< Deuteronomy 23 >
1 He that is wounded in the testicles, or hath his privy member cut, shall not enter into the congregation of the Lord.
Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
2 One born from prohibited connections shall not enter into the congregation of the Lord; even the tenth generation of him shall not enter into the congregation of the Lord.
Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
3 An 'Ammonite and a Moabite shall not enter into the congregation of the Lord; even the tenth generation of him shall not enter into the congregation of the Lord, for ever;
Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
4 For the reason, that they met you not with bread and with water on the way, when ye came forth out of Egypt; and because he hired against thee Bil'am the son of Beor of Pethor in Mesopotamia, to curse thee;
Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
5 But the Lord thy God would not hearken unto Bil'am; and the Lord thy God changed unto thee the curse into a blessing, because the Lord thy God loved thee.
Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
6 Thou shalt not seek their peace and their welfare all thy days, for ever.
Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
7 Thou shalt not abhor an Edomite; for he is thy brother; thou shalt not abhor an Egyptian; because thou wast a stranger in his land.
Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
8 The children that are born unto them in the third generation, may enter of them into the congregation of the Lord.
Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
9 When thou goest forth into camp against thy enemies, then keep thyself from every evil thing.
Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
10 If there be among thee any man, that is not clean by reason of an occurrence by night; then shall he go abroad to without the camp, he shall not come within the camp;
Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
11 But it shall be, that toward evening he shall bathe himself in water; and when the sun goeth down, he may come into the midst of the camp.
Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
12 And a place shalt thou have without the camp, whither thou shalt go forth abroad:
Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
13 And a spade shalt thou have with thy weapons: and it shall be, when thou sittest abroad, that thou shalt dig therewith, and shalt afterward cover that which cometh from thee;
na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
14 For the Lord thy God walketh in the midst of thy camp, to deliver thee and to give up thy enemies before thee; therefore shall thy camp be holy; that he see no unseemly thing in thee, and turn away from thee.
Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
15 Thou shalt not deliver unto his master the servant who may escape unto thee from his master;
Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
16 With thee shall he dwell, in the midst of thee, in the place which he may choose in any one of thy gates, where it seemeth best to him: thou shalt not oppress him.
Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
17 There shall not be a prostitute of the daughters of Israel, and there shall not be a sodomite of the sons of Israel.
Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
18 Thou shalt not bring the hire of a harlot, or the price of a dog, into the house of the Lord thy God for any vow; for both of these are equally an abomination unto the Lord thy God.
Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
19 Thou shalt not take interest from thy brother, interest of money, interest of victuals, interest of any thing that is lent upon interest:
Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
20 From an alien thou mayest take interest; but from thy brother thou shalt not take interest; in order that the Lord thy God may bless thee in all the acquisition of thy hand, in the land whither thou goest to possess it.
Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
21 When thou makest a vow unto the Lord thy God, thou shalt not delay to pay it; for the Lord thy God will surely require it of thee; and it would be sin in thee.
Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
22 But if thou forbear to vow, it shall be no sin in thee.
Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
23 What is gone out of thy lips shalt thou keep and perform, as thou hast vowed unto the Lord thy God voluntarily, as thou hast spoken with thy mouth.
Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
24 When thou comest into thy neighbor's vineyard, thou mayest eat grapes at thy own pleasure, till thou have enough; but into thy vessel shalt thou not put any.
Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
25 When thou comest into the standing corn of thy neighbor, thou mayest pluck ears with thy hand; but a sickle shall thou not move over thy neighbor's standing corn.
Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.