< Ezekiel 40 >

1 In the five and twentieth year of our captivity, in the beginning of the year, in the tenth [day] of the month, in the fourteenth year after that the city was smitten, in the selfsame day the hand of the LORD was upon me, and brought me thither.
Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
2 In the visions of God brought he me into the land of Israel, and set me upon a very high mountain, by which [was] as the frame of a city on the south.
Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
3 And he brought me thither, and, behold, [there was] a man, whose appearance [was] like the appearance of brass, with a line of flax in his hand, and a measuring reed; and he stood in the gate.
Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
4 And the man said unto me, Son of man, behold with thine eyes, and hear with thine ears, and set thine heart upon all that I shall shew thee; for to the intent that I might shew [them] unto thee [art] thou brought hither: declare all that thou seest to the house of Israel.
Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
5 And behold a wall on the outside of the house round about, and in the man’s hand a measuring reed of six cubits [long] by the cubit and an hand breadth: so he measured the breadth of the building, one reed; and the height, one reed.
Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
6 Then came he unto the gate which looketh toward the east, and went up the stairs thereof, and measured the threshold of the gate, [which was] one reed broad; and the other threshold [of the gate, which was] one reed broad.
Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
7 And [every] little chamber [was] one reed long, and one reed broad; and between the little chambers [were] five cubits; and the threshold of the gate by the porch of the gate within [was] one reed.
Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
8 He measured also the porch of the gate within, one reed.
Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
9 Then measured he the porch of the gate, eight cubits; and the posts thereof, two cubits; and the porch of the gate [was] inward.
ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
10 And the little chambers of the gate eastward [were] three on this side, and three on that side; they three [were] of one measure: and the posts had one measure on this side and on that side.
Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
11 And he measured the breadth of the entry of the gate, ten cubits; [and] the length of the gate, thirteen cubits.
Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
12 The space also before the little chambers [was] one cubit [on this side], and the space [was] one cubit on that side: and the little chambers [were] six cubits on this side, and six cubits on that side.
Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
13 He measured then the gate from the roof of [one] little chamber to the roof of another: the breadth [was] five and twenty cubits, door against door.
Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
14 He made also posts of threescore cubits, even unto the post of the court round about the gate.
Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
15 And from the face of the gate of the entrance unto the face of the porch of the inner gate [were] fifty cubits.
Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
16 And [there were] narrow windows to the little chambers, and to their posts within the gate round about, and likewise to the arches: and windows [were] round about inward: and upon [each] post [were] palm trees.
Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
17 Then brought he me into the outward court, and, lo, [there were] chambers, and a pavement made for the court round about: thirty chambers [were] upon the pavement.
Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
18 And the pavement by the side of the gates over against the length of the gates [was] the lower pavement.
Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
19 Then he measured the breadth from the forefront of the lower gate unto the forefront of the inner court without, an hundred cubits eastward and northward.
Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
20 And the gate of the outward court that looked toward the north, he measured the length thereof, and the breadth thereof.
Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
21 And the little chambers thereof [were] three on this side and three on that side; and the posts thereof and the arches thereof were after the measure of the first gate: the length thereof [was] fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
22 And their windows, and their arches, and their palm trees, [were] after the measure of the gate that looketh toward the east; and they went up unto it by seven steps; and the arches thereof [were] before them.
Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
23 And the gate of the inner court [was] over against the gate toward the north, and toward the east; and he measured from gate to gate an hundred cubits.
Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
24 After that he brought me toward the south, and behold a gate toward the south: and he measured the posts thereof and the arches thereof according to these measures.
Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
25 And [there were] windows in it and in the arches thereof round about, like those windows: the length [was] fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
26 And [there were] seven steps to go up to it, and the arches thereof [were] before them: and it had palm trees, one on this side, and another on that side, upon the posts thereof.
Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
27 And [there was] a gate in the inner court toward the south: and he measured from gate to gate toward the south an hundred cubits.
Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
28 And he brought me to the inner court by the south gate: and he measured the south gate according to these measures;
Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
29 And the little chambers thereof, and the posts thereof, and the arches thereof, according to these measures: and [there were] windows in it and in the arches thereof round about: [it was] fifty cubits long, and five and twenty cubits broad.
Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
30 And the arches round about [were] five and twenty cubits long, and five cubits broad.
(Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
31 And the arches thereof [were] toward the utter court; and palm trees [were] upon the posts thereof: and the going up to it [had] eight steps.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
32 And he brought me into the inner court toward the east: and he measured the gate according to these measures.
Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
33 And the little chambers thereof, and the posts thereof, and the arches thereof, [were] according to these measures: and [there were] windows therein and in the arches thereof round about: [it was] fifty cubits long, and five and twenty cubits broad.
Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
34 And the arches thereof [were] toward the outward court; and palm trees [were] upon the posts thereof, on this side, and on that side: and the going up to it [had] eight steps.
Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
35 And he brought me to the north gate, and measured [it] according to these measures;
Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
36 The little chambers thereof, the posts thereof, and the arches thereof, and the windows to it round about: the length [was] fifty cubits, and the breadth five and twenty cubits.
kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
37 And the posts thereof [were] toward the utter court; and palm trees [were] upon the posts thereof, on this side, and on that side: and the going up to it [had] eight steps.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
38 And the chambers and the entries thereof [were] by the posts of the gates, where they washed the burnt offering.
Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
39 And in the porch of the gate [were] two tables on this side, and two tables on that side, to slay thereon the burnt offering and the sin offering and the trespass offering.
Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
40 And at the side without, as one goeth up to the entry of the north gate, [were] two tables; and on the other side, which [was] at the porch of the gate, [were] two tables.
Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
41 Four tables [were] on this side, and four tables on that side, by the side of the gate; eight tables, whereupon they slew [their sacrifices].
Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
42 And the four tables [were] of hewn stone for the burnt offering, of a cubit and an half long, and a cubit and an half broad, and one cubit high: whereupon also they laid the instruments wherewith they slew the burnt offering and the sacrifice.
Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
43 And within [were] hooks, an hand broad, fastened round about: and upon the tables [was] the flesh of the offering.
Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
44 And without the inner gate [were] the chambers of the singers in the inner court, which [was] at the side of the north gate; and their prospect [was] toward the south: one at the side of the east gate [having] the prospect toward the north.
Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
45 And he said unto me, This chamber, whose prospect [is] toward the south, [is] for the priests, the keepers of the charge of the house.
Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
46 And the chamber whose prospect [is] toward the north [is] for the priests, the keepers of the charge of the altar: these [are] the sons of Zadok among the sons of Levi, which come near to the LORD to minister unto him.
nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
47 So he measured the court, an hundred cubits long, and an hundred cubits broad, foursquare; and the altar [that was] before the house.
Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
48 And he brought me to the porch of the house, and measured [each] post of the porch, five cubits on this side, and five cubits on that side: and the breadth of the gate [was] three cubits on this side, and three cubits on that side.
Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
49 The length of the porch [was] twenty cubits, and the breadth eleven cubits; and [he brought me] by the steps whereby they went up to it: and [there were] pillars by the posts, one on this side, and another on that side.
Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.

< Ezekiel 40 >