< 1 Kings 8 >

1 Then did Solomon assemble the elders of Israel, and all the heads of the tribes, the princes of the divisions of the children of Israel, unto king Solomon in Jerusalem, to bring up the ark of the covenant of the Lord out of the city of David, which is Zion.
Kisha Sulemani akawakusanya wazee wa Israeli, wakuu wote wa makabila, na viongozi wa familia za wana wa Israeli, mbele yake kuleYerusalemu, ili waliingize ndani lile sanduku la agano la BWANA kutoka mji wa Daudi, ambao ni Sayuni.
2 And all the men of Israel assembled themselves unto king Solomon at the feast in the month Ethanim, which is the seventh month.
Wanaume wote wa Israeli walikusanyika mbele ya mfalme Sulemani kwenye sherehe, katika mwezi wa Ethanim, ambao ndio mwezi wa saba.
3 And all the elders of Israel came, and the priests took up the ark.
Wazee wote wa Israeli walikuja, na makuhani wakalibeba lile sanduku.
4 And they brought up the ark of the Lord, and the tabernacle of the congregation, and all the holy vessels that were in the tabernacle: even these did the priests and the Levites bring up.
Wakalileta lile sanduku la BWANA, lIle hema la kukutania na mapambo yote matakatifu ambayo yalikuwa kwenye hema. Makuhani na Walawi wakavileta vitu hivi.
5 And king Solomon, and all the congregation of Israel, that were assembled unto him, were with him before the ark, sacrificing sheep and oxen, that could not be told nor numbered for multitude.
Mfame Sulemani na mkutano wote wa Israeli wakaja pamoja mbele ya sanduku, wakatoa sadaka za kondoo na makisai ambazo hazikuweza kuhasabika.
6 And the priests brought in the ark of the covenant of the Lord unto its place, into the debir of the house, into the most holy place, under the wings of the cherubim.
Makuhani wakalingiza ndani lile sanduku la agano la BWANA na wakaliweka mahali pake, ndani ya chumba cha ndani, patakatifu sana, chini ya yale mabawa ya makerubi.
7 For the cherubim spread forth their wings over the place of the ark, and the cherubim covered the ark and its staves from above.
Kwa kuwa makerubi walitandaza mabawa yao hadi mahali pa sanduku la agano, na walifunika sanduku na miti yake kwani ilitumika kulibeba.
8 And they had made the staves so long, that the ends of the staves were seen out in the holy place in the front of the debir, but they were not seen without; and they have remained there until this day.
Ile miti ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba miishio yake ilionekana tokea kwenye eneo takatifu mbele ya chumba cha ndani, lakini haikuweza kuonekana kutokea nje. Miti hiyo iko mpaka leo.
9 There was nothing in the ark save the two tables of stone, which Moses had placed therein at Horeb, where the Lord made a covenant with the children of Israel, when they came out of the land of Egypt.
Ndani ya sanduku hapakuwemo na kitu chochote isipokuwa vile vidonge vya mawe ambavyo Musa aliviweka alipokuwa mlima Horebu, wakati BWANA alipofanya agano na watu wa Israeli walipotoka kwenye nchi ya Misri.
10 And it came to pass, when the priests were come out of the holy place, that the cloud filled the house of the Lord:
Ilitokea kwamba wakati makuhani walipotoka mahali patakatifu, lile wingu lilifunika hekalu la BWANA.
11 And the priests were not able to stand to minister because of the cloud; for the glory of the Lord had filled the house of the Lord.
Makuhani hawakuweza kusimama kwa ajili ya kutumika kwa sababu utukufu wa BWANA ulifunika hekalu.
12 Then said Solomon, The Lord said that he would dwell in the thick darkness.
Kisha Sulemani akasema, “BWANA amsema kuwa anaweza kuishi hata kwenye giza nene,
13 I have indeed built a dwelling-house for thee, a settled place for thy abode for ever.
Lakinni nimekujengea makao ya kujivunia, mahali pako pa kuishi milele.”
