< Job 31 >
1 I made a covenant with mine eyes; why then should I think upon a maid?
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 For what portion of God [is there] from above? and [what] inheritance of the Almighty from on high?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 [Is] not destruction to the wicked? and a strange [punishment] to the workers of iniquity?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Doth not he see my ways, and count all my steps?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 If I have walked with vanity, or if my foot hath hasted to deceit;
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Let me be weighed in an even balance, that God may know mine integrity.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 If my step hath turned out of the way, and mine heart walked after mine eyes, and if any blot hath cleaved to mine hands;
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 [Then] let me sow, and let another eat; yea, let my offspring be rooted out.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 If mine heart have been deceived by a woman, or [if] I have laid wait at my neighbour’s door;
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 [Then] let my wife grind unto another, and let others bow down upon her.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For this [is] an heinous crime; yea, it [is] an iniquity [to be punished by] the judges.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 For it [is] a fire [that] consumeth to destruction, and would root out all mine increase.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 If I did despise the cause of my manservant or of my maidservant, when they contended with me;
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 What then shall I do when God riseth up? and when he visiteth, what shall I answer him?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Did not he that made me in the womb make him? and did not one fashion us in the womb?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 If I have withheld the poor from [their] desire, or have caused the eyes of the widow to fail;
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 Or have eaten my morsel myself alone, and the fatherless hath not eaten thereof;
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (For from my youth he was brought up with me, as [with] a father, and I have guided her from my mother’s womb; )
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 If I have seen any perish for want of clothing, or any poor without covering;
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 If his loins have not blessed me, and [if] he were [not] warmed with the fleece of my sheep;
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 If I have lifted up my hand against the fatherless, when I saw my help in the gate:
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 [Then] let mine arm fall from my shoulder blade, and mine arm be broken from the bone.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For destruction [from] God [was] a terror to me, and by reason of his highness I could not endure.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 If I have made gold my hope, or have said to the fine gold, [Thou art] my confidence;
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 If I rejoiced because my wealth [was] great, and because mine hand had gotten much;
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 If I beheld the sun when it shined, or the moon walking [in] brightness;
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 And my heart hath been secretly enticed, or my mouth hath kissed my hand:
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 This also [were] an iniquity [to be punished by] the judge: for I should have denied the God [that is] above.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 If I rejoiced at the destruction of him that hated me, or lifted up myself when evil found him:
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 Neither have I suffered my mouth to sin by wishing a curse to his soul.
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 If the men of my tabernacle said not, Oh that we had of his flesh! we cannot be satisfied.
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 The stranger did not lodge in the street: [but] I opened my doors to the traveller.
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 If I covered my transgressions as Adam, by hiding mine iniquity in my bosom:
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 Did I fear a great multitude, or did the contempt of families terrify me, that I kept silence, [and] went not out of the door?
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Oh that one would hear me! behold, my desire [is, that] the Almighty would answer me, and [that] mine adversary had written a book.
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Surely I would take it upon my shoulder, [and] bind it [as] a crown to me.
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 I would declare unto him the number of my steps; as a prince would I go near unto him.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 If my land cry against me, or that the furrows likewise thereof complain;
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 If I have eaten the fruits thereof without money, or have caused the owners thereof to lose their life:
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Let thistles grow instead of wheat, and cockle instead of barley. The words of Job are ended.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.