< 1 Samuel 9 >
1 Now there was a man of Benjamin, whose name was Kish, the son of Abiel, the son of Zeror, the son of Bechorath, the son of Aphiach, the son of a Benjamite, a mighty man of valor.
Basi kulikuwa na mtu mmoja kutoka Benyamini, mtu mashuhuri. Jina lake aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Zerori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, mwana wa Mbenyamini.
2 And he had a son whose name was Saul, young and handsome; and there was not a man among the children of Israel handsomer than he: from his shoulders and upward he was taller than any of the people.
Huyu alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Sauli, kijana mzuri wa uso. Hapakuwapo mwanaume mzuri wa uso kuliko huyu miongoni mwa watu wote wa Israeli. Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine.
3 And there were lost the asses belonging to Kish, Saul's father; and Kish said to Saul his son, Do take with thee one of the servants, and arise, go seek the asses.
Na punda wa Kishi, baba yake na Sauli walipotea. hivyo Kishi akamwambia Sauli mwanawe, “Mchukue mmoja wa watumishi; uamke uende kuwatafuta punda,”
4 And he passed through the mountain of Ephraim, and passed through the land of Shalisha, but they found [them] not; then they passed through the land of Sha'alim, and there was nothing there; and he passed through the land of Benjamin, but they found them not.
Sauli akapita katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu na akaenda akapita katika nchi ya Shalisha, lakini hawakuwaona. Kisha walipita katika nchi ya Shaalimu, lakini hawakuwa huko. Baadaye alipita katika nchi ya Wabenyamini, lakini hawakuwaona wale punda.
5 When they were come in the land of Zuph, Saul said to his servant that was with him, Come, and let us return; lest my father relinquish the care for the asses, and become anxious for us.
Na walipofika nchi ya Sufu, Sauli alimwambia mtumishi wake aliyekuwa naye, “Njoo na turudi, pengine baba aweza kuacha kuchunga punda na kuanza kutuhofia sisi.”
6 And the other said unto him, Behold now, a man of God is in this city, and the man is honored; all that he ever saith will surely come to pass: now let us go thither; perhaps he can tell us our way that we should go.
Lakini mtumishi akamwmbia, “Sikiliza, Yupo mtu wa Mungu katika mji huu. Naye ni mtu wa kuheshimiwa sana; kila asemalo huwa kweli. Hebu twende huko; labda anaweza kutuambia tupitie wapi katika safari yetu.”
7 Then said Saul to his servant, But, behold, if we should go, what shall we bring to the man? for the bread is spent out of our vessels, and there is not a present to bring to the man of God: what have we with us?
Ndipo Sauli akamwambia mtumish iwake, “Lakini kama tukienda kwake, twaweza kumpelekea nini? Maana hata mkate katika mfuko wetu umekwisha, na hakuna zawadi ya kumpelekea mtumishi wa Mungu. Tuna kitu gani?
8 And the servant answered Saul again, and said, Behold, I have here in my hand the fourth part of a shekel of silver; and I will give this to the man of God, that he may tell us our way.
Huyo mtumishi akamjibu Sauli na kusema, “Hapa, ninayo robo ya shekeli ya fedha ambayo nitampa mtumishi wa Mungu, atuambie ni njia ipi yatupasa tuiendee.”
9 In former times it was custom in Israel, that when a man went to inquire of God, he said thus, Come, and let us go as far as the seer; for the Prophet of the present day was in former times called a Seer.
(Zamani katika Israeli, mtu alipotaka kujua neno kuhusu mapenzi ya Mungu, alisema, “Njoo, haya twende kwa mwonaji.” Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji).
10 Then said Saul to his servant, Thy word is good: come, let us go. So they went unto the city where the man of God was.
Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake, “Umesema vyema. Haya, njoo twende.” Basi wakaenda katika mji ambao mtu wa Mungu alikuwamo.
11 As they went up the ascent to the city, they found some maidens going out to draw water; and they said unto them, Is the seer here?
Walipopanda mlima kuelekea mjini, walikutana na wasichana wakienda kuteka maji; Sauli na mtumishi wake wakawauliza, “Mwonaji hupo hapa?”
12 And they answered them, and said, He is; behold, he is before you: make haste now, for this day came he to the city; because the people have a sacrifice today on the high-place;
Nao wakawajibu, na kusema, “Yupo; tazameni, yuko mbele yenu. Harakisheni, kwa maana anakuja mjini leo, sababu leo watu wanatoa dhabihu zao mahali pa juu.
13 As soon as ye are come into the city, ye will straightway find him, before yet he can go up to the high-place to eat; for the people will not eat until he be come, because he always blesseth the sacrifice; afterward eat those that are invited; and now go you up; for just today will ye surely find him.
Mara tu mtakapoingia mjini mtamuona, kabla hajapanda mahali pa juu kla chakula. Watu hawatakula hata atakapokuja, kwa sababu ndiye ataibariki dhabihu; na baadaye wale ambao wamealikwa hula. Basi pandeni, mtamuona sasa hivi.”