14 And the king turned his face about, and blessed all the congregation of Israel; and all the congregation of Israel was standing;
Kisha mfalme akageuka na kuwabariki mkusanyiko wa watu wa Israeli, wakati huo mkusanyiko wa Waisraeli walikuwa wamesimama.
15 And he said, Blessed be the Lord, the God of Israel, who spoke with his mouth unto David my father, and hath with his hand fulfilled it, when he said,
Akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, asifiwe, ambaye alisema na baba yangu Daudi, na ametimiza kwa mikono yake, akisema,
16 Since the day that I brought forth my people Israel out of Egypt, I did not make choice of any city out of all the tribes of Israel to build a house, that my name might be therein; but I made choice of David to be over my people Israel.
'Tangu siku ile niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji wowote toka kwa makabila yote ya Israeli ambako ningeijenga nyumba, kwa ajili ya jina langu kuwemo humo. Hata hivyo, nilimchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.
17 And it was in the heart of David my father to build a house for the name of the Lord, the God of Israel.
Sasa ilikuwa kwenye moyo wa Daudi baba yangu kujenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wa Israeli.
18 But the Lord said unto David my father, Whereas it was in thy heart to build a house unto my name, thou didst well that it was in thy heart:
Lakini BWANA alimwambia baba yangu Daudi, 'Ilikuwa ndani ya moyo wako kunijengea nyumba kwa jina langu, ulifanya vyema kwa hilo kuwa ndani ya moyo wako.
19 Nevertheless, thou shalt not thyself build the house; but thy son that shall come forth out of thy loins, he shall build the house unto my name.
Ingawa hutanijengea nyumba; badala yake mwanao, mmoja wa wanao atakayezaliwa toka viunoni mwako, atanijengea nyumba kwa jina langu,'
20 And the Lord hath fulfilled his word that he hath spoken: and I am risen up in the room of David my father, and I sit on the throne of Israel, as the Lord hath spoken, and I have built the house for the name of the Lord the God of Israel.
BWANA amelibeba lile neno slilokuwa amesema, kwa kuwa nimeinuka mahali pa baba yangu Daudi, na nimeketi kwenye kiti cha enzi cha Israeli, kama BWANA alivyoahidi. Nimeijenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wa Israeli.
21 And I have assigned there a place for the ark, wherein is the covenant of the Lord, which he made with our fathers, when he brought them forth out of the land of Egypt.
Nimetengeneza mahali kwa ajili ya sanduku ndani yake, ambamo ndani yake kuna agano la BWANA, ambalo alifanya na baba zetu alipowatoa toka nchi ya Misri,”
22 And Solomon now placed himself before the altar of the Lord in the presence of all the congregation of Israel, and spread forth his hands toward heaven;
Sulemani alisimama mbele ya madhabahu ya BWANA, mbela ya mkusanyiko wote wa Waisraeli, naye akanyosha mikono yake kuelekea mbinguni.
23 And he said, O Lord, the God of Israel, there is no god like thee, in the heavens above, and on the earth beneath, thou who keepest the covenant and the kindness for thy servants that walk before thee with all their heart;
Akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni au chini duniani, ambaye hutunza agano lake kwa uaminifu kwa watumishi wako ambao hutembea mbele yako kwa mioyo yao yote;
24 Who hast kept for thy servant David my father what thou hadst promised him; and thou spokest with thy mouth, and hast fulfilled it with thy hand, as it is this day.
wewe ambaye umetunza ahadi yako na mtumishi wako Daudi baba yangu ile uliyomwahidi. Naam, ulisema kwa kinywa chako na sasa umeitimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
25 And now, O Lord, the God of Israel, keep for thy servant David my father what thou hast spoken concerning him, saying, There shall never fail thee a man in my sight who sitteth on the throne of Israel; if thy children but take heed to their way to walk before me, as thou hast walked before me.
