< 2 Chronicles 19 >

1 And Jehoshaphat the king of Judah returned to his house in peace, to Jerusalem.
Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
2 And there came out to meet him Jehu the son of Chanani the seer, and said to king Jehoshaphat, Shouldst thou help the wicked, and love those that hate the Lord? and because of this there is wrath over thee from before the Lord.
Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
3 Nevertheless there are good things found on thee; because thou hast removed the Asheroth out of the land, and hast directed thy heart firmly to seek God.
Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
4 And Jehoshaphat remained at Jerusalem; but he went out again through the people from Beer-sheba' as far as the mountain of Ephraim, and caused them to return unto the Lord the God of their fathers.
Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
5 And he appointed judges in the land in all the fortified cities of Judah, in city by city.
Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
6 And he said to the judges, Look [well] at what ye are doing; because not for man are ye to judge, but for the Lord, who is with you in pronouncing judgment.
Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
7 And now let the dread of the Lord be upon you: take heed and act; for with the Lord our God there is no injustice, nor respect for persons, nor taking of bribes.
Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
8 But also in Jerusalem did Jehoshaphat appoint some of the Levites, and the priests, and of the chiefs of the family divisions of Israel, for the [giving of] the judgment of the Lord, and for controversies, when they returned to Jerusalem.
Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
9 And he charged on them, saying, Thus shall ye do in the fear of the Lord, in faithfulness, and with an undivided heart.
Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
10 And whatsoever controversy may come to you from your brethren that dwell in their cities, between blood and blood, between law and commandment, statutes and ordinances, ye shall truly warn them that they incur not guilt against the Lord, and so there come wrath over you, and over your brethren: so must ye do, and ye will not incur guilt.
Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
11 And, behold, Amaryahu the chief priest is over you for every matter of the Lord; and Zebadyahu the son of Yishma'el, the ruler for the house of Judah, for every matter of the king; and the Levites are officers before you. Be strong and act, and may the Lord be with the good.
“Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”

< 2 Chronicles 19 >