< Mark 5 >
1 And they came over unto the other side of the sea, into the country of the Gadarenes.
Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2 And when he was come out of the ship, immediately there met him out of the tombs a man with an unclean spirit, (pneuma)
Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3 Who had his dwelling among the tombs; and no man could bind him, no, not with chains:
Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4 Because that he had been often bound with fetters and chains, and the chains had been plucked asunder by him, and the fetters broken in pieces: neither could any man tame him.
Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5 And always, night and day, he was in the mountains, and in the tombs, crying, and cutting himself with stones.
Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6 But when he saw Jesus far off, he ran and worshipped him,
Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7 And cried with a loud voice, and said, What have I to do with you, Jesus, you Son of the most high God? I adjure you by God, that you torment me not.
akisema kwa sauti kubwa, “Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!”
8 For he said unto him, Come out of the man, you unclean spirit. (pneuma)
(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.”)
9 And he asked him, What is your name? And he answered, saying, My name is Legion: for we are many.
Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Naye akajibu, “Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi.”
10 And he besought him much that he would not send them away out of the country.
Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11 Now there was there nigh unto the mountains a great herd of swine feeding.
Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12 And all the devils besought him, saying, Send us into the swine, that we may enter into them.
Basi, hao pepo wakamsihi, “Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie.”
13 And forthwith Jesus gave them leave. And the unclean spirits (pneuma) went out, and entered into the swine: and the herd ran violently down a steep place into the sea, (they were about two thousand; ) and were choked in the sea.
Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14 And they that fed the swine fled, and told it in the city, and in the country. And they went out to see what it was that was done.
Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15 And they come to Jesus, and see him that was possessed with the devil, and had the legion, sitting, and clothed, and in his right mind: and they were afraid.
Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16 And they that saw it told them how it befell to him that was possessed with the devil, and also concerning the swine.
Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17 And they began to pray him to depart out of their coasts.
Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18 And when he was come into the ship, he that had been possessed with the devil prayed him that he might be with him.
Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19 Nevertheless Jesus suffered him not, but says unto him, Go home to your friends, and tell them how great things the Lord has done for you, and has had compassion on you.
Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma.”
20 And he departed, and began to publish in Decapolis how great things Jesus had done for him: and all men did marvel.
Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21 And when Jesus was passed over again by ship unto the other side, much people gathered unto him: and he was nigh unto the sea.
Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22 And, behold, there comes one of the rulers of the synagogue, Jairus by name; and when he saw him, he fell at his feet,
Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23 And besought him greatly, saying, My little daughter lies at the point of death: I pray you, come and lay your hands on her, that she may be healed; and she shall live.
akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi.”
24 And Jesus went with him; and much people followed him, and thronged him.
Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25 And a certain woman, which had an issue of blood twelve years,
Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26 And had suffered many things of many physicians, and had spent all that she had, and was nothing improved, but rather grew worse,
Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27 When she had heard of Jesus, came in the press behind, and touched his garment.
Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28 For she said, If I may touch but his clothes, I shall be whole.
Alifanya hivyo, maana alijisemea, “Nikigusa tu vazi lake, nitapona.”
29 And immediately the fountain of her blood was dried up; and she felt in her body that she was healed of that plague.
Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30 And Jesus, immediately knowing in himself that virtue had gone out of him, turned him about in the press, and said, Who touched my clothes?
Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, “Nani aliyegusa mavazi yangu?”
31 And his disciples said unto him, You see the multitude thronging you, and say you, Who touched me?
Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?”
32 And he looked round about to see her that had done this thing.
Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33 But the woman fearing and trembling, knowing what was done in her, came and fell down before him, and told him all the truth.
Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34 And he said unto her, Daughter, your faith has made you whole; go in peace, and be whole of your plague.
Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
35 While he yet spoke, there came from the ruler of the synagogue's house certain which said, Your daughter is dead: why trouble you the Master any further?
Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
36 As soon as Jesus heard the word (logos) that was spoken, he says unto the ruler of the synagogue, Be not afraid, only believe.
Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, “Usiogope, amini tu.”
37 And he suffered no man to follow him, save Peter, and James, and John the brother of James.
Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38 And he comes to the house of the ruler of the synagogue, and sees the tumult, and them that wept and wailed greatly.
Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39 And when he was come in, he says unto them, Why make all of you this disturbance, and weep? the damsel is not dead, but sleeps.
Akaingia ndani, akawaambia, “Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu.”
40 And they laughed him to scorn. But when he had put them all out, he takes the father and the mother of the damsel, and them that were with him, and enters in where the damsel was lying.
Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41 And he took the damsel by the hand, and said unto her, Talitha cumi; which is, being interpreted, Damsel, I say unto you, arise.
Kisha akamshika mkono, akamwambia, “Talitha, kumi,” maana yake, “Msichana, nakwambia, amka!”
42 And immediately the damsel arose, and walked; for she was of the age of twelve years. And they were astonished with a great astonishment.
Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43 And he charged them strictly that no man should know it; and commanded that something should be given her to eat.
Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.