< Job 37 >

1 At this also my heart trembles, and is moved out of his place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Hear attentively the noise of his voice, and the sound that goes out of his mouth.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 He directs it under the whole heaven, and his lightning unto the ends of the earth.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 After it a voice roars: he thunders with the voice of his excellency; and he will not stay them when his voice is heard.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 God thunders marvellously with his voice; great things does he, which we cannot comprehend.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 For he says to the snow, Be you on the earth; likewise to the small rain, and to the great rain of his strength.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 He seals up the hand of every man; that all men may know his work.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Then the beasts go into dens, and remain in their places.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Out of the south comes the whirlwind: and cold out of the north.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 By the breath of God frost is given: and the breadth of the waters is straitened.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Also by watering he wearies the thick cloud: he scatters his bright cloud:
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 And it is turned round about by his counsels: that they may do whatsoever he commands them upon the face of the world in the earth.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 He causes it to come, whether for correction, or for his land, or for mercy.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Hearken unto this, O Job: stand still, and consider the wondrous works of God.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Do you know when God disposed them, and caused the light of his cloud to shine?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Do you know the balancings of the clouds, the wondrous works of him which is perfect in knowledge?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 How your garments are warm, when he stills the earth by the south wind?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Have you with him spread out the sky, which is strong, and as a molten looking glass?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Teach us what we shall say unto him; for we cannot order our speech by reason of darkness.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Shall it be told him that I speak? if a man speak, surely he shall be swallowed up.
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 And now men see not the bright light which is in the clouds: but the wind passes, and cleanses them.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Fair weather comes out of the north: with God is terrible majesty.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Concerning the Almighty, we cannot find him out: he is excellent in power, and in judgment, and in plenty of justice: he will not afflict.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Men do therefore fear him: he respects not any that are wise of heart.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >