< Psalms 81 >

1 To the chief Musician upon Gittith, [A Psalm] of Asaph. Sing aloud unto God our strength: make a joyful noise unto the God of Jacob.
Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
2 Take a psalm, and bring hither the timbrel, the pleasant harp with the psaltery.
Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
3 Blow up the trumpet in the new moon, in the time appointed, on our solemn feast day.
Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
4 For this [was] a statute for Israel, [and] a law of the God of Jacob.
Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
5 This he ordained in Joseph [for] a testimony, when he went out through the land of Egypt: [where] I heard a language [that] I understood not.
Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
6 I removed his shoulder from the burden: his hands were delivered from the pots.
“Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
7 Thou calledst in trouble, and I delivered thee; I answered thee in the secret place of thunder: I proved thee at the waters of Meribah. (Selah)
Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
8 Hear, O my people, and I will testify unto thee: O Israel, if thou wilt hearken unto me;
Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
9 There shall no strange god be in thee; neither shalt thou worship any strange god.
Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
10 I [am] the LORD thy God, which brought thee out of the land of Egypt: open thy mouth wide, and I will fill it.
Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
11 But my people would not hearken to my voice; and Israel would none of me.
Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
12 So I gave them up unto their own hearts’ lust: [and] they walked in their own counsels.
Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
13 Oh that my people had hearkened unto me, [and] Israel had walked in my ways!
Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
14 I should soon have subdued their enemies, and turned my hand against their adversaries.
Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
15 The haters of the LORD should have submitted themselves unto him: but their time should have endured for ever.
Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
16 He should have fed them also with the finest of the wheat: and with honey out of the rock should I have satisfied thee.
Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”

< Psalms 81 >