< Exodus 16 >
1 And they departed from Aelim, and all the congregation of the children of Israel came to the wilderness of Sin, which is between Aelim and Sina; and on the fifteenth day, in the second month after their departure from the land of Egypt,
Watu wakaendelea na safari kutoka Elimu, na jamii yote ya Waisraeli ikaja nyikani mwa Sinu, iliyopo katikati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili walipo toka Misri.
2 all the congregation of the children of Israel murmured against Moses and Aaron.
Jamii yote ya Waisraeli wali walalamikia Musa na Aruni nyikani.
3 And the children of Israel said to them, Would we had died struck by the Lord in the land of Egypt, when we sat by the flesh-pots, and ate bread to satiety! for you have brought us out into this wilderness, to kill all this congregation with hunger.
Waisraeli waliwaambia, “Kama tu tungekufa kwa mkono wa Yahweh nchi ya Misri tulipo kuwa tumeketi kwenye vyombo vya nyama na tulikuwa tunakula mkate kwa tele. Maana umetuleta nyikani uuwe jamii zetu zote kwa njaa.”
4 And the Lord said to Moses, Behold, I [will] rain bread upon you out of heaven: and the people shall go forth, and they shall gather their daily portion for the day, that I may try them whether they will walk in my law or not.
Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Nitakunyeshea mvua ya mkate. Watu wataenda na kukusanya kiasi cha siku kila siku ili niwajaribu kama wataendelea kushika sheria yangu au hapana.
5 And it shall come to pass on the sixth day that they shall prepare whatever they have brought in, and it shall be double of what they shall have gathered for the day, daily.
Itakuja kuwa siku ya sita, kwamba watakusanya mara mbili zaidi ya wanavyo kusanyaga, na watapika wanacholeta.”
6 And Moses and Aaron said to all the congregation of the children of Israel, At even you shall know that the Lord has brought you out of the land of Egypt;
Kisha Musa na Aruni wakawaambia watu wote wa Israeli, “Jioni mtajua kuwa ni Yahweh aliye waleta kutoka nchi ya Misri.
7 and in the morning you shall see the glory of the Lord, inasmuch as he hears your murmuring against God; and who are we, that you continue to murmur against us?
Asubui utaona utukufu wa Yahweh, kwa maana anasikia mna mlalamikia. Sisi ni nani hadi mtulalamikie?”
8 And Moses said, [This shall be] when the Lord gives you in the evening flesh to eat, and bread in the morning to satiety, because the Lord has heard your murmuring, which you murmur against us: and what are we? for your murmuring is not against us, but against God.
Musa pia akasema, “Utajua hili pale Yahweh atakapo kupa nyama jioni na mkate asubui kwa tele - kwa kuwa amesikia malalamishi mnayo tamka dhidi yake. Nani ni Aruni na mimi? Malalamishi yenu sio dhidi yetu; ni dhidi ya Yahweh.”
9 And Moses said to Aaron, Say to all the congregation of the children of Israel, Come near before God; for he has heard your murmuring.
Musa akamwambia Aruni, “Sema kwa jamii yote ya watu wa Israeli, 'Njoo karibu ya Yahweh, kwa kuwa amesikia malalamishi yenu.'”
10 And when Aaron spoke to all the congregation of the children of Israel, and they turned toward the wilderness, then the glory of the Lord appeared in a cloud.
Ikawa, Aruni alipo sema na jamii yote ya watu wa Israeli, wakaangalia kuelekea nyikani, na, tazama, utukufu wa Yahweh ukatokea kwenye wingu.
11 And the Lord spoke to Moses, saying,
Kisha Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
12 I have heard the murmuring of the children of Israel: speak to them, saying, Towards evening you shall eat flesh, and in the morning you shall be satisfied with bread; and you shall know that I am the Lord your God.
“Nimesikia malalamishi ya watu wa Israeli. Sema nao na useme, 'Jioni utakula nyama, na asubui utashiba mkate. Kisha utajua mimi ni Yahweh Mungu wako.'”
13 And it was evening, and quails came up and covered the camp:
Ikaja kuwa kwamba jioni kware wakaja juu na kufunika kambi. Asubui umande ulitanda kambini.
14 in the morning it came to pass as the dew ceased round about the camp, that, behold, on the face of the wilderness [was] a small thing like white coriander seed, as frost upon the earth.
Umande ulipo kwisha, pale juu ya ardhi ya nyikani kulikuwa na kama barafu iliyo ganda kwenye ardhi.
15 And when the children of Israel saw it, they said one to another, What is this? for they knew not what it was; and Moses said to them,
Watu wa Israeli walipo ona, walisema mmoja kwa mwenzake, “Hii ni nini?” Hawakujua ilikuwa ni nini. Musa akawaambia, “Ni mkate Yahweh aliyo wapa mle.
16 This [is] the bread which the Lord has given you to eat. This is that which the Lord has appointed: gather of it each man for his family, a homer for each person, according to the number of your souls, gather each of you with his fellow-lodgers.
Hii ni amri Yahweh aliyotoa: 'Lazima ukusanye, kila mmoja wenu, kiasi unacho itaji kula, lita mbili kwa kila mtu. Hivi ndivyo utakavyo kusanya: Kusanya cha kutosha kula cha kila mtu anaye ishi hemani mwako.'”
17 And the children of Israel did so, and gathered some much and some less.
Watu wa Israeli wakafanya hivyo. Baadhi wakakusanya zaidi, baadhi wakakusanya kidogo.
