< 2 Kings 10 >

1 And Achab had seventy sons in Samaria. And Jehu wrote letters and sent them to Samaria, unto the rulers of Yizre'el, the elders, and to those that brought up Achab's children, saying,
Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
2 And now as soon as this letter cometh to you, seeing that there are with you your master's sons, and there are with you the chariots and the horses, and the fortified city, and the armor:
“Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
3 Select then the best and the most fitting of your master's sons, and set him on his father's throne, and fight for your master's house.
mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
4 But they were exceedingly much afraid, and said, Behold, the two kings could not stand before him: how then shall we be able to stand?
Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
5 And the superintendent over the house, and the commander over the city, and the elders, and the bringers up of the children, sent to Jehu, saying, We are thy servants, and all that thou mayest say unto us will we do; we will not set up any one as king: do what is good in thy eyes.
Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
6 Then wrote he to them a letter the second time, saying, If ye be for me, and if ye will hearken unto my voice, then take the heads of the men, your master's sons, and come to me to Yizre'el by this time tomorrow. Now the king's sons, seventy persons, were with the great men of the city, who brought them up.
Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
7 And it came to pass, when the letter came to them, that they took the king's sons and slaughtered them, seventy persons, and put their heads in baskets, and sent them to him to Yizre'el.
Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
8 And the messenger came, and told him, saying, They have brought the heads of the king's sons. And he said, Place ye them in two heaps at the entrance of the gate until the morning.
Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
9 And it came to pass in the morning, that he went out, and stood, and said to all the people, Ye are righteous: behold, I conspired against my master, and slew him; but who hath killed all these?
Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
10 Know now that there shall not fall of the word of the Lord unto the earth, the least that the Lord hath spoken concerning the house of Achab; and the Lord hath done that which he spoke by means of his servant Elijah.
Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
11 And Jehu smote all that yet remained of the house of Achab in Yizre'el, and all his great men, and his acquaintance, and his priests, until he had left him none that escaped.
Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
12 And he arose and departed, and came to Samaria; he was just at the binding-house of the shepherds, on the way:
Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
13 When Jehu met with the brothers of Achazyahu the king of Judah, and he said, Who are ye? And they said, The brothers of Achazyahu are we; and we are come down to salute the children of the king and the children of the queen.
Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
14 And he said, Seize them alive. And they seized them alive, and slaughtered them at the pit of the binding-house, two and forty men; and he left not one of them remaining.
Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
15 And he went away thence, and met Yehonadab the son of Rechab coming to meet him: and he saluted him, and said to him, Is all right in thy heart, as my heart is with thy heart? And Yehonadab answered, It is; it is: give me thy hand. And he gave him his hand; and he took him up to him into the chariot.
Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
16 And he said, Come with me, and behold my zeal for the Lord. So they made him ride in his chariot.
Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
17 And when he came to Samaria, he smote all that yet remained unto Achab in Samaria, till he had exterminated him, according to the word of the Lord which he had spoken to Elijah.
Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
18 And Jehu assembled all the people, and said unto them, Achab hath served Ba'al a little: Jehu will serve him much.
Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
19 And now call unto me all the prophets of Ba'al, all his worshippers, and all his priests: let no one be missing; for I have a great sacrifice to make for Ba'al; whosoever will be missing, shall not live. But Jehu did it in subtilty, in order to destroy the worshippers of Ba'al.
Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
20 And Jehu said, Sanctify a solemn assembly for Ba'al. And they proclaimed it.
Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
21 And Jehu sent throughout all Israel: and there came all the worshippers of Ba'al, so that there was not a man remaining that came not; and they came into the house of Ba'al; and the house of Ba'al was full from one end to another.
Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
22 And he said unto him that was over the wardrobe, Bring forth vestments for all the worshippers of Ba'al. And he brought forth for them the vestments.
Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
23 And Jehu went, with Yehonadab the son of Rechab, into the house of Ba'al, and he said unto the worshippers of Ba'al, Search, and look that there be not here with you any of the servants of the Lord, but the worshippers of Ba'al entirely alone.
Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
24 And they went in to prepare sacrifices and burnt-offerings; but Jehu had set for himself without eighty men, and said, [If there be] a man that escapeth from the men whom I deliver into your hands, [there shall be given] life for his life.
Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
25 And it came to pass, as soon as they had made an end of preparing the burnt-offering, that Jehu said to the runners and to the officers, Go in, smite them: let none come forth. And they smote them with the edge of the sword; and the runners and the captains cast them out, and went as far as the city of the house of Ba'al.
Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
26 And they brought forth the statues out of the house of Ba'al, and burnt every one of them.
Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
27 And they broke down the statue of Ba'al, and broke down the house of Ba'al, and made it a common sewer unto this day.
Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
28 Thus Jehu exterminated Ba'al out of Israel.
Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
29 Nevertheless the sins of Jerobo'am the son of Nebat, who induced Israel to sin, Jehu departed not from in following them, [namely, ] the golden calves that were in Beth-el, and that were in Dan.
Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
30 And the Lord said unto Jehu, Forasmuch as thou hast acted well in doing what is right in my eyes, and hast done in accordance with all that was in my heart unto the house of Achab: children of the fourth generation after thee shall sit upon the throne of Israel.
Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
31 But Jehu took no heed to walk in the law of the Lord the God of Israel with all his heart: he departed not from the sins of Jerobo'am, who induced Israel to sin.
Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
32 In those days the Lord began to cut Israel short; and Chazael smote them in all the boundary of Israel;
Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
33 From the Jordan to the rising of the sun, all the land of Gil'ad, the Gadites, and the Reubenites, and the Menassites, from 'Aro'er which is by the river Arnon, both Gil'ad and Bashan.
mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
34 Now the rest of the acts of Jehu, and all that he did, and all his mighty deeds, behold, they are written in the book of the chronicles of the kings of Israel.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
35 And Jehu slept with his fathers, and they buried him in Samaria. And Jehoachaz his son became king in his stead.
Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
36 And the time that Jehu reigned over Israel in Samaria was twenty and eight years.
Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.

< 2 Kings 10 >