< Mark 11 >
1 And when they came nigh to Jerusalem, unto Bethphage and Bethany, at the mount of Olives, he sends forth two of his disciples,
Walipokuwa wanakaribia Yerusalemu walifika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni. Hapo aliwatuma wawili wa wanafunzi wake,
2 And says unto them, Go your way into the village opposite to you: and as soon as all of you be entered into it, all of you shall find a colt tied, whereon never man sat; loose him, and bring him.
akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia humo, mtakuta mwana punda amefungwa ambaye bado hajatumiwa na mtu. Mfungueni mkamlete.
3 And if any man say unto you, Why do all of you this? say all of you that the Lord has need of him; and immediately he will send him here.
Kama mtu akiwauliza, Mbona mnafanya hivyo? Mwambieni, Bwana anamhitaji na atamrudisha hapa mara.”
4 And they went their way, and found the colt tied by the door without in a place where two ways met; and they loose him.
Basi, wakaenda, wakamkuta mwana punda barabarani amefungwa mlangoni. Walipokuwa wakimfungua,
5 And certain of them that stood there said unto them, What do all of you, loosing the colt?
baadhi ya watu waliokuwa wamesimama hapo wakawauliza “Kwa nini mnamfungua huyo mwana punda?”
6 And they said unto them even as Jesus had commanded: and they let them go.
Wanafunzi wakajibu kama Yesu alivyokuwa amewaambia; nao wakawaacha waende zao.
7 And they brought the colt to Jesus, and cast their garments on him; and he sat upon him.
Wakampelekea Yesu huyo mwana punda. Wakatandika mavazi yao juu ya huyo mwana punda, na Yesu akaketi juu yake.
8 And many spread their garments in the way: and others cut down branches off the trees, and scattered them in the way.
Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani; wengine wakatandaza matawi ya miti waliyoyakata mashambani.
9 And they that went before, and they that followed, cried, saying, Hosanna; Blessed is he that comes in the name of the Lord:
Watu wote waliotangulia na wale waliofuata wakapaaza sauti zao wakisema, “Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana!
10 Blessed be the kingdom of our father David, that comes in the name of the Lord: Hosanna in the highest.
Ubarikiwe Ufalme ujao wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni!”
11 And Jesus entered into Jerusalem, and into the temple: and when he had looked round about upon all things, and now the evening was come, he went out unto Bethany with the twelve.
Yesu aliingia mjini Yerusalemu akaenda moja kwa moja mpaka Hekaluni, akatazama kila kitu kwa makini. Lakini kwa vile ilikwisha kuwa jioni, akaenda Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
12 And on the next day, when they were come from Bethany, he was hungry:
Kesho yake, walipokuwa wanatoka Bethania, Yesu aliona njaa.
13 And seeing a fig tree far off having leaves, he came, if lest by any means he might find any thing thereon: and when he came to it, he found nothing but leaves; for the time of figs was not yet.
Basi, akaona kwa mbali mtini wenye majani mengi. Akauendea ili aone kama ulikuwa na tunda lolote. Alipoufikia, aliukuta bila tunda lolote ila majani matupu, kwa vile hayakuwa majira ya mtini kuzaa matunda.
14 And Jesus answered and said unto it, No man eat fruit of you hereafter for ever. And his disciples heard it. (aiōn )
Hapo akauambia mtini, “Tangu leo hata milele mtu yeyote asile matunda kwako.” Nao wanafunzi wake walisikia maneno hayo. (aiōn )
15 And they come to Jerusalem: and Jesus went into the temple, and began to cast out them that sold and bought in the temple, and overthrew the tables of the moneychangers, and the seats of them that sold doves;
Basi, wakafika Yerusalemu. Yesu akaingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza nje watu waliokuwa wanauza na kununua vitu humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilishana fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
16 And would not suffer that any man should carry any vessel through the temple.
Hakumruhusu mtu yeyote kupitia Hekaluni akichukua kitu.
17 And he taught, saying unto them, Is it not written, My house shall be called of all nations the house of prayer? but all of you have made it a den of thieves.
Kisha akawafundisha, “Imeandikwa: Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote! Lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi!”
18 And the scribes and chief priests heard it, and sought how they might destroy him: for they feared him, because all the people was astonished at his doctrine.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria waliposikia hayo, walianza kutafuta njia ya kumwangamiza. Lakini walimwogopa kwa sababu umati wa watu ulishangazwa na mafundisho yake.
19 And when even was come, he went out of the city.
Ilipokuwa jioni, Yesu na wanafunzi wake waliondoka mjini.
20 And in the morning, as they passed by, they saw the fig tree dried up from the roots.
Asubuhi na mapema, walipokuwa wanapita, waliuona ule mtini umenyauka wote, hata mizizi.
21 And Peter calling to remembrance says unto him, Master, behold, the fig tree which you cursed is withered away.
Petro aliukumbuka, akamwambia Yesu, “Mwalimu, tazama! Ule mtini ulioulaani, umenyauka!”
22 And Jesus answering says unto them, Have faith in God.
Yesu akawaambia, “Mwaminini Mungu.
23 For verily I say unto you, That whosoever shall say unto this mountain, Be you removed, and be you cast into the sea; and shall not doubt in his heart, but shall believe that those things which he says shall come to pass; he shall have whatsoever he says.
Nawaambieni kweli, mtu akiuambia mlima huu: Ng'oka ukajitose baharini bila kuona shaka moyoni mwake, ila akaamini kwamba mambo yote anayosema yanafanyika, atafanyiwa jambo hilo.
24 Therefore I say unto you, What things whatsoever all of you desire, when all of you pray, believe that all of you receive them, and all of you shall have them.
Kwa hiyo nawaambieni, mnaposali na kuomba kitu, aminini kwamba mmekipokea, nanyi mtapewa.
25 And when all of you stand praying, forgive, if all of you have ought against any: that your Father also which is in heaven may forgive you your trespasses.
Mnaposimama kusali, sameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu.
26 But if all of you do not forgive, neither will your Father which is in heaven forgive your trespasses.
Lakini msipowasamehe wengine, hata Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.”
27 And they come again to Jerusalem: and as he was walking in the temple, there come to him the chief priests, and the scribes, and the elders,
Basi, wakafika tena Yerusalemu. Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee walimwendea,
28 And say unto him, By what authority do you these things? and who gave you this authority to do these things?
wakamwuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Nani aliyekupa mamlaka ya kufanya mambo haya?”
29 And Jesus answered and said unto them, I will also ask of you one question, (logos) and answer me, and I will tell you by what authority I do these things.
Lakini Yesu akawaambia, “Nitawaulizeni swali moja; mkinijibu, na pia nitawaambieni ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
30 The baptism of John, was it from heaven, or of men? answer me.
Je, mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka mbinguni ama kwa watu? Nijibuni.”
31 And they reasoned with themselves, saying, If we shall say, From heaven; he will say, Why then did all of you not believe him?
Wakaanza kujadiliana, “Tukisema, Yalitoka mbinguni, atatuuliza, Basi, mbona hamkumsadiki?
32 But if we shall say, Of men; they feared the people: for all men counted John, that he was a prophet indeed.
Na tukisema, Yalitoka kwa watu...” (Waliogopa umati wa watu maana wote waliamini kwamba Yohane alikuwa kweli nabii.)
33 And they answered and said unto Jesus, We cannot tell. And Jesus answering says unto them, Neither do I tell you by what authority I do these things.
Basi, wakamjibu Yesu, “Sisi hatujui.” Naye Yesu akawaambia, “Nami pia sitawaambieni ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”