< 2 Kings 5 >

1 And Na'aman, the captain of the army of the king of Syria, was a great man before his Lord, and highly honored; because by him had the Lord given victory unto Syria: and this man was valiant in war, [but] a leper.
Basi Naamani, amri jeshi wa mfalme wa Shamu, alikuwa mtu mkubwa na mtu mwenye kuheshimiwa mbele ya bwana wake, kwa sababu kwa ajili yake Yahwe aliwapa ushindi Washami. Pia alikuwa hodari, mtu shujaa, lakini alikuwa anaukoma.
2 And the Syrians had gone out in predatory troops, and had brought away captive out of the land of Israel a little maiden; and she waited on Na'aman's wife.
Washami walikuwa wametoka kuongoza kikosi na kumchukua kijana mdogo wa kike kutoka nchi ya Israeli. Akamuhudumia mke wa Naamani.
3 And she said unto her mistress, Oh that my Lord were but before the prophet that is in Samaria! then would he heal him of his leprosy.
Yule binti akamwambia bibi yake, “Natamani kwamba bwana wangu angelikuwa na nabii ambaye yupo Samaria! Halafu angelimponya bwana wangu ukoma wake.
4 And he went in, and told his lord, saying, Thus and thus hath spoken the maiden that is from the land of Israel.
Hivyo Naamani akaingia na kumwambia mfalme kile ambacho yule binti kutoka nchi ya Israeli alichokuwa amekisechosema.
5 And the king of Syria said, Go to, go, and I will send a letter unto the king of Israel. And he departed, and took with him ten talents of silver, and six thousand pieces of gold, and ten changes of garments.
Kisha mfalme wa Shamu akase, “Nenda sasa, na nitatuma barua kwa mfalme wa Israeli.” Naamani akaondoka na kuchukua talanta zake kumi za fedha, vipande elfu sita vya dhahabu, na nguo kumi za kubadilisha.
6 And he brought the letter to the king of Israel, which said, And now when this letter cometh unto thee, behold, I have sent to thee Na'aman my servant, that thou mayest heal him of his leprosy.
Pia alichukua barua ya kumpelekea mfalme wa Israeli inayosema, “Sasa wakati hii barua itakapoletwa kwako, utaona kwamba nimemtuma mtumishi wangu Naamani kwako, hivyo basi utamponya ukoma wake.”
7 And it came to pass, when the king of Israel read the letter, that he rent his clothes, and said, Am I God, to kill and to make alive, that this one doth send unto me to heal a man of his leprosy? for know to a certainty, I pray you, and see that he but seeketh a quarrel against me.
Wakati mfalme wa Israeli alipoisoma ile barua, alichana mavazi yake na kusema, “Je mimi ni Mungu, niue na nirudishe uhai, kwamba huyu mtu anataka nimponye mtu ukoma wake? Inaonekana anatafuta mashindano na mimi.”
8 And it happened, when Elisha' the man of God heard that the king of Israel had rent his clothes, that he sent to the king, saying, Wherefore hast thou rent thy clothes? let him but come to me, and he shall know that there is a prophet in Israel.
Ikawa wakati Elisha mtu wa Mungu aliposikia kwamba mfalme wa Israeli alichana nguo zake, akatuma neno kwa mfalme akisema, “Kwa nini umechana nguo zako? Muache aje kwangu sasa, na atajua kwamba kuna nabii katika Israeli.”
9 And Na'aman came with his horses and with his chariot, and remained at the door of the house of Elisha'.
Basi Naamani akaja na farasi wake na mikokoteni yake ya kukokotwa na farasi na kusimama kwenye mlango wa nyumba ya Elisha.
10 And Elisha' sent a messenger unto him, saying, Go and bathe seven times in the Jordan, and thy flesh shall be restored [healthy] to thee, and thou shalt become clean.
