< Deuteronomy 1 >
1 These are the words which Moses spoke unto all Israel on this side of the Jordan, in the wilderness, in the plain opposite Suph, between Paran, and Tophel, and Laban, and Chazeroth, and Di-zahab.
Haya ni maneno ambayo Musa aliyasema kwa Israeli wote ng'ambo ya jangwa la Yordani, katika tambarare ya mto wa Yordani juu ya Suph, katikati mwa Paran, Topheli, Laban, Hazeroth, na Di Zahab.
2 It is a journey of eleven days from Horeb by the way of mount Seir unto Kadesh-barnea'.
Ni safari ya siku kumi na moja toka Horabu kupitia njia ya mlima wa Seir kwenda Kadeshi Barnea.
3 And it came to pass in the fortieth year, in the eleventh month, on the first day of the month, that Moses spoke unto the children of Israel, according to all that the Lord had commanded him concerning them;
Ilitokea kwenye mwaka wa nne, mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, Musa alizungumza kwa watu wa Israeli, kuambia yote yale Yahwe aliyomwamuru kuhusu wao.
4 After he had smitten Sichon the king of the Emorites, who dwelt in Cheshbon, and 'Og the king of Bashan, who dwelt at 'Ashtaroth in Edre'i.
Hii ilikuwa baada ya Yahwe kumvamia Sihoni mfalme wa Amoria, ambaye aliishi huko Heshboni, na Ogi mfalme wa Bashani, ambaye aliishi huko Ashtarothi ya Edrei.
5 On this side of the Jordan, in the land of Moab, began Moses to explain this law, saying,
Ng'ambo ya Yordani, katika nchi ya Moabu, Musa alianza kutangaza maelekezo haya, akisema,
6 The Lord our God spoke unto us in Horeb, saying, Ye have tarried long enough at this mount;
“Yahwe Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, akisema, umeishi vya kutosha katika milima ya nchi hii.
7 Turn you, and take your journey, and go to the mountain of the Emorites, and unto all its neighboring places, in the plain, in the mountain, and in the lowlands, and in the southern country, and by the coast of the sea, to the land of the Canaanites, and unto the Lebanon, up to the great river, the river Euphrates.
Geuka na uanze safari yako, na uende kwenye nchi ya milima ya Amorites, na kwenye maeneo yote karibu na tambarare ya mto Yordani, katika nchi ya milima, na nyanda za chini, huko Negev, na pwani - nchi ya Wakanani na huko Lebanoni mbali ya mto mkuu wa Euphratesi.
8 Behold, I have given up the land before you: go in and take possession of the land which the Lord hath sworn unto your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give it unto them and to their seed after them.
Tazama, nimetenga nchi kwa ajili yako, nenda ndani na umiliki nchi ambayo Yahwe aliapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka na Yakobo, kuwapa na uzao wao baada yao.
9 And I said unto you at that time, as followeth, I am not able alone to bear you:
Nilisema nawe kwa wakati huo, nikisema, siwezi nikakubeba peke yangu,
10 The Lord your God hath multiplied you, and, behold, ye are this day as the stars of heaven for multitude.
Yahwe Mungu wako amekuzidisha, na tazama, leo umekuwa umati wa nyota angani.
11 May the Lord the God of your fathers make you a thousand times as many more as ye are; and bless you, as he hath spoken unto you.
Yahwe aweza, Mungu wa baba zako, kukufanya wewe mara elfu moja zaidi ya ulivyo, na kukubariki, kama alivyokuahidi!
12 How can I by myself alone bear your cumbrance, and your burden, and your strife!
Lakini inawezekanaje mimi peke yangu kubeba shehena zako, mizigo yako, na migogoro yako?
13 Furnish for yourselves wise and understanding men, and those known among your tribes, and I will place them as chiefs over you.
Chukua wanaume wa hekima, wanaume waelewa, na wanaume walio na sifa nzuri toka kila kabila, nitawafaya kuwa vichwa juu yenu.
14 And ye answered me, and said, The thing which thou hast spoken is good to do.
Mlinijibu na kusema, 'Jambo ulilolisema ni zuri kwetu kufanya.'
15 And I took the chiefs of your tribes, wise and known men, and I set them as heads over you, captains over thousands, and captains over hundreds, and captains over fifties, and captains over tens, and as officers for your tribes.
Kwa hiyo nilichukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wa hekima, na wanaume wenye sifa nzuri, na nikawafanya kuwa vichwa juu yenu, jemedari kwa elfu, jemedari kwa hamsini, jemedari kwa kumi, na maakida, kabila kwa kabila.
16 And I commanded your judges at that time, saying, Hear the causes between your brethren, and judge righteously, between a man and his brother, and between his stranger.
