< 2 Kings 13 >

1 In the three and twentieth year of Joash the son of Achazyahu the king of Judah became Jehoachaz the son of Jehu king over Israel in Samaria [for] seventeen years.
Katika mwaka wa ishirini na tatu wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoazi mwana wa Yehu alianza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; alitawala miaka kumi na saba.
2 And he did what is evil in the eyes of the Lord, and followed the sins of Jerobo'am the son of Nebat, who induced Israel to sin: he departed not therefrom.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe na kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli kuasi; na Yehoazi hakurudi kutoka kwao
3 And the anger of the Lord was kindled against Israel; and he gave them up into the hand of Chazael the king of Syria, and into the hand of Ben-hadad the son of Chazael, all the time.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, na akaendelea kuwakabidhi kwenye mikono ya Hazaeli mfalme wa Shamu na kwenye mikono ya Ben Hadadi mwana wa Hazaeli.
4 And Jehoachaz besought the Lord; and the Lord hearkened unto him; for he saw the oppression of Israel, how the king of Syria oppressed them.
Hivyo Yehoazi akamsihi Yahwe, na Yahwe akamsikiliza kwa sababu aliona mateso ya Israeli, vile mfalme wa Shamu alivyokuwa akiwatesa.
5 (And the Lord gave Israel a deliverer, so that they came out from under the power of the Syrians: and the children of Israel dwelt in their tents, as in times past.
Basi Yahwe akawapa Israeli ulinzi, na wakakimbia kutoka kwenye mikono ya Washami, na watu wa Israeli wakaanza kuishi kwenye nyumba zao kama walivyokuwa kabla.
6 Nevertheless they departed not from the sins of the house of Jerobo'am, who induced Israel to sin, therein the people walked: and the Asherah also remained standing in Samaria.)
Hata hivyo, hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambaye alisabisha Israeli kuasi, na wakaendelea katika hayo; na huyo Ashera akabaki hivyo katika Samaria.
7 For he had left of people to Jehoachaz none but fifty horsemen, and ten chariots, and ten thousand men on foot; for the king of Syria had destroyed them, and had made them like the dust at threshing.
Washami wakamuacha Yehoazi pamoja na waendesha farasi hamsini tu, magari ya farasi kumi, na watembea kwa miguu elfu kumi, kwa ajili ya mfalme wa Shamu alikuwa ameiharibu na kuwafanya kama makapi yaliyopurwa.
8 Now the rest of the acts of Jehoachaz, and all that he did, and his mighty deeds, behold, they are written in the book of the chronicles of the kings of Israel.
Kama mambo mengine yanayomuhusu Yehoazi, na yote aliyoyafanya na nguvu zake, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
9 And Jehoachaz slept with his fathers; and they buried him in Samaria: and Joash his son became king in his stead.
Basi Yehoyazi akalala na mababu zake, na wakamzika katika samaria. Yohoashi mwanaye akawa mfalme katika sehemu yake.
10 In the thirty and seventh year of Joash the king of Judah became Jehoash the son of Jehoachaz king over Israel in Samaria, [for] sixteen years.
Katika mwaka wa thelathini na saba wa Yoashi mfalme wa Yuda, utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoazi ulianza juu ya Israeli katika Samaria; alitawala miaka kumi na sita.
11 And he did what is evil in the eyes of the Lord; he departed not from all the sins of Jerobo'am the son of Nebat, who induced Israel to sin: therein he walked.
Akafanya yaliyo maovu kwenye uso wa Yahwe. Hakuacha nyuma dhambi zozote za Yeroboamu mwana wa Nebati, kwa kuwa aliwafanya Israeli kuasi, lakini alitembea pamoja nao.
12 And the rest of the acts of Joash, and all that he did, and his mighty deeds wherewith he fought against Amazyah the king of Judah, behold, they are written in the book of the chronicles of the kings of Israel.
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Yehoashi, na yote aliyoyafanya, na shujaa wake ambaye aliyepigana dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
13 And Joash slept with his fathers; and Jerobo'am sat upon his throne: and Joash was buried in Samaria with the kings of Israel.
Yehoashi akalala na mababu zake, na Yeroboamu akakalia kiti chake cha enzi cha kifalme. Yehoashi akazikwa katika Samaria pamoja na wafalme wa Israeli.
14 Now Elisha' was fallen sick of his sickness whereof he had to die. And Joash the king of Israel came down unto him, and wept over his face, and said, O my father, my father, the chariot of Israel, and their horsemen.