Elisha akamtumia mjumbe, akisema, “Nenda na ukazame mwenyewe katika Yordani mara saba, na ngozi ya mwili wako itajirudi; utakuwa msafi.”
11 But Na'aman became wroth, and went away, and said, Behold, I had thought, He will surely come out to me, and stand, and call on the name of the Lord his God, and swing his hand over the place, and heal the leper.
Lakini Naamani alikasirika na kuondoka na kusema, “Tazama, Nilidhani bila shaka angekuja kwangu na kusimama na kuliita jina la Yahwe Mungu wake, na kupitisha mkono wake kwenye sehemu ya ugonjwa na kuponya ukoma wangu.
12 Are not Amanah and Pharpar, the rivers of Damascus, better than all the waters of Israel? may I not bathe in them, and become clean? and he turned and went away in a rage.
Je sio Abana na Faepari, mito ya Damaskasi, bora kuliko maji yote ya Israeli?” Je siwezi kuoga ndani yao na kuwa safi?” Hivyo akageuka na kwenda kwa hasira.
13 And his servants came near, and spoke unto him, and they said, My father, if the prophet had bidden thee a great thing, wouldst thou not do it? how much rather then, when he hath said to thee, Bathe, and become clean?
Ndipo watumishi wa Naamani wakaja karibbu na kumwambia, “Baba yangu, kama yule nabii alikuamuru kufanya kitu kigumu, singelifanya? Je si zaidi basi, atakapokwambia rahisi, 'Zama mwenyewe na uwe safi?”
14 Then went he down, and dived seven times in the Jordan, according to the word of the man of God: and his flesh was restored [healthy] like the flesh of a little boy, and he became clean.
Ndipo akashuka chini na kuzama mwenyewe mara saba kwenye Yordani, akitii maelekezo ya mtu wa Mungu. Nyama ya mwili wake ikarudi tena kama nyama ya mwili ya mtoto mdogo, na alikuwa amepona.
15 And he returned to the man of God, he with all his camp, and came and stood before him, and said, Behold, now I know that there is no god on all the earth, but in Israel; and now, I pray thee, take a present from thy servant.
Naamani akarudi kwa yule mtu wa Mungu, yeye na watu wake wengine, na kuja na kusimama mbele yake. Akasema, “Tazama, sasa najua kwamba hakuna Mungu katika Dunia nzima isipokuwa katika Israeli. Kwa hiyo basi, chukua zawadi kutoka kwa mtumishi wako tafadhali.”
16 But he said, As the Lord liveth before whom I have stood, I will take none: and he urged him to take it; but he refused.
Lakini Elisha akajibu, “Kama Yahwe aishivyo, ambaye nimesimama mbele yake, sintopokea chochote.”Naamani akamsihi Elisha apokee zawadi, lakini alikataa.
17 And Na'aman said, If [thou wilt] not, [then] let there be given, I pray thee, unto thy servant two mules' burden of earth; for thy servant will not offer henceforth either burnt-offering or peace-sacrifice unto other gods, except unto the Lord.
Hivyo Naamani akasema, “Kama sivyo, nakuomba ache apewe mtumishi wako pale mzigo wa baghala mbili za aridhi, kwa kuwa kuanzia sasa, mtumishi wako hatotoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa mungu yeyote isipokuwa Yahwe.
18 For this thing may the Lord pardon thy servant, that when my Lord goeth into the house of Rimmon to prostrate himself there, and he leaneth on my hand, and I prostrate myself also in the house of Rimmon: when I prostrate myself in the house of Rimmon, may the Lord pardon thy servant for this thing.
Katika jambo hili moja Yahwe anaweza kumsamehe mtumishi wako, hii ni, wakati mfalme wangu atakapoenda kwenye nyumba ya Rimoni kuabudu pale, na kujifunza kwenye mikono yangu na kumuinamia mwenyewe kwenye nyumba ya Rimoni, Yahwe aweze kumsamehe mtumishi wako katika hili jambo.”