14 And they went up into the city. They were entering into the city, when, behold, Samuel came out toward them, to go up to the high-place.
Kwa hiyo walikwea kwenda mjini. Walipokuwa wakiingia mjini, walimuona Samweli akija mbele yao, akipanda kwenda mahali pa juu.
15 And the Lord had revealed to Samuel's ear one day before Saul's coming, saying,
Siku moja kabla Sauli hajafika, BWANA alikuwa amemfunulia Samweli:
16 About this time tomorrow will I send unto thee a man out of the land of Benjamin, and thou shalt anoint him as chief over my people Israel, that he may save my people out of the hand of the Philistines; for I have beheld my people, because their cry is come unto me.
“Kesho wakati kama huu nitakutumia mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe utamtia mafuta awe mfalme juu ya watu wangu Israeli. Atawaokoa watu wangu kutoka mkono wa Wafilisti. Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu na kilio cha kutaka msaada kimenifikia.”
17 And when Samuel saw Saul, the Lord addressed him, Behold, the man of whom I spoke to thee, This one shall rule over my people.
Samweli alipomuona Sauli, BWANA akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekwambia habari zake! Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
18 And Saul drew near to Samuel within the gate, and said, Tell me, I pray thee, where is the house of the seer.
Ndipo Sauli akaja karibu na Samweli katika lango na kusema, “Niambie nyumba ya Mwonaji iko wapi?
19 And Samuel answered Saul, and said, I am the seer: go up before me unto the high-place, and ye shall eat with me today; and I will let thee go in the morning, and all that is in thy heart will I tell thee.
Samweli akamjibu Sauli akisema, “Mimi ndiye mwonaji. Tangulia mbele hadi mahali pa juu, nami nitakueleza kila kitu kilichomoyoni mwako.
20 And as for thy asses that were lost unto thee this day three days ago, do not set thy heart on them; for they have been found. And to whom belongeth all that is desirable in Israel? Is it not to thee, and to all thy father's house?
Kama punda wenu waliopotea siku tatu zilizopita, msihofu kuhusu hao punda, kwa kuwa wamekwishapatikana. Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?”
21 And Saul answered and said, Am not I a son of Benjamin, of one of the smallest tribes of Israel? and [is not] my family the least of all the families of the tribes of Benjamin? wherefore then hast thou spoken to me such thing?
Sauli akamjibu na kusema, Siyo mimi Mbenyamini, kutoka kabila lililo dogo sana kwa makabila ya Israeli? Siyo ukoo wangu ulio mdogo sana kwa kabila la Benyamini? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?”
22 And Samuel took Saul and his servant, and brought them into the apartment; and he assigned them a place at the head of the invited guests, who were about thirty persons.
Hivyo Samweli akamchukua Sauli na mtumishi wake, akawaingiza ukumbini, akawakalisha mahali pa heshima pa wale walioalikwa, idadi yao takribani watu thelathini.
23 And Samuel said unto the cook, Hand here the portion which I gave thee, of which I said unto thee, Put it away by thee.
Samweli akamwambia mpishi, “Lete sehemu niliyokupatia, sehemu ambayo nilikwambia hivi, “Itenge.”'
24 And the cook took up the shoulder, and that which was on it, and set it before Saul; and he said, Behold what is left! set it before thee, and eat; for unto this time hath it been kept from thee, since I said, I have invited the people. And Saul ate with Samuel on that day.
Basi mpishi alichukua paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu na kile kilichokuwa pamoja nalo, akaitenga mbele ya Sauli. Kisha Samweli akasema, “Angalia kile kilichokuwa kimetunzwa kwa ajili yako! Kula, kwa sababu kilitunzwa hadi wakati maalum ufike kwa ajili yako. Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.”' Kwa hiyo Sauli alikula pamoja na Samweli siku hiyo.
25 And they went down from the high-place into the city, and he spoke with Saul upon the roof.
Walipokuwa wamekwisha shuka chini kutoka sehemu ya juu na kuingia mjini, Samweli akazungumza na Sauli darini.
26 And they got up early; and it came to pass when the morning-dawn arose, that Samuel called Saul to the roof, saying, Up, that I may send thee away. And Saul arose, and they went out, both of them, he and Samuel, into the street.
Na kulipopambazuka, Samweli alimwita Sauli darini na kusema, “Amka, kusudi nikusindikize uende zako,” Hivyo Sauli aliamka, na wote wawili, yeye na Samweli walitoka kwenda mtaani.
27 As they were going down to the end of the city, Samuel said to Saul, Say to the servant that he pass on before us, —and he passed on, —but thou remain standing a while, and I will let thee hear the word of God.
Walipokuwa wakienda nje ya viunga vya mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi wako atanguliye mbele yetu(na alitangulia mbele), Lakini wewe sharti usubiri kidogo, nipate kukuambia ujumbe wa Mungu.”