< Psalms 115 >

1 Not to us, O Lord, not to us, but to your name give glory, because of your mercy and your truth;
Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
2 lest at any time the nations should say, Where is their God?
Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
3 But our God has done in heaven and on earth, whatever he has pleased.
Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
4 The idols of the nations are silver and gold, the works of men's hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
5 They have a mouth, but they can’t speak; they have eyes, but they can’t see:
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
6 they have ears, but they can’t hear; they have noses, but they can’t smell;
zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
7 they have hands, but they can’t handle; they have feet, but they can’t walk: they can’t speak through their throat.
Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
8 Let those that make them become like to them, and all who trust in them.
Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
9 The house of Israel trusts in the Lord: he is their helper and defender.
Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
10 The house of Aaron trusts in the Lord: he is their helper and defender.
Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
11 They that fear the Lord trust in the Lord: he is their helper and defender.
Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
12 The Lord has remembered us, and blessed us: he has blessed the house of Israel, he has blessed the house of Aaron.
Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
13 He has blessed them that fear the Lord, both small and great.
Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
14 The Lord add [blessings] to you and to your children.
Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
15 Blessed are you of the Lord, who made the heaven and the earth.
Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
16 The heaven of heavens [belongs] to the Lord: but he has given the earth to the sons of men.
Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
17 The dead shall not praise you, O Lord, nor any that go down to Hades.
Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
18 But we, the living, will bless the Lord, from henceforth and for ever.
bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.

< Psalms 115 >