Niliwaamuru waamuzi wenu kwa wakati huo, kusema, 'Zikiliza mabishano kati ya ndugu zenu, na muhukumu ya haki kati ya ndugu na ndugu zake, na mgeni aliye pamoja naye.
17 Ye shall not respect persons in judgment; the small as well as the great shall ye hear; ye shall not be afraid of any man; for the judgment belongeth to God: and the cause that is too hard for you shall ye bring unto me, and I will hear it.
Hamtaonesha upendeleo kwa yeyote katika mgogoro, mtasikia madogo na makubwa pia. Hamtaogopa uso wa mtu, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Migogoro iliyo migumu kwenu, mtaniletea mimi, na mimi nitaisikiliza.
18 And I commanded you at that time all the things which ye should do.
Niliwaamuru kwa wakati huo mambo yote mtakayofanya.
19 And we departed from Horeb, and we went through all that great and terrible wilderness, which ye have seen, by the way of the mountain of the Emorites, as the Lord our God had commanded us; and we came as far as Kadesh-barnea'.
Tulisafiri toka Horebu na kwenda kupitia jangwa lile kubwa lote na lenye kutisha lile mliloliona, katika njia yetu kuelekea nchi ya milima huko Amorites, kama Yahwe Mungu wetu alivyotuamuru sisi, na tukaja Kadeshi ya Barnea.
20 And I said unto you, Ye are come unto the mountain of the Emorites, which the Lord our God doth give unto us.
Niliwambia, mmekuja kwenye nchi ya milima ya Amorites, ambayo Yahwe Mungu wetu anatupa sisi.
21 Behold, the Lord thy God hath given up the land before thee: go up and take possession of it, as the Lord the God of thy fathers hath spoken unto thee; do not fear, and be not discouraged.
Tazama, Yahwe Mungu wenu amekwisha weka nchi mbele yenu; nenda juu, muimiliki, kama Yahwe, Mungu wa baba zenu, amekwisha zungumza nanyi, msiogope wala kukata tamaa.
22 And ye all came near unto me and said, Let us send out men before us, that they may search out for us the land, and bring us word again concerning the way by which we must go up, and the cities to which we shall come.
Kila moja wenu alikuja kwangu na kusema, 'Basi tutume watu mbele yetu, ili kwamba waweze kupepeleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea sisi neno kuhusiana na njia ya wapi tuvamie, na kuhusiana na miji tutakayoingia.
23 And the thing was pleasing in my eyes; and I took of you twelve men, one man for every tribe:
Shauri hilo lilinibariki mimi, 'Nilichukua watu kumi na mbili kutoka kwenu, mtu moja kwa kila kabila.
24 And they turned and went up into the mountain, and came unto the valley of Eshcol, and spied it out.
Waligeuka na kwenda juu ya nchi ya milima, kufika kwenye bonde la Eshcol na kufanya upepelezi wa kina.
25 And they took in their hand some of the fruit of the land, and brought it down unto us; and they brought us word again, and said, The land which the Lord our God doth give us is good.
Walichukua baadhi ya mazao ya ardhi mikononi mwao na kuleta kwetu, Pia walileta neno na kusema, 'Ni nchi nzuri ambayo Yahweh Mungu wetu anatupa sisi'
26 But you would not go up, and ye rebelled against the order of the Lord your God;
Bado mlikataa kushambulia, lakini mliasi dhidi ya amri ya Yahwe Mungu wenu.
27 And ye murmured in your tents, and said, On account of the hatred of the Lord toward us, hath he brought us forth out of the land of Egypt, to deliver us into the hand of the Emorites, to destroy us.
Mlilalamika katika mahema yenu na kusema, “Ni kwa sababu Yahwe alituchukia sisi kwa kuwa ametutoa katika nchi ya Misri, kuteweka katika mikono ya Amorites kutuangamiza.
28 Whither shall we go up? our brethren have made faint our heart, saying, The people is greater and taller than we; the cities are great and fortified up to heaven; and moreover the sons of the 'Anakim have we seen there.
Tuende wapi sasa? Ndugu zetu wamefanya mioyo yetu kuyeyuka, kusema, Hao watu ni wakubwa na warefu zaidi yetu, miji yao ni mikubwa na imeimarishwa kwenda mbinguni; zaidi ya yote, tumewaona wana wa Anakim huko”
29 And I said unto you, Have no dread, nor be ye afraid of them.
Kisha nikasema nao, msitishwe wala msiwaogope.