Sasa basi, BWANA, Mungu wa Israeli, timiza kile ulichomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu, pale uliposema, 'Hautashindwa kunipa mtu mbele ya macho yangu ambaye ataketi katika kiti cha enzi cha Israeli, kama tu uzao wako watakuwa waangalifu kutembea mbele yangu, kama vile wewe ulivyotembea mbele yangu.'
26 And now, O God of Israel, I pray thee, let thy word be verified, which thou hast spoken unto thy servant David my father.
Sasa basi, Mungu wa Israeli, Ninaomba kwamba ile ahadi uliyofanya kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, itimie.
27 For in truth will God then dwell on the earth? behold, the heavens and the heavens of heavens cannot contain thee: how much less then this house that I have built!
Je, ni kweli kwamba Mungu ataishi duniani? Tazama, Ulimwengu wote na mbingu hazikutoshi - sembuse nyumba hii niliyoijenga!
28 Yet wilt thou turn thy regard unto the prayer of thy servant, and to his supplication, O Lord my God, to listen unto the entreaty and unto the prayer, which thy servant prayeth before thee today;
Kwa hiyo Mungu naomba uyajali maombi haya ya mtumishi wako na maombi yake, BWANA, Mungu wangu; sikiliza kilio na maombi ambayo mtumishi wako anakuomba leo.
29 That thy eyes may be open toward this house night and day, toward the place of which thou hast said, My name shall be there; that thou mayest listen unto the prayer which thy servant shall pray at this place.
Naomba ulitazame hekalu hili mchana na usiku, mahali ambapo ulisema, 'Jina langu na uwepo wangu utakuwa' - ili niweze kuwa nasikiliza maombi ambayo mtumishi wako ataomba mahali hapa.
30 And listen thou to the supplication of thy servant, and of thy people Israel, which they will pray at this place: and oh, do thou hear in heaven thy dwelling-place; and hear, and forgive.
Kwa hiyo sikia maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli tunapokuwa tunaomba mahali hapa. Ndiyo, sikia kutokea mahali ambapo unaishi, kutoka katika mbingu za mbingu; na unaposikia tafadhali samehe.
31 If any man trespass against his neighbor, and an oath be laid upon him to cause him to swear, and the oath come before thy altar in this house:
Kama mtu atamtendea uovu jirani yake na anapewa sharti la kiapo, na kama atakuja na kuapa mbele ya madhabahu yako katika nyumba hii,
32 Then do thou hear in heaven, and act, and judge thy servants, by condemning the wicked, to bring his way upon his head; and by justifying the righteous, to give him according to his righteousness.
basi usikie kutoka mbinguni ukatende na kuwahukumu watumishi wako, ukamhukumu mwovu, ili kuwaletea tabia zake kichwani mwake, na kumtunza mwenye haki kuwa hana hatia, na kumpa thawabu yake ya haki.
33 When thy people Israel are struck down before the enemy, because they have sinned against thee, and they return then to thee, and confess thy name, and pray, and make supplication unto thee in this house:
Watu wako Israeli watakapopigwa na adui kwa sabau ya kutenda dhambi dhidi yako, na kama watakurudia, na kulikiri jina lako, na kukusihi, na kuomba msamaha kwako katika hekalu hili-
34 Then do thou hear in heaven, and forgive the sin of thy people Israel, and cause them to return unto the land which thou hast given unto their fathers.
tafadhali nakuomba usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi za watu wako Israeli; uwarudishe katika nchi ambayo uliwapa mababu zao.
35 When the heavens be shut up, and there be no rain, because they have sinned against thee, and they pray toward this place, and confess thy name, and turn from their sin, because thou hast afflicted them:
Kama mbingu zitafungwa na mvua hazinyeshi kwa sababu watu wamekutenda dhambi wewe - na kama wataomba mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kugeuka toka dhambi zao na kama umewapiga -
36 Then do thou hear in heaven, and forgive the sin of thy servants, and of thy people Israel; for thou wilt teach them the good way wherein they should walk; and give then rain upon thy land, which thou hast given to thy people for an inheritance.
basi sikia tokea mbinguni na usamehe dhambi za watumishi wako na za watu wako Israeli, utakapowafundisha njia njema inayowapasa; basi uinyeshee mvua nchi yako, ambayo uliwapa watu wako kuwa urithi.
