< Hebrews 3 >
1 Wherefore, holy brethren, partakers of the heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our profession, Christ Jesus;
Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa wito wa mbinguni, mumfikiri Yesu, Mtume na Kuhani Mkuu wa ukiri wetu.
2 Who was faithful to him that appointed him, as also Moses was faithful in all his house.
Alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua, kama Musa alivyokuwa mwaminifu pia katika nyumba yote ya Mungu.
3 For this man was counted worthy of more glory than Moses, inasmuch as he who has built the house has more honour than the house.
Kwa kuwa Yesu amehesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko aliyokuwa nayo Musa, kwa sababu yule anayejenga nyumba anahesabiwa kuwa na heshima kubwa kuliko nyumba yenyewe.
4 For every house is built by some man; but he that built all things is God.
Kwa kuwa kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule anayejenga kila kitu ni Mungu.
5 And Moses verily was faithful in all his house, as a servant, for a testimony of those things which were to be spoken after;
Hakika Musa alikuwa mwaminifu kama mtumishi katika nyumba yote ya Mungu, akitoa ushuhuda kuhusu mambo yatakayosemwa wakati ujao.
6 But Christ as a son over his own house; whose house are we, if we hold fast the confidence and the rejoicing of the hope firm unto the end.
Lakini Kristo ni Mwana katika usimamizi wa nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tutashikilia haraka katika kujiamini na fahari ya kujiamini.
7 Wherefore (as the Holy Spirit (pneuma) says, To day if all of you will hear his voice,
Kwa hiyo, ni kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, kama utasikia sauti yake,
8 Harden not your hearts, as in the provocation, in the day of temptation in the wilderness:
Usiufanye moyo wako kuwa mgumu kama Waisraeli walivyofanya katika uasi, katika wakati wa kujaribiwa nyikani.
9 When your fathers tempted me, proved me, and saw my works forty years.
Huu ulikuwa wakati ambao baba zenu waliniasi kwa kunijaribu, na wakati, kwa miaka arobaini, waliona matendo yangu.
10 Wherefore I was grieved with that generation, and said, They do always go astray in their heart; and they have not known my ways.
Kwa hiyo sikufurahishwa na kizazi hicho. Nilisema, 'Wanapotea kila mara katika mioyo yao, na hawajui njia zangu.
11 So I swore in my wrath, They shall not enter into my rest.)
Ni kama vile nilivyoapa katika hasira yangu: hawataiingia raha yangu.”
12 Take heed, brethren, lest there be in any of you an evil heart of unbelief, in departing from the living God.
Muwe waangalifu, ndugu, ili kwamba usije ukawepo moyo mwovu wa kutokuamini kwa mmoja wenu, moyo ambao utakwenda mbali na Mungu aliye hai.
13 But exhort one another daily, while it is called To day; lest any of you be hardened through the deceitfulness of sin.
Badala yake, mhamasishane kila siku kila mmoja na mwenzie, ili kila iitwapo leo mtamani, ili kwamba mmoja kati yenu asifanywe kuwa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
14 For we are made partakers of Christ, if we hold the beginning of our confidence steadfast unto the end;
Kwa maana tumekuwa washiriki wa Kristo ikiwa tutashikamana na uthabiti wetu kwa nguvu katika yeye kutoka mwanzo hadi mwisho.
15 While it is said, To day if all of you will hear his voice, harden not your hearts, as in the provocation.
Kuhusu hili imekwisha kusemwa, “Leo kama mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu, kama Waisraeli walivyofanya wakati wa uasi.”
16 For some, when they had heard, did provoke: nevertheless not all that came out of Egypt by Moses.
Ni akina nani hao waliomsikia Mungu na kuasi? Hawakuwa wale wote ambao Musa alikuwa amewaongoza kutoka Misri?
17 But with whom was he grieved forty years? was it not with them that had sinned, whose carcasses fell in the wilderness?
Na kina nani ambao Mungu aliwakasirikia kwa miaka arobaini? Siyo pamoja na wale waliotenda dhambi, ambao miili yao iliyokufa ililala jangwani?
18 And to whom swore he that they should not enter into his rest, but to them that believed not?
Ni akina nani aliowaapia Mungu kwamba hawataingia katika raha yake, kama siyo wale ambao hawakumtii yeye?
19 So we see that they could not enter in because of unbelief.
Tunaona kwamba hawakuweza kuingia katika raha yake kwa sababu ya kutokuamini.