< 2 Kings 11 >

1 And when 'Athalyah the mother of Achazyahu saw that her son was dead, she arose and destroyed all the seed royal.
Basi Athalia, mama yake na Ahazia, alipoona kwamba mtoto wake amekufa, aliinuka na kuwaua watoto wote wa kifalme.
2 But Yehosheba', the daughter of king Joram, the sister of Achazyahu, took Joash the son of Achazyahu, and stole him away from among the king's sons that were slain, him and his nurse into the bed-chamber: and they hid him from 'Athalyah, so that he was not slain.
Lakini Yehosheba, binti wa mfalme Yehoramu na dada wa Ahazia, akamchukua Yoashi mwana wa Ahazia, na kumficha mbali mwa miongoni mwa watoto wa mfalme waliokuwa wameuawa, wakati wote pamoja na mlezi wake; akawaweka kwenye chumba cha kulala. Wakamficha kutoka Athalia kwa hiyo hakuuawa.
3 And he was with her in the house of the Lord hidden for six years, while 'Athalyah was reigning over the land.
Alikuwa pamoja na Yehosheba, wamejificha kwenye nyumba ya Yahwe, kwa mda wa miaka sita, wakati Athalia alipotawala juu ya nchi.
4 And in the seventh year Yehoyada' sent and fetched the rulers over the hundreds, of the guards and the runners, and brought them to him into the house of the Lord, and made a covenant with them, and made them swear in the house of the Lord, and showed them the king's son.
Katika mwaka wa saba, Yehoyada alituma ujumbe na kuleta maamiri jeshi mamia wa Wakari na wa walinzi, na kuwaleta kwake mwenyewe, ndani ya nyumba ya Yahwe. Akafanya agano pamoja nao, na kuwaapisha kiapo katika nyumba ya Yahwe. Kisha akawaonyesha mtoto wa mfalme.
5 And he commanded them, saying, This is the thing that ye shall do: A third part of you that enter in on the sabbath shall even be keeping watch in the king's house;
Akawaamuru, akisema, “Hivi ndivyo mnavyotakiwa kufanya. Theluthi yenu mtakaokuja kwenye Sabato mtakuwa mkiiangalia nyumba ya mfalme,
6 And a third part shall be at the gate of Sur; and a third part at the gate behind the runners; so shall ye keep watch at the house, as a defence.
na theluthi mtakuwa langoni mwa Suri, na theluthi langoni nyuma ya walinzi.”
7 And two parts of you all that are relieved on the sabbath, even they shall keep watch in the house of the Lord about the king.
Makundi mengine mawili ambayo hayatumikii Sabato, Mtayalinda juu ya nyumba ya Yahwe kwa ajili ya mfalme.
8 And ye shall encompass the king round about, every man with his weapons in his hand; and he that cometh within the ranges shall be put to death: and be ye with the king when he goeth out and when he cometh in.
Ni lazima mumzunguke mfalme, kila mmoja na silaha zake kwenye mkono wake. Yeyote aingiaye ndani ya safu, auwawe. Lazima mkae pamoja na mfalme kila atokapo na kila aingiapo.
9 And the captains over the hundreds did in accordance with all that Yohayada' the priest had commanded: and they took every man his men that came in on the sabbath, with those that were to be relieved on the sabbath, and came to Yehoyada' the priest.
Hivyo mamia ya maamri jeshi wakatii kila kitu Yehoyada kuhani alichokiamuru. Kila mmoja akachukua watu wake, wale ambao walitakiwa kuja kutumika siku ya hiyo Sabato, na wale ambao wataacha kuitumika kwenye hiyo Sabato; ndipo wakaja kwa Yehoyada kuhani.
10 And the priest gave to the captains over the hundred the spears and shields that had belonged to king David, that were in the house of the Lord.
Kisha Yehoyada yule kuhani akawapa mikuki na ngao mamia wa maamri jeshi ambayo ilikuwa mali ya mfalme Daudi ambayo ilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe.
11 And the runners stood every man with his weapons in his hand, from the right side of the house to the left side of the house, by the altar and within, round about the king.