37 If there be a famine in the land, if there be pestilence, blasting, mildew, or if there be locust, caterpillar, if their enemy besiege them in the land of their gates; at whatsoever plague, whatsoever sickness;
Na kama kuna njaa katika nchi, au kama kuna magonjwa, au ukungu, nzige au funza; au kama adui atavamia malango ya mji katika nchi yao, kama kuna tauni au magonjwa yeyote -
38 What prayer and supplication soever be made by any man, of all thy people Israel, when they shall be conscious every man of the plague of his own heart, and he then spread forth his hands toward this house:
na kama kuna mtu au wata wa Israeli wataomba - kila mmoja akaijua hiyo tauni katika moyo wake wakati akinyosha mikono yake katika hekalu hili.
39 Then do thou hear in heaven the place of thy dwelling, and forgive, and act, and give to every man in accordance with all his ways, as thou mayest know his heart; for thou, thyself alone, knowest the heart of all the children of men;
Basi usikie kutoka mbinguni, mahali unapoishi, utende na kusamehe, na umpe kila mtu thawabu anayostahili kwa kile anachofanya; wewe unajua moyo wake, kwa sababu ni wewe pekee yako ujuaye mioyo ya watu.
40 In order that they may fear thee all the days that they live on the face of the land which thou hast given unto our fathers.
Fanya hivi ili kwamba wawe na hofu kwako katika siku zote za maisha yao wanayoishi katika nchi uliyowapa mababu zetu.
41 But also to the stranger, who is not of thy people Israel, but cometh out of a far-off country for the sake of thy name;
Na nyongeza yake, kuhusiana na mgeni ambaye si mtu wako wa Israeli: atakapokuja kutokea nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako -
42 For they will hear of thy great name, and of thy strong hand, and of thy outstretched arm; when he will come and pray at this house:
kwa sababu watasikia jina lako lilivyo kuu, mkono wako wenye nguvu, na mkono wako ulioinuliwa - atakapokuja na kuomba mahali hapa pa hekalu,
43 Mayest thou listen in heaven the place of thy dwelling, and do according to all that the stranger will call on thee for; in order that all the nations of the earth may know thy name, to fear thee, as [do] thy people Israel; and that they may understand that this house, which I have built, is called by thy name.
tafadhali usikie kutokea katika mbingu, mahali unapoishi, na umfanyie huyo mgeni akuombacho. Fanya hivi ili makundi ya wtu wote duniani wakujue jina lako na kukuhofia, kama wanavyofanya watu Israeli. Fanya hivyo ili wajue kwamba nyumba hii niliyoijenga inaitwa kwa jina lako.
44 If thy people go out to battle against their enemy, on the way on which thou mayest send them, and they do pray unto the Lord in the direction of the city which thou hast chosen, and of the house that I have built for thy name:
Na kama watu wko wataenda vitani dhidi ya adui, kwa njia yeyote unayoweza kuwatuma, na kama watakuomba wewe, BWANA, kuelekea mji huu uliuchagua, na kuekea nyumba ambayo nimeijenga kwa jina lako.
45 Then hear thou in heaven their prayer and their supplication, and procure them justice.
Basi sikia tokea mbinguni maombi yao, dua zao, na uwasaidie wanachohitaji.
46 If they sin against thee, [for there is no man that may not sin, ] and thou be angry with them, and give them up before the enemy, so that their captors carry them away captive unto the land of the enemy, [be it] far or near;
Na kama watafanya dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna hata mtu mmoja asiyefanya dhambi, na kama una hasira dhidi yao na kuwapeleka kwa maadui, ili kwamba maadui wawachukue mateka katika nchi yao, mbali au karibu.
