< Deuteronomy 25 >
1 If there be a controversy between men, and they come nigh unto a court of justice, and they judge them; and they justify the righteous, and condemn the wicked:
Iwapo kutakuwa na malumbano kati ya wanaume na wakaenda mahakamani, na waamuzi wakawahukumu, basi watamwachilia mtakatifu na kumhukumu muovu.
2 Then shall it be, if the guilty man deserve to be beaten, that the judge shall cause him to lie down, and to be beaten before his face, according to the degree of his fault, by a [certain] number.
Iwapo mwanamume mwenye hatia anastahili kupigwa, basi muamuzi atamfanya alale chini na kupigwa mbele zake kwa idadi iliyoamriwa kulingana na kosa lake.
3 Forty stripes may he give him, not more; so that he shall not exceed to have him beaten above these with too many stripes, and thy brother be thus rendered vile before thy eyes.
Muamuzi anaweza kumpatia mapigo arobaini, lakini hapaswi kuvuka idadi hiyo; kwa maana akivuka idadi hiyo na kumpiga kwa mapigo mengi zaidi, basi Muisraeli mwenzako atakuwa kaaibishwa mbele ya macho yenu.
4 Thou shalt not muzzle the ox when he thresheth out the corn.
Haupaswi kumfunga punda wako pua na mdomo anapokuwa akilima shamba lako.
5 If brothers dwell together, and one of them die, and have no child: then shall the wife of the dead not be married abroad, unto a stranger; her husband's brother shall go in unto her, and take her to himself for wife, and perform the duty of a husband's brother unto her.
Iwapo kaka wanaishi pamoja na mmoja wao akafariki bila kuwa na mwana, basi mke wa marehemu hatakiwi kuolewa na mtu nje ya familia. Badala yake, kaka yake mumewe anapaswa kulala naye na kumchukua kuwa mke wake na kutekeleza wajibu wa kaka wa mume kwake.
6 And it shall be, that the first-born whom she may bear shall succeed in the name of his brother who is dead; so that his name be not blotted out of Israel.
Hii ni kwamba mtoto wa kwanza atakayezaliwa arithi chini ya jina la kaka yake mwanamume aliyefariki, ili jina lake lisiangamie ndani ya Israeli.
7 And if the man have no desire to take his sister-in-law: then shall his sister-in-law go up to the gate unto the elders, and say, My husband's brother refuseth to raise up unto his brother a name in Israel, he will not perform on me the duty of a husband's brother.
Lakini kama mwanamume hataki kumchukua mke wa kaka yake awe wake, basi mke wa kaka yake anapaswa kwenda malangoni mpaka kwa wazee na kusema, “Kaka wa mume wangu amekataa kuwajibika kwa niaba ya jina la kaka yake humu Israeli; hataki kufanya wajibu wa kaka wa mume kwangu”.
8 Then shall the elders of his city call him, and speak unto him; and if he persist, and say, I have no desire to take her:
Kisha wazee wa mji wake wanapaswa kumuita na kuzungumza naye. Lakini tuseme atasisitiza na kusema, “Sitaki kumchukua”.
9 Then shall his sister-in-law come nigh unto him in the presence of the elders, and pull his shoe from off his foot, and spit out before him, and shall commence and say, Thus shall be done unto that man that will not build up his brother's house.
Basi mke wa kaka yake anatakiwa kuja kwake mbele ya wazee, kumvua ndara zake miguuni mwake, na kumtemea usoni. Anapaswa kumjibu na kusema, “Hivi ndivyo kinachofanyika kwa mwanamume asiyetaka kujenga nyumba ya kaka yake”.
10 And his name shall be called in Israel, The house of the barefooted.
Jina lake Israeli litaitwa, “Nyumba ya mtu aliyevuliwa ndara zake”.
11 When men strive together one with the other, and the wife of the one draweth near to deliver her husband out of the hand of him that smiteth him, and putteth forth her hand, and taketh him by the secrets:
Iwapo wanamume wamepigana wao kwa wao, na mke wa mmoja wao kaja kumkomboa mumewe dhidi ya yule aliyempiga, naye akanyosha mkono wake na kumshika sehemu za siri,
12 Then shalt thou cut off her hand, thy eye shall not have pity.
basi unapaswa kuukata mkono yake; jicho lako halipaswi kuwa na huruma.
13 Thou shalt not have in thy bag divers weights, a great and a small.
Haupaswi kuwa na mizani ya uzito tofauti katika mfuko wako, mkubwa na mdogo.
14 Thou shalt not have in thy house divers measures, a great and a small.
Hautakiwi kuwa na vipimo tofauti ndani ya nyumba yako, vikubwa na vidogo.
15 A perfect and just weight shalt thou have, a perfect and just measure shalt thou have; in order that thy days may be prolonged in the land which the Lord thy God giveth thee;
Unatakiwa kuwa na uzito kamili na wa haki; unatakiwa kuwa na vipimo kamili na vya haki, ili siku zako ziwe ndefu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia.
16 For an abomination of the Lord thy God is every one that doth such things, every one that acteth unrighteously.
Kwa maana wote wanaofanya vitu hivi, wote wanaovunja haki, ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
17 Remember what 'Amalek did unto thee, by the way, at your coming forth out of Egypt;
Kumbuka ni jambo gani Amaleki alichofanya kwako barabarani ulipokuwa ukitoka Misri,
18 How he met thee by the way, and smote the hindmost of thee, all that were feeble behind thee, when thou was faint and weary; and he feared not God.
jinsi alivyokutana na wewe barabarani na kuwashambulia kati yenu kwa nyuma, wale waliokuwa wamelegea nyuma, mlipokuwa dhaifu na kuchoka, hakumheshimu Mungu.
19 And it shall come to pass, when the Lord thy God giveth thee rest from all thy enemies round about, in the land which the Lord thy God giveth thee for an inheritance to possess it, that thou shalt blot out the remembrance of 'Amalek from under the heavens: thou shalt not forget.
Kwa hiyo, Yahwe Mungu wako atakapowapa pumziko kutoka kwa maadui zako kila sehemu, katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia kumiliki kama urithi, hautakiwi kusahau kuwa unapaswa kufuta kumbukumbu ya Waamaleki chini ya mbingu.