< Mark 15 >

1 And straightway in the morning the chief priests held a consultation with the elders and scribes and the whole council, and bound Jesus, and carried [him] away, and delivered [him] to Pilate.
Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2 And Pilate asked him, Art thou the King of the Jews? And he answering said unto him, Thou sayest [it].
Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 And the chief priests accused him of many things: but he answered nothing.
Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4 And Pilate asked him again, saying, Answerest thou nothing? behold how many things they witness against thee.
Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
5 But Jesus yet answered nothing; so that Pilate marvelled.
Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6 Now at [that] feast he released unto them one prisoner, whomsoever they desired.
Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7 And there was [one] named Barabbas, [which lay] bound with them that had made insurrection with him, who had committed murder in the insurrection.
Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8 And the multitude crying aloud began to desire [him to do] as he had ever done unto them.
Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9 But Pilate answered them, saying, Will ye that I release unto you the King of the Jews?
Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he knew that the chief priests had delivered him for envy.
Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11 But the chief priests moved the people, that he should rather release Barabbas unto them.
Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12 And Pilate answered and said again unto them, What will ye then that I shall do [unto him] whom ye call the King of the Jews?
Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 And they cried out again, Crucify him.
Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
14 Then Pilate said unto them, Why, what evil hath he done? And they cried out the more exceedingly, Crucify him.
Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
15 And [so] Pilate, willing to content the people, released Barabbas unto them, and delivered Jesus, when he had scourged [him], to be crucified.
Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16 And the soldiers led him away into the hall, called Prætorium; and they call together the whole band.
Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 And they clothed him with purple, and platted a crown of thorns, and put it about his [head],
Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18 And began to salute him, Hail, King of the Jews!
Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
19 And they smote him on the head with a reed, and did spit upon him, and bowing [their] knees worshipped him.
Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20 And when they had mocked him, they took off the purple from him, and put his own clothes on him, and led him out to crucify him.
Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21 And they compel one Simon a Cyrenian, who passed by, coming out of the country, the father of Alexander and Rufus, to bear his cross.
Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22 And they bring him unto the place Golgotha, which is, being interpreted, The place of a skull.
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
23 And they gave him to drink wine mingled with myrrh: but he received [it] not.
Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24 And when they had crucified him, they parted his garments, casting lots upon them, what every man should take.
Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25 And it was the third hour, and they crucified him.
Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 And the superscription of his accusation was written over, THE KING OF THE JEWS.
Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 And with him they crucify two thieves; the one on his right hand, and the other on his left.
Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
28 And the scripture was fulfilled, which saith, And he was numbered with the transgressors.
Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
29 And they that passed by railed on him, wagging their heads, and saying, Ah, thou that destroyest the temple, and buildest [it] in three days,
Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30 Save thyself, and come down from the cross.
Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
31 Likewise also the chief priests mocking said among themselves with the scribes, He saved others; himself he cannot save.
Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32 Let Christ the King of Israel descend now from the cross, that we may see and believe. And they that were crucified with him reviled him.
Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33 And when the sixth hour was come, there was darkness over the whole land until the ninth hour.
Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34 And at the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, Eloi, Eloi, lama sabachthani? which is, being interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me?
Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
35 And some of them that stood by, when they heard [it], said, Behold, he calleth Elias.
Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
36 And one ran and filled a spunge full of vinegar, and put [it] on a reed, and gave him to drink, saying, Let alone; let us see whether Elias will come to take him down.
Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
37 And Jesus cried with a loud voice, and gave up the ghost.
Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38 And the veil of the temple was rent in twain from the top to the bottom.
Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39 And when the centurion, which stood over against him, saw that he so cried out, and gave up the ghost, he said, Truly this man was the Son of God.
Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 There were also women looking on afar off: among whom was Mary Magdalene, and Mary the mother of James the less and of Joses, and Salome;
Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41 (Who also, when he was in Galilee, followed him, and ministered unto him; ) and many other women which came up with him unto Jerusalem.
Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42 And now when the even was come, because it was the preparation, that is, the day before the sabbath,
Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43 Joseph of Arimathaea, an honourable counsellor, which also waited for the kingdom of God, came, and went in boldly unto Pilate, and craved the body of Jesus.
Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44 And Pilate marvelled if he were already dead: and calling [unto him] the centurion, he asked him whether he had been any while dead.
Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
45 And when he knew [it] of the centurion, he gave the body to Joseph.
Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
46 And he bought fine linen, and took him down, and wrapped him in the linen, and laid him in a sepulchre which was hewn out of a rock, and rolled a stone unto the door of the sepulchre.
Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47 And Mary Magdalene and Mary [the mother] of Joses beheld where he was laid.
Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.

< Mark 15 >