< Psalms 31 >

1 In you, O LORD, do I put my trust; let me never be ashamed: deliver me in your righteousness.
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
2 Bow down your ear to me; deliver me speedily: be you my strong rock, for an house of defence to save me.
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
3 For you are my rock and my fortress; therefore for your name's sake lead me, and guide me.
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
4 Pull me out of the net that they have laid privately for me: for you are my strength.
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
5 Into your hand I commit my spirit: you have redeemed me, O LORD God of truth.
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
6 I have hated them that regard lying vanities: but I trust in the LORD.
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
7 I will be glad and rejoice in your mercy: for you have considered my trouble; you have known my soul in adversities;
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
8 And have not shut me up into the hand of the enemy: you have set my feet in a large room.
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
9 Have mercy upon me, O LORD, for I am in trouble: mine eye is consumed with grief, yea, my soul and my belly.
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
10 For my life is spent with grief, and my years with sighing: my strength fails because of mine iniquity, and my bones are consumed.
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
11 I was a reproach among all mine enemies, but especially among my neighbours, and a fear to mine acquaintance: they that did see me without fled from me.
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
12 I am forgotten as a dead man out of mind: I am like a broken vessel.
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
13 For I have heard the slander of many: fear was on every side: while they took counsel together against me, they devised to take away my life.
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
14 But I trusted in you, O LORD: I said, You are my God.
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
15 My times are in your hand: deliver me from the hand of mine enemies, and from them that persecute me.
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
16 Make your face to shine upon your servant: save me for your mercies' sake.
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
17 Let me not be ashamed, O LORD; for I have called upon you: let the wicked be ashamed, and let them be silent in the grave. (Sheol h7585)
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
18 Let the lying lips be put to silence; which speak grievous things proudly and contemptuously against the righteous.
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
19 Oh how great is your goodness, which you have laid up for them that fear you; which you have wrought for them that trust in you before the sons of men!
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
20 You shall hide them in the secret of your presence from the pride of man: you shall keep them secretly in a pavilion from the strife of tongues.
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
21 Blessed be the LORD: for he has showed me his marvellous kindness in a strong city.
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
22 For I said in my haste, I am cut off from before your eyes: nevertheless you heard the voice of my supplications when I cried unto you.
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
23 O love the LORD, all you his saints: for the LORD perserves the faithful, and plentifully rewards the proud doer.
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
24 Be of good courage, and he shall strengthen your heart, all you that hope in the LORD.
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.

< Psalms 31 >