Basi walinzi wakasimama, kila mtu na silaha kwenye mkono wake, kutoka upande wa kuume wa hekalu, kwenda upande wa kushoto, karibu na madhabahu ya hekelu, wakimzunguka mfalme.
12 And he brought forth the king's son, and put the crown upon him, and [gave him] the testimony, and they made him king, and anointed him; and they clapped their hands, and said, Long live the king.
Kisha Yehoyada akamleta nje mtoto wa mfalme Yoashi, na kumvalisha taji la kifalme, na kumpatia mikataba ya agano. Kisha wakamfanya mfalme na kummiminia mafuta. Wakapiga makofi wakisema, “Mfalme na aishi!”
13 And when 'Athalyah heard the noise of the runners [and] of the people, she came to the people in the house of the Lord.
Wakati Athalia aliposikia sauti za walinzi na za watu, alikuja kwa wale watu kwenye nyumba ya Yahwe.
14 And she looked, and, behold, the king stood upon a stand, according to custom, and the princes and the trumpeters were by the king, and all the people of the land were rejoicing, and blowing with trumpets: and 'Athalyah then rent her clothes, and cried, Conspiracy! conspiracy!
Akatazama, na, kisha, yule mfalme alikuwa amesimama kwenye nguzo, kama ilivyokuwa desturi, na manahodha na wapiga mabaragumu walikuwa karibu na mfalme. Watu wote wa nchi hiyo walikuwa wakifurahi na kupiga matarumbeta. Kisha Athalia akachana mavazi yake kwa hasira na kupiga kelele, “Uhaini! Uhaini!”
15 But Yehoyada' the priest commanded the captains of the hundreds, the commanders of the army, and said unto them, Lead her forth to within the ranges: and him that followeth her put to death with the sword. For the priest had said, She shall not be slain in the house of the Lord.
Ndipo Yehoyada yule kuhani akawaagiza maamri jeshi wa mamia ambao waliokuwa juu ya jeshi, akisema, “Mtoeni kwenye safu.” Atakayemfuata, muueni kwa upanga.” Kwa kuwa kuhani alisema, “Msimwache auawe kwenye nyumba ya Yahwe.”
16 And they made way for her; and she went by the way of the entrance of the horses into the king's house: and she was put to death there.
Hivyo wakamtwaa kadiri walivyokuwa wakiikaribia hiyo sehemu iliyokuwa na farasi wakaingia chini, na akauawa huko.
17 And Yehoyada' made a covenant between the Lord and between the king and between the people, that they should be a people unto the Lord; and between the king and between the people.
Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yahwe na mfalme na watu, ambao wangekuwa watu wa Yahwe, na pia kati ya mfalme na watu.
18 And then came all the people of the land into the house of Ba'al, and pulled it down: his altars and his images they broke in pieces thoroughly, and Mattan the priest of Ba'al they slew before the altars. And the priest appointed superintendents over the house of the Lord.
Basi watu wote wa nchi wakaenda kwenye nyumba ya Baali na kuingusha chini. Wakaangusha madhabahu ya Baali na sanamu zake wakazivunja vipande vipande, na kumuua Matani, mfalme wa Baali, mbele ya haya madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawachagua walinzi juu ya hekalu la Yahwe.
19 And he took the chiefs over hundreds, and the guards, and the runners, and all the people of the land, and they brought down the king from the house of the Lord, and came by the way of the gate of the runners to the king's house: and he sat on the throne of the kings.
Yehoyada akawachukua maamiri jeshi wa mamia, Wakari, walinzi, na watu wote wa nchi, na kwa pamoja wakamleta chini mfalme kutoka kwenye nyumba ya Yahwe na wakaenda kwenye nyumba ya mfalme, wakaingia kwa njia ya lango la walinzi. Yoashi akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi cha mfalme.
20 And all the people of the land rejoiced, and the city was quiet; but 'Athalyah they had slain with the sword at the king's house.
Hivyo watu wote wa nchi wakamsifu, na nchi ilikuwa kimya baada ya Athalia kuuawa kwa upanga kwenye nyumba ya mfalme.
21 Seven years old was Jehoash when he became king.
Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba tangu alipoanza kutawala.

< 2 Kings 11 >