< Psalms 111 >

1 Praise ye the LORD. I will praise the LORD with [my] whole heart, in the assembly of the upright, and [in] the congregation.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 The works of the LORD [are] great, sought out of all them that have pleasure therein.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 His work [is] honourable and glorious: and his righteousness endureth for ever.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 He hath made his wonderful works to be remembered: the LORD [is] gracious and full of compassion.
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 He hath given meat unto them that fear him: he will ever be mindful of his covenant.
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 He hath shewed his people the power of his works, that he may give them the heritage of the heathen.
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 The works of his hands [are] verity and judgment; all his commandments [are] sure.
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 They stand fast for ever and ever, [and are] done in truth and uprightness.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 He sent redemption unto his people: he hath commanded his covenant for ever: holy and reverend [is] his name.
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 The fear of the LORD [is] the beginning of wisdom: a good understanding have all they that do [his commandments: ] his praise endureth for ever.
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.

< Psalms 111 >