47 And if they then take it to their heart in the land whither they have been carried captive, and repent, and make supplication unto thee in the land of their captors, saying, We have sinned, and have committed iniquity, we have acted wickedly;
Na kama watatambua kuwa wako katika nchi ya utumwa, na kama watatubu na kuomba neema kwako kutokea katika nchi ya watekaji. Na kama watasema, 'tumetenda kwa ukaidi na tumefanya dhambi. Tumetenda kwa uovu.'
48 And they return unto thee with all their heart, and with all their soul, in the land of their enemies, who have led them away captive, and they pray unto thee in the direction of their land, which thou hast given unto their fathers, of the city which thou hast chosen, and of the house which I have built for thy name:
Na kama watarudi kwako kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote katika chi ya maadui ambao wanawakamata, na kama watakuomba wewe kuelekea nchi yao, ambayo uliwapa mababu zao, na kuelekea katika mji uliouchagua, nakuelekea kaika nyumba ambayo nimeijenga kwa jina lako.
49 Then hear thou in heaven the place of thy dwelling their prayer and their supplication, and procure them justice;
Basi usikie maombi yao, na dua zao tokea mbinguni, mahali unapoishi, na ukaitetee haki yao.
50 And forgive thy people for what they have sinned against thee, and all their transgressions whereby they have transgressed against thee, and cause them to find mercy before their captors, that they may have mercy on them;
Wasamehe watu wako waliotenda dhambi dhidi yako, na dhambi zao zote ambazo kwazo wamekukosea wewe dhidi ya amri zako. Uwahurumie mbele ya maadui zao ambao waliwachukua mateka, ili kwamba maadui zao pia wawahurumie watu wako.
51 For they are thy people, and thy heritage, whom thou hast brought forth out of Egypt, from the midst of the iron furnace;
Hawa ni watu wako uliowachagau, ambao uliwaokoa toka nchi ya Misri kama kwamba walikuwa katikati ya tanuru amabamo vyuma huyeyushwa.
52 That thy eyes may be open unto the supplication of thy servant, and unto the supplication of thy people Israel, to listen unto them in all for which they call unto thee;
Naomba kwamba macho yako yatazame dua za mtumishi wako na kwa dua za watu wako Issraeli, ili uwasike kila wanapokulilia.
53 For thou hast separated them unto thee as a heritage from all the people of the earth, as thou spokest by the hand of Moses thy servant, when thou broughtest forth our fathers out of Egypt, O Lord Eternal.
Kwa kuwa uliwatenga toka kwa watu wengine wa duniani ili wawe wako nakupokea ahadi zako, kama vile ulivyomwambia Musa mtumishi wako, wakati ulipowatoa babazetu toka Misri, BWANA.”
54 And it happened, that, when Solomon had made an end of praying all this prayer and supplication unto the Lord, he arose from before the altar of the Lord from kneeling on his knees, with his hands spread out toward heaven.
Kwa hiyo ilitokea wakati Sulemaeni alipomaliza kuomba maombi haya na dua zake kwa BWANA, aliamka toka madhabahu ya BWANA, pale alipokuwa amepiga magoti na mikono yake ikiwa imenyoshwa kuelekea mbinguni.
55 And he stood up, and blessed all the congregation of Israel with a loud voice, saying,
Alisimama na kuubariki mkutano wote wa Israeli kwa sauti kuu, alisema,
56 Blessed be the Lord, who hath given rest unto his people Israel, in accordance with all that he hath spoken: [so that] there hath not failed one word of all his good promise, which he spoke by the hand of Moses his servant.
“Asifiwe BWANA, aliywapatia pumziko watu hawa Israeli, akitunza ahadi zake zote. Hakuna hata moja ambayo haijatekelezwa katika ahadi njema za BWANA ambazo aliahidi akiwa na Musa mtumishi wake.
