< Luke 22 >
1 Now the feast of unleavened bread drew nigh, which is called the Passover.
Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2 And the chief priests and scribes sought how they might kill him; for they feared the people.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3 Then entered Satan into Judas surnamed Iscariot, being of the number of the twelve.
Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4 And he went his way, and communed with the chief priests and captains, how he might betray him unto them.
Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5 And they were glad, and covenanted to give him money.
Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6 And he promised, and sought opportunity to betray him unto them in the absence of the multitude.
Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7 Then came the day of unleavened bread, when the passover must be killed.
Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8 And he sent Peter and John, saying, Go and prepare us the passover, that we may eat.
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
9 And they said unto him, Where wilt thou that we prepare?
Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
10 And he said unto them, Behold, when ye are entered into the city, there shall a man meet you, bearing a pitcher of water; follow him into the house where he entereth in.
Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11 And ye shall say unto the goodman of the house, The Master saith unto thee, Where is the guestchamber, where I shall eat the passover with my disciples?
Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12 And he shall shew you a large upper room furnished: there make ready.
Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
13 And they went, and found as he had said unto them: and they made ready the passover.
Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14 And when the hour was come, he sat down, and the twelve apostles with him.
Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15 And he said unto them, With desire I have desired to eat this passover with you before I suffer:
Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16 For I say unto you, I will not any more eat thereof, until it be fulfilled in the kingdom of God.
Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
17 And he took the cup, and gave thanks, and said, Take this, and divide [it] among yourselves:
Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18 For I say unto you, I will not drink of the fruit of the vine, until the kingdom of God shall come.
Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
19 And he took bread, and gave thanks, and brake [it], and gave unto them, saying, This is my body which is given for you: this do in remembrance of me.
Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
20 Likewise also the cup after supper, saying, This cup [is] the new testament in my blood, which is shed for you.
Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21 But, behold, the hand of him that betrayeth me [is] with me on the table.
“Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22 And truly the Son of man goeth, as it was determined: but woe unto that man by whom he is betrayed!
Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
23 And they began to enquire among themselves, which of them it was that should do this thing.
Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24 And there was also a strife among them, which of them should be accounted the greatest.
Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25 And he said unto them, The kings of the Gentiles exercise lordship over them; and they that exercise authority upon them are called benefactors.
Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26 But ye [shall] not [be] so: but he that is greatest among you, let him be as the younger; and he that is chief, as he that doth serve.
Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27 For whether [is] greater, he that sitteth at meat, or he that serveth? [is] not he that sitteth at meat? but I am among you as he that serveth.
Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28 Ye are they which have continued with me in my temptations.
“Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29 And I appoint unto you a kingdom, as my Father hath appointed unto me;
na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30 That ye may eat and drink at my table in my kingdom, and sit on thrones judging the twelve tribes of Israel.
Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31 And the Lord said, Simon, Simon, behold, Satan hath desired [to have] you, that he may sift [you] as wheat:
“Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32 But I have prayed for thee, that thy faith fail not: and when thou art converted, strengthen thy brethren.
Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
33 And he said unto him, Lord, I am ready to go with thee, both into prison, and to death.
Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
34 And he said, I tell thee, Peter, the cock shall not crow this day, before that thou shalt thrice deny that thou knowest me.
Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
35 And he said unto them, When I sent you without purse, and scrip, and shoes, lacked ye any thing? And they said, Nothing.
Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
36 Then said he unto them, But now, he that hath a purse, let him take [it], and likewise [his] scrip: and he that hath no sword, let him sell his garment, and buy one.
Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37 For I say unto you, that this that is written must yet be accomplished in me, And he was reckoned among the transgressors: for the things concerning me have an end.
Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
38 And they said, Lord, behold, here [are] two swords. And he said unto them, It is enough.
Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
39 And he came out, and went, as he was wont, to the mount of Olives; and his disciples also followed him.
Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40 And when he was at the place, he said unto them, Pray that ye enter not into temptation.
Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
41 And he was withdrawn from them about a stone’s cast, and kneeled down, and prayed,
Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42 Saying, Father, if thou be willing, remove this cup from me: nevertheless not my will, but thine, be done.
“Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
43 And there appeared an angel unto him from heaven, strengthening him.
Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44 And being in an agony he prayed more earnestly: and his sweat was as it were great drops of blood falling down to the ground.
Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45 And when he rose up from prayer, and was come to his disciples, he found them sleeping for sorrow,
Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46 And said unto them, Why sleep ye? rise and pray, lest ye enter into temptation.
Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
47 And while he yet spake, behold a multitude, and he that was called Judas, one of the twelve, went before them, and drew near unto Jesus to kiss him.
Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48 But Jesus said unto him, Judas, betrayest thou the Son of man with a kiss?
Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
49 When they which were about him saw what would follow, they said unto him, Lord, shall we smite with the sword?
Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
50 And one of them smote the servant of the high priest, and cut off his right ear.
Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51 And Jesus answered and said, Suffer ye thus far. And he touched his ear, and healed him.
Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52 Then Jesus said unto the chief priests, and captains of the temple, and the elders, which were come to him, Be ye come out, as against a thief, with swords and staves?
Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53 When I was daily with you in the temple, ye stretched forth no hands against me: but this is your hour, and the power of darkness.
Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
54 Then took they him, and led [him], and brought him into the high priest’s house. And Peter followed afar off.
Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55 And when they had kindled a fire in the midst of the hall, and were set down together, Peter sat down among them.
Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56 But a certain maid beheld him as he sat by the fire, and earnestly looked upon him, and said, This man was also with him.
Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
57 And he denied him, saying, Woman, I know him not.
Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
58 And after a little while another saw him, and said, Thou art also of them. And Peter said, Man, I am not.
Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
59 And about the space of one hour after another confidently affirmed, saying, Of a truth this [fellow] also was with him: for he is a Galilæan.
Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
60 And Peter said, Man, I know not what thou sayest. And immediately, while he yet spake, the cock crew.
Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61 And the Lord turned, and looked upon Peter. And Peter remembered the word of the Lord, how he had said unto him, Before the cock crow, thou shalt deny me thrice.
Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
62 And Peter went out, and wept bitterly.
Hapo akatoka nje, akalia sana.
63 And the men that held Jesus mocked him, and smote [him].
Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64 And when they had blindfolded him, they struck him on the face, and asked him, saying, Prophesy, who is it that smote thee?
Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
65 And many other things blasphemously spake they against him.
Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66 And as soon as it was day, the elders of the people and the chief priests and the scribes came together, and led him into their council, saying,
Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67 Art thou the Christ? tell us. And he said unto them, If I tell you, ye will not believe:
Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68 And if I also ask [you], ye will not answer me, nor let [me] go.
na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69 Hereafter shall the Son of man sit on the right hand of the power of God.
Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
70 Then said they all, Art thou then the Son of God? And he said unto them, Ye say that I am.
Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
71 And they said, What need we any further witness? for we ourselves have heard of his own mouth.
Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”