< Psalms 86 >

1 A Prayer of David. O Lord, incline your ear, and listen to me; for I am poor and needy.
Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
2 Preserve my soul, for I am holy; save your servant, O God, who hopes in you.
Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
3 Pity me, O Lord: for to you will I cry all the day.
Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
4 Rejoice the sold of your servant: for to you, O Lord, have I lifted up my soul.
Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
5 For you, O Lord, are kind, and gentle; and plenteous in mercy to all that call upon you.
Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
6 Give ear to my prayer, o Lord; and attend to the voice of my supplication.
Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
7 In the day of my trouble I cried to you: for you did hear me.
Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
8 There is none like to you, O Lord, among the god; and there are no [works] like to your works.
Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
9 All nations whom you have made shall come, and shall worship before you, O Lord; and shall glorify your name.
Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
10 For you are great, and do wonders: you are the only [and] the great God.
Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
11 Guide me, O Lord, in your way, and I will walk in your truth: let my heart rejoice, that I may fear your name.
Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
12 I will give you thanks, O Lord my God, with all my heart; and I will glorify your name for ever.
Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
13 For your mercy is great toward me; and you have delivered my soul from the lowest hell. (Sheol h7585)
Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol h7585)
14 O God, transgressors have risen up against me, and an assembly of violent [men] have sought my life; and have not set you before them.
Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
15 But you, O Lord God, are compassionate and merciful, longsuffering, and abundant in mercy and true.
Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
16 Look you upon me, and have mercy upon me: give your strength to your servant, and save the son of your handmaid.
Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
17 Establish with me a token for good; and let them that hate me see [it] and be ashamed; because you, O Lord, have helped me, and comforted me.
Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.

< Psalms 86 >