vijana wenu.
4 For he would turn away thy son from following me, so that they might serve other gods; and the anger of the Lord would be kindled against you, and he would destroy thee speedily.
Kwa kuwa watawabadilisha vijana wenu kutonifuata mimi, ili kwamba waweze kuabudu miungu yao. Kwa hiyo hasira ya Yahwe itawashwa dhidi yenu na atawaangamiza haraka.
5 But thus shall ye do unto them: their altars shall ye pull down, and their statues shall ye break, and their groves shall ye cut down, and their graven images shall ye burn with fire.
Hivi ndivyo mtakavyo washughulikia nao; mtavunja madhabahu zao, vunja nguzo zao za mawe katika vipande, kata chini ncha za Asherahi, na kuzichoma sanamu za kutupwa.
6 For thou art a holy people unto the Lord thy God; of thee the Lord thy God hath made choice to be unto himself a special people, above all the nations that are upon the face of the earth.
Kwa kuwa wewe ni taifa uliyetengwa kwa Yahwe Mungu wako. Amekuchagua wewe kuwa watu kwa ajili yake kumiliki, zaidi ya watu wengine wote ambao wako katika uso wa dunia.
7 Not because ye are more in number than all the nations, did the Lord desire you and make choice of you; for ye are the fewest of all the nations;
Yahwe hakuweka upendo wake juu yenu au kuwachagua kwa sababu mlikuwa zaidi katika idadi kuliko watu wowote, kwa kuwa mlikuwa wachache kuliko watu wote-
8 But on account of the love of the Lord for you, and because he keepeth the oath which he hath sworn unto your fathers, hath the Lord brought you out with a mighty hand, and redeemed you out of the house of bond-men, out of the hand of Pharaoh the king of Egypt.
Lakini kwa sababu anawapenda ninyi, anataka kushika kiapo alichoapa kwa baba zenu. Huyu ni Yahwe aliyewatoa kwa mkono wa uweza na kuwakomboa kutoka nyumba ya utumwa, kutoka mkono wa Farao, mfalme wa Misri.
9 Know then that the Eternal thy God, is the God, the faithful God, who keepeth the covenant and the mercy with those that love him and with those that keep his commandments to the thousandth generation;
Kwa hiyo tambua ya kuwa Yahwe Mungu wako-ni Mungu, Mungu mwaminifu, anayetunza maagano na uaminifu kwa vizazi elfu kwa wale wanaompenda na kuyashika maagizo yake,
10 And repayeth those that hate him to their face, to destroy them; he will not delay to him that hateth him, he will repay him to his face.
lakini huwalipa wale wanaomchukia kwa sura zao, kuwaangamiza, hatakuwa na huruma kwa yeyote anayemchukia; atamlipa kwa uso wake.
11 Therefore shalt thou keep the commandment, and the statutes, and the ordinances, which I command thee this day, to do them.
Kwa hiyo utashika maagizo, amri, na sheria ninazokuamuru leo, ili kwamba uzifanye.
12 And it shall come to pass in reward for that ye will hearken to these ordinances, and keep, and do them, that the Lord thy God will keep unto thee the covenant and the kindness which he hath sworn unto thy fathers:
Kama mtasikiliza maagizo haya, kuyashika na kuyafanya, itakuwa Yahwe Mungu wenu atawashika pamoja na agano na uaminifu ambao aliapa kwa baba zenu.
13 And he will love thee, and bless thee, and multiply thee; and he will bless the fruit of thy womb, and the fruit of thy land, thy corn, and thy wine, and thy oil, the increase of thy cattle, and the young of thy flocks, in the land which he hath sworn unto thy fathers to give unto thee.
Atawapenda, atawabariki, na kuwazidisha, pia atabariki tunda la miili yenu na tunda la ardhi yenu, nafaka zenu, divai mpya, mafuta yenu, atazidisha mifugo na kundi lako la mifugo michanga, katika nchi ambayo aliapa kwa baba zenu kuwapa.
14 Blessed shalt thou be above all the nations; there shall not be a barren male or female among thee, nor among thy cattle.
Mtabarikiwa zaidi kuliko watu wengine wote; hapatakuwa na mwanaume asiyekuwa na mtoto au mwanamke tasa miongoni mwenu au miongoni mwa mifugo.