Basi Elisha akaugua ugonjwa ambao baadae ulimuua, hivyo Yehoashi yule mfalme wa Israeli akashuka chini kwake na kumlilia juu yake. Akasema, “Baba yangu, baba yangu, haya magari ya farasi ya Israeli na hawa waendesha farasi wanakuchukua!”
15 And Elisha' said unto him, Fetch a bow and arrows. And he fetched unto him a bow and arrows.
Elisha akamwambia, “Chukua upinde na mishale,” basi Yoashi akachukua upinde na mishale.
16 And he said to the king of Israel, Place thy hand upon the bow. And he placed his hand [upon it]: and Elisha' laid his hands upon the king's hands.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Weka mkono wako kwenye upinde,” basi akaweka mkono wake kwenye huo. Kisha Elisha akalaza mikono yake kwenye mikono ya mfalme.
17 And he said, Open the window eastward. And he opened it. Then said Elisha', Shoot. And he shot. And he said, The arrow of victory from the Lord, and the arrow of victory over Syria; and thou shalt smite the Syrians in Aphek, till they be consumed.
Elisha akasema, “Fungua dirisha upande wa mashariki,” basi akalifungua. Kisha Elisha akasema, “Funga”, na akafunga. Elisha akasema, “Huu ndiyo mshale wa ushindi wa Yahwe, huu mshale wa ushindi juu ya Shamu, kwa kuwa utawapiga Washami katika Afeki hadi utakapowaangamiza.”
18 And he said, Take the arrows. And he took them. And he said unto the king of Israel, Strike upon the ground. And he struck three times, and stopped.
Kisha Elisha aksema, “Chukua mishale,” basi Yoashi akaichukua. Akamwambia mfalme wa Israeli, “Piga chini pamoja nao,” na akapiga chini mara tatu, kisha akaacha.
19 And the man of God was angry with him, and said, Thou shouldst have struck five or six times; then wouldst thou have smitten the Syrians till they had been consumed: whereas now thou shalt smite the Syrians three times.
Lakini mtu wa Mungu alikuwa na hasira naye na akasema, “Ungelipiga chini mara tano au mara sita. Ndipo ungeipiga Shamu hadi kuiangamiza, lakini sasa utaipiga Shamu mara tatu tu.”
20 And Elisha' died, and they buried him. And the predatory bands of Moabites frequently invaded the land at the coming in of the year.
Kisha Elisha akafa, na wakamzika. Sasa vikundi vya Wamoabi wakaingia kwenye nchi mwanzoni mwa mwaka.
21 And it came to pass, as they were burying a man, that, behold, they saw the band; and they cast down the man into the sepulchre of Elisha': and as the man came, and touched the bones of Elisha', he revived, and rose up on his feet.
Ikawa walipokuwa wakimzika huyo mtu, wakaona kundi la Wamoabi, hivyo wakautupia ule mwili kwenye kaburi la Elisha. Mara yule mtu alipoigusa mifupa ya Elisha, alifufuka na kusimama kwa miguu yake.
22 But Chazael the king of Syria oppressed Israel all the days of Jehoachaz.
Hazaeli mfalme wa Shamu akawatesa Israeli siku zote za Yehoazi.
23 And the Lord became gracious unto them, and had mercy on them, and turned his regard unto them, because of his covenant with Abraham, Isaac, and Jacob, and would not destroy them, and he cast them not off from his presence even until now.
Lakini Yahwe aliwahurumia Israeli, na alikuwa na huruma juu yao na kushuhulika kwa ajili yao, kwa sababu ya agano lake na Ibrahimu, Isaka, na Yakobo. Hivyo Yahwe hakuwaangamiza, na bado hakuwatupa kutoka kwenye uwepo wake.
24 And Chazael the king of Syria died: and Ben-hadad his son became king in his stead.
Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, na Ben Hadadi mtoto wake akawa mfalme katika sehemu yake.
25 And Jehoash the son of Jehoachaz took again the cities out of the power of Ben-hadad the son of Chazael, which he had taken out of the power of Jehoachaz his father in the war. Three times did Joash beat him, and he recovered the cities of Israel.
Yehoashi mwana wa Yehoazi akairudisha kutoka kwa Ben Hadadi mwana wa Hazaeli miji ambayo aliichukua kutoka Yehoazi baba yake kwa vita. Yehoashi akamshambulia mara tatu, na akaipata miji ya Israeli.

< 2 Kings 13 >