30 The Lord your God who goeth before you, he it is who will fight for you; all just as he did for you in Egypt before your eyes;
Yahwe Mungu wenu, ambaye aenda mbele yenu, atawapigania, kama yote aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu,
31 And in the wilderness which thou hast seen, where the Lord thy God bore thee, as a man doth bear his son, on all the way that ye have gone, until ye came unto this place.
na pia katika jangwa, ambapo mmekwisha muona Yahwe Mungu wenu jinsi alivyowabeba, kama mtu abebavyo mtoto wake, kokote mlikoenda mpaka kufika hapa.'
32 Yet in this thing do ye not believe in the Lord your God,
Bado licha ya neno hili hakumwamini Yahwe Mungu wenu,
33 Who goeth before you on the way to seek out for you a place for your encamping, in fire by night, to cause you to see on the way in which ye are to go, and in a cloud by day.
aliyeenda mbele yenu kwenye njia kutafuta eneo kwa ajili yenu kuweka kambi, katika moto kwa usiku, katika mawingu kwa mchana.
34 And the Lord heard the voice of your words; and he was wroth, and swore, saying,
Yahwe alisikia sauti ya maneno yenu na alikasirika; aliapa na kusema,
35 Surely there shall not one of these men of this evil generation see that good land, which I have sworn to give unto your fathers;
Hakika hakuna mmoja ya hawa watu wa kizazi hiki kiovu wataona nchi nzuri ambayo niliapa kuwapa babu zao,
36 Save Caleb the son of Yephunneh, he shall see it, and to him will I give the land upon which he hath trodden, and to his children; because he hath wholly followed the Lord.
kasoro Kalebu mwana wa Jephuneeh; yeye ataiona. Yeye nitampa nchi ambayo amekwisha kuikanyanga, na watoto wake, kwa sababu alimfuata Yahwe kwa ukamilifu.'
37 also with me was the Lord angry for your sakes, saying, also thou shalt not go in thither.
Pia Yahweh alinikasirikia mimi kwa sababu yenu, kusema, 'Wewe pia hautaingia huko,
38 Joshua the son of Nun, who standeth before thee, he shall go in thither: him encourage; for he shall cause Israel to inherit it.
Yoshua mwana wa Nuh, ambaye amesimama mbele yako, yeye ataingia, mtie moyo, kwani yeye atawaongoza Israeli kuimiliki.
39 And your little ones, of whom ye said, They will become a prey, and your children who know not this day either good or evil, these shall go in thither; and unto them will I give it, and they shall possess it.
Zaidi ya yote, watoto wenu wadogo, ambao mlisema watakuwa waathirika, ambao leo hawana elimu ya uzuri au ubaya-wataenda ndani huko. Wao nitawapa nchi hiyo, na wataimiliki.
40 But as for you, turn you, and take your journey into the wilderness by the way of the Red Sea.
Lakini ninyi, geuka na muuanza safari kwenda jangwani kwa kuambaa njia ya bahari ya mianzi'.
41 And ye answered and said unto me, We have sinned against the Lord; we indeed will go up and we will fight, according to all that the Lord our God hath commanded us; and ye girded on every man his weapons of war, and ye insisted to go up into the mountain.
Kisha mlinijibu na kusema kwangu, 'Tumetenda dhambi dhidi ya Yahwe, tutaenda juu na kupigana, tutafuata yote ambayo Yahwe Mungu wetu ametuamuru sisi kufanya'. Kila mtu miongoni mwenu aliweka silaha za vita, na mlikuwa tayari kuvamia nchi ya milima.
42 And the Lord said unto me, Say unto them, Go not up, and do not fight; for I am not among you; lest ye be smitten before your enemies.
Yahwe alisema nami, 'Waambie, msivamie na kupigana, kwa kuwa sitakuwa pamoja nanyi, na mtashindwa na adui zenu'.
43 And I spoke unto you; but ye would not hear; and ye rebelled against the order of the Lord, and you were presumptuous, and went up into the mountain.
Nilizungumza nanyi kwa njia hii, lakini hamkunisikiliza, Mliasi dhidi ya amri ya Yahwe, mlikuwa wenye kiburi na mlivamia nchi ya milima.
44 And the Emorites, who dwelt in that mountain: came out against you, and they pursued you, as the bees do, and they overthrew you in Seir, as far as Chormah.
Lakini Amorites, ambayo waliishi katika nchi hiyo ya milima, walitoka dhidi yenu na kuwafukuza kama nyuki, na kuwapiga chini huko Seir, mbali kama Hormah.
45 And ye returned and wept before the Lord; but the Lord hearkened not to your voice, nor gave ear unto you.
Mlirudi na kulia mbele ya Yahwe; lakini Yahwe hakusikiliza sauti zenu, wala hakuwa makini kwenu.
46 And ye tarried in Kadesh many days, according unto the days that ye tarried there.
Kwa hiyo mlibaki Kadeshi siku nyingi, siku zote mlibaki huko.