< Job 40 >
1 And the Lord God answered Job, and said,
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Will [any one] pervert judgment with the Mighty One? and he that reproves God, let him return it for answer.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 And Job answered and said to the Lord,
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Why do I yet plead? being rebuked even while reproving the Lord: hearing such things, whereas I am nothing: and what shall I answer to these [arguments]? I will lay my hand upon my mouth.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 I have spoken once; but I will not do so a second time.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 And the Lord yet again answered and spoke to Job out of the cloud, [saying],
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Nay, gird up now your loins like a man; and I will ask you, and do you answer me.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Do not set aside my judgment: and do you think that I have dealt with you in any other way, than that you might appear to be righteous?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Hast you an arm like the Lord's? or do you thunder with a voice like his?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Assume now a lofty bearing and power; and clothe yourself with glory and honor.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 And send forth messengers with wrath; and lay low every haughty one.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Bring down also the proud man; and consume at once the ungodly.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 And hide them together in the earth; and fill their faces with shame.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 [Then] will I confess that your right hand can save [you].
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 But now look at the wild beasts with you; they eat grass like oxen.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Behold now, his strength is in his loins, and his force is in the navel of his belly.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 He sets up his tail like a cypress; and his nerves are wrapped together.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 His sides are sides of brass; and his backbone is [as] cast iron.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 This is the chief of the creation of the Lord; made to be played with by his angels.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 And when he has gone up to a steep mountain, he causes joy to the quadrupeds in the deep.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 He lies under trees of every kind, by the papyrus, and reed, and bulrush.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 And the great trees make a shadow over him with their branches, and [so do] the bushes of the field.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 If there should be a flood, he will not perceive it; he trust that Jordan will rush up into his mouth.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 [Yet one] shall take him in his sight; [one] shall catch [him] with a cord, and pierce his nose.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?