19 And he said unto him, Go in peace: so he departed from him some distance.
Elisha akamwambia, “Nenda kwa amani.” Hivyo Naamani akaondoka.
20 But Gechazi, the servant of Elisha' the man of God, said, Behold, my master hath spared Na'aman, this Syrian, in not receiving from his hand what he had brought; but, as the Lord liveth, I will run after him, and take some little thing from him.
Alikuwa amesafiri lakini umbali mfupi, wakati Gehazi mtumishi wa Elisha mtumishi wa Mungu alisema mwenyewe, “Tazama, bwana wangu amemuandaa huyu Naamani Mshami kwa kuacha kupokea zawadi kutoka kwenye mikono yake ambazo alizileta. Kama Yahwe aishivyo, Nitakimbia nikimfuata na kupokea kitu kutoka kwake.
21 So Gechazi hurried after Na'aman; and when Na'aman saw him running after him, he lighted doom from the chariot to meet him, and said, Is [all] well?
Hivyo Gehazi akamfuata Naamani. Wakati Naamani alipomuona mtu mmoja anakimbia akimfuata, aliruka chini kutoka kwenye gari yake kuonana naye na kusema, “Je kila kitu kiko sawa?”
22 And he said, [all] is well. My master hath sent me, saying, Behold, even now there are come to me from the mountain of Ephraim two young men of the sons of the prophets: do give them, I pray thee, a talent of silver, and two changes of garments.
Gehazi akasema, “kila kitu kiko sawa. Bwana wangu amenituma, akisema, 'Tazama, sasa wamekuja kwangu kutoka nchi ya mlima ya Efraimu vijana wawili wa watoto wa manabii. Tafadhali, wapatie talanta ya fedha na nguo mbili za kubadilisha.”
23 And Na'aman said, Give thy assent, take two talents. And he urged him, and bound up two talents of silver in two bags, with two changes of garments, and he gave them unto his two young men, and they carried them before him.
Naamani akajibu, “Ninafuraha kubwa kukupatia talanta mbili.” Naamani akamsihi Gehazi na kujaribu talanta mbili za fedha kwenye mifuko miwili ya kubebea, pamoja na nguo mbili za kubadilisha, na kutandaza kwa wafanyakazi wake wawili, ambao walikuwa wamebebea ile mifuko miwili ya fedha mbele ya Gehazi.
24 And when he came to the hill, he took them from their hand, and bestowed them in the house: and he dismissed the men, and they departed.
Wakati Gehazi alipokuja kwenye ule mlima, alichukua ile mifuko ya fedha kutoka kwenye mikono yao na kuificha kwenye nyumba; akawatuma wale watu, na wakaondoka.
25 But he went in, and stood before his master. And Elisha' said unto him, Whence comest thou, Gechazi? And he said, Thy servant went not hither or thither.
Wakati Gehazi alipoingia na kusimama mbele ya bwana wake, Elisha akamwambia, “Umetokea wapi, Gehazi?” Akajibu, “Mtumishi wako hakwenda mahali.”
26 And he said unto him, My mind was not gone, when the man turned round from his chariot to meet thee. Is it a time to take money, and to take garments, and oliveyards, and vineyards, and sheep, and oxen, and men-servants, and maid-servants?
Elisha akamwambia Gehazi, “Je roho yangu haikuwa na wewe wakati yule mtu alipoyarudisha magari yake ya farasi ili kukutana na wewe? Je uu ni mda wa kupokea pesa na nguo, mashamba ya mzaituni na mizabibu, na kondoo na Ng'ombe, na watumishi wakiume na watumishi wakike?
27 May then the leprosy of Na'aman cleave unto thee, and unto thy seed for ever. And he went out from his presence a leper [as white] as snow.
Basi ukoma wa Naamani utakuwa kwenye uzao wako daima.” Basi Gehazi akatoka kwenye uwepo wake, mwenye ukoma kama theluji.

< 2 Kings 5 >