15 And the Lord will take away from thee all sickness; and all the evil diseases of Egypt, which thou knowest, will he not put upon thee; but he will lay them upon all those that hate thee.
Yahwe atawaondolea magonjwa yote; hakuna magonjwa mabaya ya Misri ambayo mnayajua yatawekwa juu yenu, Lakini atayaweka kwa wote wanaowachukia ninyi.
16 And thou shalt consume all the nations which the Lord thy God giveth unto thee; thy eye shall not look with pity upon them: and thou shalt not serve their gods; for that would be a snare unto thee.
Mtayaondoa makundi ya watu wote ambayo Yahwe Mungu wenu awapa ushindi, na jicho lenu halitawaonea huruma. Na hamtaabudu miungu yao, kwa kuwa huo utakuwa mtego kwenu.
17 If thou shouldst say in thy heart, These nations are more numerous than I: how shall I be able to dispossess them?
Kama mtasema kwenye mioyo, Haya mataifa ni mengi zaidi kuliko mimi; nitawezaje kuwafukuza?
18 Thou shalt not be afraid of them; [but] thou shalt well remember what the Lord thy God did unto Pharaoh, and unto all Egypt;
Usiwaogope; utakumbuka akilini Yahwe nini Mungu wenu alifanya kwa Farao na Misri yote?
19 The great proofs which thy eyes have seen, and the signs, and the wonders, and the mighty hand, and the outstretched arm, whereby the Lord thy God brought thee out: in this wise will the Lord thy God do unto all the people of whom thou art afraid.
Mateso makuu ambayo macho yenu yaliona, ishara, maajabu, mkono wa uweza, mkono ulionyoshwa ambao Yahwe Mungu wenu alivyowatoa. Yahwe Mungu wenu atafanya kile kile kwa watu wote ambao mnawaogopa.
20 Moreover the hornet will the Lord thy God send out against them, until they that are left, and hide themselves from thee, be destroyed.
Zaidi ya yote, Yahwe Mungu wenu atatuma nyigu miongoni mwao, mpaka wale waliobaki na wale wanaojificha wenyewe mbele yenu waangamizwa mbele ya uwepo wenu.
21 Thou shalt not be affrighted at them; for the Lord thy God is in the midst of thee, a mighty and terrible God.
Hamtatishikeni nao, kwa kuwa Yahwe Mungu wenu yuko miongoni mwenu, Mungu mkuu na wa kuogofya.
22 And the Lord thy God will chase out these nations before thee, little by little: thou shalt not be able to make an end of them speedily, lest the beasts of the field increase upon thee.
Yahwe Mungu wenu atayaondoa mataifa mbele zenu kidogo kidogo. Hamtayashinda yote kwa wakati mmoja, au wanyama wa mwitu watakuwa wengi karibu yenu.
23 And the Lord thy God will give them up before thee, and he will bring among them a mighty confusion, until they be destroyed.
Lakini Yahwe Mungu wenu atawapa ninyi ushindi dhidi yao wakati mkutanapo vitani; atawachanganya kwa kiasi kikubwa mpaka wameangamizwa.
24 And he will give their kings into thy hand, and thou shalt destroy their name from under the heavens: no man shall be able to stand up before thee, until thou have destroyed them.
Atawaweka wafalme wao chini ya utawala wenu, na mtafanya jina lao kuangamia toka chini ya mbingu. Hakuna atakayeweza kusimama mbele yenu, mpaka muwaangamize.
25 The graven images of their gods shall ye burn with fire: thou shalt not covet the silver or gold that is on them, so that thou wouldst take it unto thyself, lest thou be ensnared thereby; for it is an abomination to the Lord thy God.
Utazichoma sanamu za kuchonga za miungu yao- usitamani madini ya fedha au dhahabu yanayofunika na kuichukua kwa ajili yenu, kwa sababu mkifanya, mtanaswa nayo-kwa kuwa ni chukizo kwa Yahwe Mungu wenu.
26 And thou shalt not bring an abomination into thy house, lest thou become accursed like it: thou shalt utterly detest it, and thou shalt utterly abhor it; for it is accursed.
Hamtaleta chukizo lolote ndani ya nyumba zenu na kuanza kuiabudu. Mtachukizwa kabisa na kuchukia kwa kuwa imetengwa kwa ajili ya uharibifu.