< Psalms 56 >

1 For the end, concerning the people that were removed from the sanctuary, by David for a memorial, when the Philistines caught him in Geth. Have mercy upon me, O God; for man has trodden me down; all the day long he warring has afflicted me.
Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
2 Mine enemies have trodden me down all the day from the dawning of the day; for there are many warring against me.
Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
3 They shall be afraid, but I will trust in you.
Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
4 In God I will praise my words; all the day have I hoped in God; I will not fear what flesh shall do to me.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
5 All the day long they have abominated my words; all their devices [are] against me for evil.
Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
6 They will dwell near and hide [themselves]; they will watch my steps, accordingly as I have waited patiently in my soul.
Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
7 You will on no account save them; you will bring down the people in wrath.
Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
8 O God, I have declared my life to you; you has set my tears before you, even according to your promise.
Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
9 Mine enemies shall be turned back, in the day wherein I shall call upon you; behold, I know that you are my God.
Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
10 In God, will I praise [his] word; in the Lord will I praise [his] saying.
Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
11 I have hoped in God; I will not be afraid of what man shall do to me.
katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
12 The vows of your praise, O God, which I will pay, are upon me.
Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
13 For you have delivered my soul from death, and my feet from sliding, that I should be well-pleasing before God in the land of the living.
Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.

< Psalms 56 >