57 The Lord our God be with us, as he was with our fathers; oh may he not leave us, nor forsake us;
BWANA, mungu wetu awe pamoja nasi, kama alivyokuwa pamoja na mababu zetu. Asituache wala kututelekeza,
58 That he may incline our heart unto him, to walk in all his ways, and to keep his commandments, and his statutes, and his ordinances, which he commanded our fathers.
kwamba aunganishe mioyo yetu na yeye, ili tuishi katika njia zake na kuzishika amri zake na taratibu zake na maagizo yake, ambayo aliwaagiza baba zetu.
59 And may these my words, wherewith I have made supplication before the Lord, be nigh unto the Lord our God day and night, that he may maintain the cause of his servant, and the cause of his people Israel in their daily requirements;
Na maeneo haya ambayo nimesema, ambayo nimesihi mbele ya BWANA, yawe karibu n a BWANA, Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba awasadie katika haki za mtumishi wake na haki za watu wake Israeli, kama watakavyoomba kila siku;
60 In order that all the nations of the earth may know that the Lord is the [true] God, and none else.
kwamba watu wote duniani wajue kwamba BWANA, ndiye Mungu, na hakuna Mungu mwingine!
61 Let your heart therefore be entire with the Lord our God, to walk in his statutes, and to keep his commandments, as at this day.
Kwa hiyo ifanyeni mioyo yenu iwe ya haki mbele ya BWANA. Mungu wetu, ili tutembee katika maagizo na kuzishika amri zake, kama ilivyo leo.
62 And the king, and all Israel with him, offered sacrifices before the Lord.
Kwa hiyo mfalme na watu wote pamoja naye wakatoa sadaka kwa BWANA.
63 And Solomon offered [as] the sacrifice of peace-offering which he offered unto the Lord, two and twenty thousand oxen, and a hundred and twenty thousand sheep. And thus did the king and all the children of Israel dedicate the house of the Lord.
Sulemani akatoa sadaka ya amani, ambayo aliifanya kwa BWANA: Nayo ilikuwa makisai elfu ishirini na mbili, na kondoo 120, 000. Kwa hiyo mfalme na watu wa Israeli wakaiweka wakfu nyumba ya BWANA.
64 On the same day did the king hallow the interior of the court that was before the house of the Lord; for he prepared there the burnt-offerings, and the meat-offerings, and the fat of the peace-offerings; because the copper altar that was before the Lord was too small to contain the burnt-offerings, and the meat-offerings, and the fat of the peace-offerings.
Siku hiyo mfalme aliweka wakfu behewa ya katikati mbele ya hekalu la BWANA, kwa kuwa pale ndipo alipotoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga, na sadaka za mafuta ya amani, kwa sababu ile madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele ya BWANA ilikuwa ndogo sana kwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga, na mafuta ya sadaka za amani.
65 And Solomon held at that time the feast, and all Israel with him, a great assembly, from the entrance of Chamath unto the river of Egypt, before the Lord our God, seven days and seven days, even fourteen days.
Kwa hiyo Sulemani akafanya sherehe wakati huo, Nayo Israeli yote pamoja naye, mkutano mkubwa, kutoka Lebo Hamathi hadi kijito cha Misri, wakaja mbele ya BWANA, Mungu wetu kwa muda wa siku saba na pia kwa siku saba zingine, ambayo jumla yake ni siku kumi na nne.
66 On the eighth day he dismissed the people, and they blessed the king; and they went unto their tents joyful and glad of heart, because of all the good that the Lord had done for David his servant, and for Israel his people.
Na ilipofika siku ya nane aliwatawanya watu, nao wakambariki mfalme kisha wakaenda nyumbani kwao kwa furaha na mioyo ya shangwe kwa wema wote ambao BWANA alimwonyesha Daudi, mtumishi wake, na kwa watu wake, Israeli.

< 1 Kings 8 >