18 And having measured the homer [full], he that gathered much had nothing over, and he that had gathered less had no lack; each gathered according to the need of those who belonged to him.
Walipo pima kwa kipimo cha lita, hao walio kusanya zaidi hawakuwa na kilicho salia, na hao walio kusanya kidogo hawakuwa na pungufu. Kila mmoja alikusanya cha kutosha kukidhi maitaji yake.
19 And Moses said to them, Let no man leave of it till the morning.
Kisha Musa akawaambia, “Hakuna ata mmoja kubakiza hadi asubui.”
20 But they did not listen to Moses, but some left of it till the morning; and it bred worms and stank: and Moses was irritated with them.
Walakini, hawakumsikiliza Musa. Baadhi yao waliacha baadhi hadi asubui, lakini ilizalisha wadudu na kuwa batili. Kisha Musa akawa na hasira juu yao.
21 And they gathered it every morning, each man what he needed, and when the sun waxed hot it melted.
Walikusanya asubui kwa asubui. Kila mtu alikusanya cha kutosha kula kwa hiyo siku. Jua lilipo kuwa kali, ili yayuka.
22 And it came to pass on the sixth day, they gathered double what was needed, two homers for one [man]; and all the chiefs of the synagogue went in and reported it to Moses.
siku ya sita walikusanya mkate mara mbili zaidi, lita mbili kwa kila mtu. Viongozi wote wa jamii walikuja na kumwambia hili kwa Musa.
23 And Moses said to them, Is not this the word which the Lord spoke? To-morrow [is] the sabbath, a holy rest to the Lord: bake that you will bake, and seethe that you will seethe, and all that is over leave to be laid by for the morrow.
Aliwaambia, “Hili ndilo Yahweh alililo lisema: 'Kesho ni mapumziko ya kujiliwaza, sabato takatifu kwa utukufu wa Yahweh. Oka kile unataka kuoka, na chemsha kile unataka kuchemsha. Vyote vitakavyo baki, jihifadhie hadi asubui.”'
24 And they left of it till the morning, as Moses commanded them; and it stank not, neither was there a worm in it.
Hivyo wakaeka pembeni hadi asubui, kama Musa alivyo elekeza. Haikuharibika, wala haikuwa na mdudu yeyote.
25 And Moses said, Eat [that] today, for today is a sabbath to the Lord: [it] shall not be found in the plain.
Musa alisema, “Kula hicho cha kula leo, kwa kuwa leo ni siku iliyo tengwa ya kumtukuza Yahweh. Leo hamtaikuta mashambani.
26 Six days you shall gather it, and on the seventh day is a sabbath, for there shall be none on that [day].
Mtaikusanya ndani ya siku sita, lakini siku ya saba ni Sabato. Siku ya Sabato hakuta kuwa na manna.”
27 And it came to pass on the seventh day [that] some of the people went forth to gather, and found none.
Ilikuja kuwa siku ya saba ambapo baadhi ya watu walienda kukusanya manna, lakini hawakukuta
28 And the Lord said to Moses, How long are you unwilling to listen to my commands and my law?
Kisha Yahweh akamwambia Musa, Kwa muda gani utaendelea kukataa kushika amri zangu na sheria zangu?
29 See, for the Lord has given you this day [as] the sabbath, therefore he has given you on the sixth day the bread of two days: you shall sit each of you in your houses; let no one go forth from his place on the seventh day.
Tazama, Yahweh amekupa Sabato. Hivyo siku ya sita anakupa mkate wa siku mbili. Kila mmoja wenu lazima akae kwenye sehemu yake; hakuna hata mmoja wa kutoka sehemu yake siku ya saba.”
30 And the people kept sabbath on the seventh day.
Hivyo watu watapumzika siku ya saba.
31 And the children of Israel called the name of it Man; and it was as white coriander seed, and the taste of it as a wafer with honey.
Watu wa Israeli walikiita chakula kile “manna.” Ilikuwa ni nyeupe kama mbegu ya mgiligani, na ladha yake kama maandazi yaliyo pikwa na asali.
32 And Moses said, This [is] the thing which the Lord has commanded, Fill an homer with manna, to be laid up for your generations; that they may see the bread which you ate in the wilderness, when the Lord led you forth out of the land of Egypt.
Musa akasema, “Hili ndilo Yahweh alilo amuru: 'Acha lita mbili ya manna ihifadhiwe kwa ajili vizazi vya watu wako ili kwamba uzao wako uone mkate niliyo kulisha nyikani, baada ya kukutoa kutoka nchi ya Misri.
33 And Moses said to Aaron, Take a golden pot, and cast into it one full homer of manna; and you shall lay it up before God, to be kept for your generations,
Musa akamwambia Aruni, “Chukuwa jagi na uweke lita mbili za manna ndani yake. Hifadhi kwa Yahweh i dumu vizazi vyote vya watu.”
34 as the Lord commanded Moses: and Aaron laid it up before the testimony to be kept.
Kama Yahweh alivyo muamuru Musa, Aruni akahifadhi pembeni mwa mawe yaliyo kuwa na amri za agano.
35 And the children of Israel ate manna forty years, until they came to the land they ate the manna, until they came to the region of Phoenicia.
Watu wa Israeli walikula manna miaka arobaini mpaka walipo kuja nchi yenye watu. Walikula mpaka walipo fika kwenye mipaka ya nchi ya Kanani.
36 Now the homer was the tenth part of three measures.
Lita mbili ni makumi ya efa.