< Job 34 >

1 And Elius continued, and said,
Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
2 Hear me, you wise men; listen, you that have knowledge.
“Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
3 For the ear tries words, and the mouth tastes meat.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
4 Let us choose judgment to ourselves: let us know amount ourselves what is right.
Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
5 For Job has said, I am righteous: the Lord has removed my judgment.
Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
6 And he has erred in my judgment: my wound is severe without unrighteousness [of mine].
Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
7 What man is as Job, drinking scorning like water?
Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
8 [saying], I have not sinned, nor committed ungodliness, nor had fellowship with workers of iniquity, to go with the ungodly.
ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
9 For you should not say, There shall be no visitation of a man, whereas [there is] a visitation on him from the Lord.
Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
10 Therefore hear me, you that are wise in heart: far be it from me to sin before the Lord, and to pervert righteousness before the almighty.
Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
11 Yes, he renders to a man accordingly as each of them does, and in a man's path he will find him.
na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
12 And think you that the Lord will do wrong, or will the Almighty who made the earth wrest judgment?
Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
13 And who is he that made [the whole world] under heaven, and all things therein?
Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
14 For if he would confine, and restrain his spirit with himself;
Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
15 all flesh would die together, and every mortal would return to the earth, whence also he was formed.
basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
16 Take heed lest he rebuke [you]: hear this, listen to the voice of words.
Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
17 Behold then the one that hates iniquities, and that destroys the wicked, who is for ever just.
Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
18 [He is] ungodly that says to a king, You are a transgressor, [that says] to princes, O most ungodly one.
Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
19 [Such a one] as would not reverence the face of an honorable man, neither knows how to give honor to the great, so as that their persons should be respected.
Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
20 But it shall turn out vanity to them, to cry and beseech a man; for they dealt unlawfully, the poor being turned aside [from their right].
Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
21 For he surveys the works of men, and nothing of what they do has escaped him.
Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
22 Neither shall there be a place for the workers of iniquity to hide themselves.
Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
23 For he will not lay upon a man more [than right].
Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
24 For the Lord looks down upon all men, who comprehends unsearchable things, glorious also and excellent things without number.
Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
25 Who discovers their works, and will bring night about [upon them], and they shall be brought low.
Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
26 And he quite destroys the ungodly, for they are seen before him.
Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
27 Because they turned aside from the law of God, and did not regard his ordinances,
kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
28 so as to bring before him the cry of the needy; for he will hear the cry of the poor.
Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
29 And he will give quiet, and who will condemn? and he will hide his face, and who shall see him? whether [it be done] against a nation, or against a man also:
Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
30 causing a hypocrite to be king, because of the waywardness of the people.
ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
31 For [there is] one that says to the Mighty One, I have received [blessings]; I will not take a pledge:
Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
32 I will see apart from myself: do you show me if I have done unrighteousness; I will not do [so] any more.
nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
33 Will he take vengeance for it on you, whereas you will put [it] far [from you]? for you shall choose, and not I; and what you know, speak you.
Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
34 Because the wise in heart shall say this, and a wise man listens to my word.
Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
35 But Job has not spoken with understanding, his words are not [uttered] with knowledge.
Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
36 Howbeit do you learn, Job: no longer make answer as the foolish:
Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
37 that we add not to our sins: for iniquity will be reckoned against us, if [we] speak many words before the Lord.
Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”

< Job 34 >